Mnakumbuka East African Airways?

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
East+African+Airways+1.jpg


EastAfricanAirways-vi.jpg

East+african+airlines.jpg


Wadau hapo zamani za kale kulikuwa na shirika la ndege East African Airlines. Ilikuwa sehemu ya East African Community. Waliokuwa wanakmiliki ni Tanzania, Kenya na Uganda.

Mwaka 1971, familia tulisafiri Mbeya hadi Dar na ndege ya East African Airways. Ilikuwa Prop Job kama ile kwenye picha ya kati kati. Tulikuwa tunatoka kijijini Manda kwa ndugu wa baba. Mkikaa kwenye kiti kama vile mnatazama hewani, halafu ilisha ruka ndo mnakuwa sawa. Ingawa nilikuwa na miaka saba nakumbuka waliwapa aibiria lunch box. Mwaka 1976 tulisafiri na ndege 727 Nairobi -Dar. Haikuwa mbaya. Pia tulisafiri na treni, lakini jamani zilikuwa safi na wenye wahudumu waliopenda kazi yao.

Nakumbuka nikiwa Form One mwaka 1977, ghafla shirika hiyo ilivunjwa. Waliokuwa na mali (treni, ndege, mabasi) kwenye nchi yao ndo ilikuwa mali yao. Wakati ule damu ulikuwa mbaya kweli kati ya WaTanzania na WaKenya.

Mwalimu shuleni alitusimulia hivi, waKenya walivizia siku ambayo ndege kubwa na nzuri zitakuwa zimetua pale Embakasi airport Nairobi, ndo wakazizoa na kuita Kenya Airways! Tanzania tuliambulia zile Fokker Friendships na ndege nyingine 737 ikawa Air Tanzania, halafu Uganda walikuwa wazembe eti walipata ndege moja tu! Ikawa Uganda Airways.

Lakini jamani nakumbuka watu walikuwa na huzuni kubwa mno jumuiya ilivyovunjika. Mbaya zaidi watu wakawa wanyama. WaTanzania walifukuzwa Kenya kama mbwa. Hasa hao waliokuwa wanafanya kazi na East African community. Wengine walirudi Tanzania kwa mguu na begi moja!
Wenye stori za wakati ule hebu mtupashe.
 
East+African+Airways+1.jpg


EastAfricanAirways-vi.jpg

East+african+airlines.jpg


Wadau hapo zamani za kale kulikuwa na shirika la ndege East African Airlines. Ilikuwa sehemu ya East African Community. Waliokuwa wanakmiliki ni Tanzania, Kenya na Uganda.

Mwaka 1971, familia tulisafiri Mbeya hadi Dar na ndege ya East African Airways. Ilikuwa Prop Job kama ile kwenye picha ya kati kati. Tulikuwa tunatoka kijijini Manda kwa ndugu wa baba. Mkikaa kwenye kiti kama vile mnatazama hewani, halafu ilisha ruka ndo mnakuwa sawa. Ingawa nilikuwa na miaka saba nakumbuka waliwapa aibiria lunch box. Mwaka 1976 tulisafiri na ndege 727 Nairobi -Dar. Haikuwa mbaya. Pia tulisafiri na treni, lakini jamani zilikuwa safi na wenye wahudumu waliopenda kazi yao.

Nakumbuka nikiwa Form One mwaka 1977, ghafla shirika hiyo ilivunjwa. Waliokuwa na mali (treni, ndege, mabasi) kwenye nchi yao ndo ilikuwa mali yao. Wakati ule damu ulikuwa mbaya kweli kati ya WaTanzania na WaKenya.

Mwalimu shuleni alitusimulia hivi, waKenya walivizia siku ambayo ndege kubwa na nzuri zitakuwa zimetua pale Embakasi airport Nairobi, ndo wakazizoa na kuita Kenya Airways! Tanzania tuliambulia zile Fokker Friendships na ndege nyingine 737 ikawa Air Tanzania, halafu Uganda walikuwa wazembe eti walipata ndege moja tu! Ikawa Uganda Airways.

Lakini jamani nakumbuka watu walikuwa na huzuni kubwa mno jumuiya ilivyovunjika. Mbaya zaidi watu wakawa wanyama. WaTanzania walifukuzwa Kenya kama mbwa. Hasa hao waliokuwa wanafanya kazi na East African community. Wengine walirudi Tanzania kwa mguu na begi moja!
Wenye stori za wakati ule hebu mtupashe.

Mimi nina kumbukumbu sana kuhusu hili ndiyo maana hii harufu ya EAC mpya na msukumo unaotolewa na Kenya unanikera sana. Yaani viongozi wetu hawajifunzi kutokana na historia kabisa, ndio ubaya wa kuwa ni viongozi myopic. Kuna wafanyakzi wa EAC waliohangaishwa na serikali yetu kuhusu mafao yao muda wote huo hadi mwaka jana; nina imani kuna waliokufa bila kupata mafao yao.
 
..Thank You for the Memory! Hizo Ndege zinayoangalia hewani kabla ya kuruka zilikuwa Dakota 9 na yalikuwa so rugged, mandege ya kazi kiasi cha kuweza kutua hata kwenye uwanja wa mpira! I dont think they are producing them anymore. halafu angalia kichekesho. Miaka mingi iliyopita kama anavyosema mkuu kulikuwa na schedule flights kwenda Mbeya moja ya miko muhimu sana kiuchumi, saa hizi kumekuchwa ndio tunaaza kukumbuka kujenga kiwanja cha ndege ambacho hata maendeleo yake hatuambiwi! Mungu Ibariki Tanzania.
 
..Thank You for the Memory! Hizo Ndege zinayoangalia hewani kabla ya kuruka zilikuwa Dakota 9 na yalikuwa so rugged, mandege ya kazi kiasi cha kuweza kutua hata kwenye uwanja wa mpira! I dont think they are producing them anymore. halafu angalia kichekesho. Miaka mingi iliyopita kama anavyosema mkuu kulikuwa na schedule flights kwenda Mbeya moja ya miko muhimu sana kiuchumi, saa hizi kumekuchwa ndio tunaaza kukumbuka kujenga kiwanja cha ndege ambacho hata maendeleo yake hatuambiwi! Mungu Ibariki Tanzania.

Kwa taarifa nilizo nazo kwenye deski langu Kiwanja cha Ndege cha Mbeya kinafunguliwa rasmi mwezi wa 11 mwaka huu, na kazi za finalization zimepamba moto sana huko sasa....Kwa ujumla mambo mengi ya kimaendeleo ya jamii na huduma yamekuwa na tendency ya kurudi nyuma ukilinganisha na miaka ya zamani!....Fikiria treni linakwama kwa miezi 6, huku wananchi wa huko wakikwama kabisa kimaendeleo, ambapo timu ya Brazil inapokelewa kwa gharama ya 3bn!...do we have people or the likes?
 
Miaka hiyo hata sikumbuki maana hata kunusa aridhi ya dunia hii nilikuwa bado..ila hii habari imeniingia mpaka kwenye damu. PJ wewe unazifahamu habari hizi??
 
kwa habari hii kimaendeleo tumerudi nyuma....maana kama miaka ya 1970 kulikuwa na schedule za ndege kwenda mbeya na 2010 hakuna schedule basi maana yake ni kurudi nyuma.
 
kwa habari hii kimaendeleo tumerudi nyuma....maana kama miaka ya 1970 kulikuwa na schedule za ndege kwenda mbeya na 2010 hakuna schedule basi maana yake ni kurudi nyuma.
Lakini sasa tumeanza kwenda mbele ila kuna matapeli wa kisiasa wanaumia roho sana.
 
mjomba wangu zee [HASHTAG]#Buchanimanza[/HASHTAG] pita hapa utuwekee mambo sawa. maana wewe ulikuwa kiongozi wa routes hizi kabla hujajiuzulu kuitikia wito wa kumtumikia Mungu.

cc. [HASHTAG]#jessejohn[/HASHTAG]
 
Kweli ukiwa mwongo usiwe msahaulifu... hapajawahi tokea mkoa wa Mbeya kukawa na airport miaka hio
Na hata baada ya hilo shirika kuvunjika EAA lkn bado mkoa wa mbeya palikua hapana airport ya kutua ndege aina ya FOKER yenye kubeba abiria 20 hadi 30
Palikua na small airport tu ya kutua vi ndege vidogo
 
Lakini sasa tumeanza kwenda mbele ila kuna matapeli wa kisiasa wanaumia roho sana.
Tatizo lenu mbaya MTU anayewaelekeza njia nzuri zaidi ya kupita ili usije potea njia kama awali...kubalini kuelekezwa sio kila njia mpitayo ni sahihi nyny sio malaika...kama mnaakili mbona uchumi unaoza kila siku mngewasikiliza kina zitto dangote tungefika huku na bado tunazidi kudidimia kwa ubinafsi wenu...wahini kukubali kukosolewa msije kukubali tukiwa marehemu tayari
 
Heshima yako mkuu, inaonyesha ulikua wakishua haswa hahaha btw asante kwa kushare kumbukumbu nzuri kiukweli nmejifunza kitu kikubwa kuhusu EAC, pia imeniacha namaswali mengi
 
Ni kweli - Kenya walichukua ndege nyingi. Actually moja ya ndege - DC 9 - bado inafanya kazi mpaka sasa. Inamilikiwa na moja ya Kampuni binafsi ya ndege ya Kenya. Mimi niliipanda hiyo ndege miaka hiyo nikiwa mdogo; na nimeipanda tena sasa hivi - miaka hii kuanzia 2013 Mpaka 2016. Mpaka sasa iko inapiga kazi.
 
Kweli ukiwa mwongo usiwe msahaulifu... hapajawahi tokea mkoa wa Mbeya kukawa na airport miaka hio
Na hata baada ya hilo shirika kuvunjika EAA lkn bado mkoa wa mbeya palikua hapana airport ya kutua ndege aina ya FOKER yenye kubeba abiria 20 hadi 30
Palikua na small airport tu ya kutua vi ndege vidogo
Acha urongo wewe, kafanye utafiti vizuri.
 
Back
Top Bottom