Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mapenzi si pesa ingawa pesa ina nafasi kubwa katika mapenzi.
Hivi mnapokuwa mnahonga pesa, nyumba, simu, magari etc huwa mmependa na unaonesha kuwa unajali au unafanya hivyo ili upewe utamu?
Mapenzi si pesa ingawa pesa ina nafasi kubwa katika mapenzi.
Hivi mnapokuwa mnahonga pesa, nyumba, simu, magari etc huwa mmependa na unaonesha kuwa unajali au unafanya hivyo ili upewe utamu?
kumbuka mhongwaji na mhongaji wote wapo kwenye pool moja!kimoja kikikosekana basi kingine survival yake ni almost negligible!
Hivi mbona sheria haingalii rushwa hii ya kuhonga ili umege kuna kesi yeyote imewahi tokea kweli?
Mapenzi si pesa ingawa pesa ina nafasi kubwa katika mapenzi.
Hivi mnapokuwa mnahonga pesa, nyumba, simu, magari etc huwa mmependa na unaonesha kuwa unajali au unafanya hivyo ili upewe utamu?
hebu peruzi vizuri mkuu, rushwa ya ngono inatambulika kisheria bila shaka!!!!!
nikihongwa mwenzio huwa nakataa.
Mimi kuhonga huwa nachukulia kama rushwa
Unatoa rushwa ili upate kitu au huduma flani
Ile ya kuomba kazi au ufanyiwe kitu mkuu
Sasa ile rushwa au hongo kama vile wewe unatongoza si unahonga Escudo ili mtoto akubali sheria inajua hii?
ila fidel, nafikiri rushwa huwa na malengo ya papo kwa papo.
Ukija kwenye hiyo hongo mwanaume anaweza akakuhonga hata mwaka mzima huku hagusii neno lolote la maloveee.
Kuna bankteller mmoja wa kike imemkuta hiyo.
Jamaa anadeposit mamillion yake anamuachia bankteller laki 3 au 5 na yeye aingize kwenye akaunti yake. Halafu jamaa anaondoka hamuulizi hata jina huyo dada wala haombi contacts.
Halafu sio mara moja sasa.
Ninavyojua mimi na kwa kutazama kidogo baadhi ya watu, ni kuwa mara nyingi mwanaume anapohonga inatokana na mapenzi aliyo nayo kwa mwanamke na kumuonesha kuwa anamjali katika mahitaji yake.Na pia hilo ni jukumu muhimu sana kwa mwanaume katika familia na kama asipofanya hivyo ndio majina ya mwanaume suruali huanza.Lakini inapokuja kwa wenzetu wanamama anapomuhonga mwanaume,mh,hapo lazima ujiulize kuna tatizo gani?Japo ni jambo la kawaida lakini kwa wenzetu nimeshashuhudia kesi nyingi ambapo mama anahonga ili amkabidhi kijana wa watu ngwengwe,au anakuhonga lakini siku ikija zamu yako kumsaidia utakoma.