Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,356
Wapendwa waungwana wenzangu wa MMU na vitongoji vyake (Chit Chat na Mambo ya wakubwa)
Najua kuwa leo ni Ijumaa (Furahi Dei)
Najua kwamba hili si jukwaa la siasa
Najua kuwa wengi wetu mna aleji la malumbano ya kisisasa
Najua jukwaa letu pendwa hili huwa hatuna chuki wala malumbano makali ya kisiasa/kikabila wala udini
Najua hapa tunaishi kama ndugu wa familia moja
Vile vile nafahamu kuwa:
Sisi ni wahanga wa mgomo wa madaktari
Sisi ni wahanga wa yatokanayo na mgomo huo na maamuzi ya viongozi wake ambao baadhi yao tumewachagua sisi.
Sisi tunaumizwa sana na tukio hili ambalo linapoteza ndugu, jamaa, marafiki, majirani, watoto, wazazi na wapenzi wetu.
Yaani mimi ODM mimi:
Naumia sana kwa mtu mmoja kushindwa kufanya maamuzi yatakayoepusha dhahma hili
Naumia sana kwa watu wawili kushindwa kubeba dhamana ya kuwajibika kuepusha kadhia hii
Naumia sana kwa maelfu ya wataaluma wanaonewa na kudharauliwa kushindwa kutimiza majukumu yao kwa sababu ya watu wawili jumlisha mmoja.
Naumia sana kuona mamilioni ya watanzania maskini na walipa kodi kuteseka kwa sababu ya watu wachache namna hii.
Sasa naanza kuichukia nchi yangu (kama si bia ningekunywa sumu)
Eti waungwana wenzangu wa MMU (Wanatukandyaga sana hatuna time na SIHASA, msijali) Mnalionaje jambo hili? Tufanyeje sisi yailah toba??
Je Tuingie mitaani kuandamana?
Tusubiri mpaka 2015 kwa matumaini?
Tuwalambe madaktari miguu wavumilie kama sisi mpaka 2015 tufanye maamuzi magumu?
Tuhamishie kambi loliondo na kwa waganga wa jadi?
Au tutumie bia kama tiba mbadala?
Mimi bana mimi nimekasirika sana bana! Na MOD atakayeihamisha hii sredi MMU, naongozana naye lupango!.
Nikiongea kwa masikitiko toka kaunta ya juu hapa Kingstar Bar,
Ni mimi ODM wa wajukuu.
Kwa masikitiko makuu.
Najua kuwa leo ni Ijumaa (Furahi Dei)
Najua kwamba hili si jukwaa la siasa
Najua kuwa wengi wetu mna aleji la malumbano ya kisisasa
Najua jukwaa letu pendwa hili huwa hatuna chuki wala malumbano makali ya kisiasa/kikabila wala udini
Najua hapa tunaishi kama ndugu wa familia moja
Vile vile nafahamu kuwa:
Sisi ni wahanga wa mgomo wa madaktari
Sisi ni wahanga wa yatokanayo na mgomo huo na maamuzi ya viongozi wake ambao baadhi yao tumewachagua sisi.
Sisi tunaumizwa sana na tukio hili ambalo linapoteza ndugu, jamaa, marafiki, majirani, watoto, wazazi na wapenzi wetu.
Yaani mimi ODM mimi:
Naumia sana kwa mtu mmoja kushindwa kufanya maamuzi yatakayoepusha dhahma hili
Naumia sana kwa watu wawili kushindwa kubeba dhamana ya kuwajibika kuepusha kadhia hii
Naumia sana kwa maelfu ya wataaluma wanaonewa na kudharauliwa kushindwa kutimiza majukumu yao kwa sababu ya watu wawili jumlisha mmoja.
Naumia sana kuona mamilioni ya watanzania maskini na walipa kodi kuteseka kwa sababu ya watu wachache namna hii.
Sasa naanza kuichukia nchi yangu (kama si bia ningekunywa sumu)
Eti waungwana wenzangu wa MMU (Wanatukandyaga sana hatuna time na SIHASA, msijali) Mnalionaje jambo hili? Tufanyeje sisi yailah toba??
Je Tuingie mitaani kuandamana?
Tusubiri mpaka 2015 kwa matumaini?
Tuwalambe madaktari miguu wavumilie kama sisi mpaka 2015 tufanye maamuzi magumu?
Tuhamishie kambi loliondo na kwa waganga wa jadi?
Au tutumie bia kama tiba mbadala?
Mimi bana mimi nimekasirika sana bana! Na MOD atakayeihamisha hii sredi MMU, naongozana naye lupango!.
Nikiongea kwa masikitiko toka kaunta ya juu hapa Kingstar Bar,
Ni mimi ODM wa wajukuu.
Kwa masikitiko makuu.