Mmoja wa Wagombea Urais 2015 ahusishwa na Mgomo wa Madaktari?

ikionekana hoteli quality mjini- YA LOWASA
Likionekana Jengo quality mjini- YA LOWASA
Ikionekana biashara ya kulipa vizuri kiulaini - YA LOWASA
Richmond Bado ya Lowasa(Wakati kuna m2 alikuja kudai pesa zake akagoma kupigwa Picha
Madaktari wakigoma - NI LOWASA
Mgogoro ndani ya CCM- NI LOWASA

Jaribuni kuwa na Utu wa huruma

majengo siyo yote ila ana majengo yake machache na siyo uzushi, hotel nafikiri hana, biashara ya kulipa kama telecom anayo, richmond hata kama akufaidika binafsi (ilikua ya kikwete)lakini si alijua ni uozo na akaishughulikia kwa style yake ile ya kutumia nguvu zote ili ipite (na hapa ni guilty) na tukakaa gizani hili halina mjadala kuhusika kwake kupo wazi. MaDr mgomo ni moja tu ya strategy za EL za kuifanya serikali ionekane mbaya zaidi ili yeye apate points za urais anaweza kua mhusika au la lakini dhamira yake ipo kweupe kabisa kua serikali isifanye kazi yeyote na nchi isitawalike..utasikia mgomo wa walimu, na wafanya kazi wa serikali na sitoshangaa nikisikia EL anahusika
 
Sometimes huwa tunampa Lowasa Nguvu ambazo hata hastahili! Hili la Madaktari wala halikuihitaji Lowasa awaongoze Wakuu. Madaktari wanafanya kazi katika Mazingira Magumu sana. Daktari anamwandikia Mgonjwa dawa halafu Mgonjwa anamwambia Daktari kwamba hana hata senti tano sometimes Madaktari kwa UTU wao wanawapa wagonjwa Pesa ya kunua Dawa. Inafikia kipindi Daktari kabla ya kumuandikia Mgonjwa Dawa unamwangalia Economic Status yake ukiona atakuomba Pesa unamwandikia Panadol badala ya Fansida. Madaktari WAMEDHARAULIWA sana kwa Muda Mrefu,WAMETWEZWA sana kwa Muda Mrefu. No wonder Pinda mara ya kwanza alitaka kutumia Ubabe ambao umekuja kumtokea puanai. Katika Hili hata Pinda anastahili kuwajibika maana alipata Nafasi ya kusuluhisha hili ila kwa Sababu walishazoea Kusuluhisha kwa Vitisho vya Ajira matokeo yake ndiyo tumeyaoan
 
Kwa hiyo kupinga MuO na CSSC ni Udini?..lakini hukubali kupinga OIC kama ni udini isipokuwa ni uzalendo sio?..

Mkuu Huwezi Kuzungumzia UHARAMU wa MOU hala Ukaunyamazia UHAHALI wa Morogoro Muslim University (MUM) Ambayo Serikali iliwapa Waislam Pasipo hata kuingia nayo MOU yeyote. Lakini mbona sisikii Wakristo wakilalamika hilo? Mkuu Mkandara vipi Ndugu yangu?
 
Mgomo wa madaktari ulisababishwa na umangimeza uliokithiri ndani ya serikali ambapo katibu mkuu wa wizara na Mganga mkuu wa serikali ndani ya wizara walikuwa wanawachukulia "intern Doctors" kama panya. Yaani watu wamekaa miezi miwili wanachapa kazi hawalipwi mshahara, wakauliza kwa nini hawalipwi wakajibiwa utumbo. Hii ndo ikazusha yote yaliyofuatia! Sasa kama kuna watu wanataka kujizolea credit kwamba ndo walisaidia nadhani hizi ni conspiracy theories.

Kuhusisha mgomo huu na siasa za makundi za ndani ya CCM ni jambo ambalo haliwezi kuonekana kuwa la kweli kwa mtu yeyote mwenye fikra huru. Madaktari wa intern walikaa miezi miwili bila malipo! Dharau na umangimeza serikalini ni jambo la muda mrefu hasa baada ya utamaduni wa watu kuwajibika na kuwajibishwa kuondoka hasa baada ya kifo cha Mwalimu. Kuna watu ndani ya serikali wanajiona wao ndo mwanzo na mwisho na watu hawa wanataka wanyenyekewe. Mfano wa watu hawa ni hao waliotangazwa kusimamishwa!

Kama siasa za ndani ya CCM zina mchango, OK, ni kwa kulea umangimeza, ufisadi na takataka nyingine huko serikalini. Haya ni mambo ambayo wanaoyalea hawajui kuwa iko siku yatawaangusha. Na siku mambo hayo yakiwaangusha wasitafute mchawi!!

Kuhusisha mgomo huo na kitu kingine chochote ni ajabu.
 
Mungu hadhihakiwi,hizi ni mbio za sakafuni tu,kanisani kuna watu wanafikiri vizuri hatutatoa kura kwa mtu nayeonyesha wazi kuwa nia yake ni kupata mwanya wa kuiba,pesa anazomwaga kanisani hazilingani hata chembe na kipato chake,na uchaguzi ni 2015,haihitaji mjadala kujua kuwa jamaa akichukua nchi ataiba hadi uraia wetu,stail ya kutumia makanisa ni big mistake,bakora ya Mungu itamlamba yeye na watumishi walafi wote wanaosherekea mapato ya udhalimu,' Ipo njia ionekanayo njema machoni pa mtu bali mwisho wake ni mauti" Time will tell.God is always just.
 
Mkuu lisemwalo lipo maadam hawakusema ni Kardinal Pengo basi haikuwepo..Jiulize kwa nini iwe Lowassa na sio Kardinal, Anna Kilango au Sheikh Ponda!..Unasema madaktari sio cheap mbona wanadai posho na kuwaacha watu wafe - kuna U cheap zaidi ya hilo..

yes we are cheap as u think! Lakini kumbuka kwamba ilifikia hatua hospitali haziendesheki hata kwa wale wanaolipia huduma acha na wazee,watoto na wajawazito ambao kelele za kila siku huduma ni bure. Unajua kwamba lawama zote j
 
Gazeti la Dira Ya Mtanzania linamuhusisha Mh. Edward Lowassa kuwa ndio chanzo cha mgomo wa madaktari ili kumkwamisha Rais kiutendaji kwa manufaa yake ya kuusaka urais 2015. Vilevile linazidi kuripoti kwamba, Ikulu imetayarisha mipango kabambe kukabiliana naye. Licha ya Yote, inasemekana waziri huyu mku wa zamani kutokana na ukwasi wake wa kifedha, ametayarisha mipango kabambe pamoja na kutumia uwezo wake wa kifedha kuwanunua wabunge kuhasi dhidi ya mwenyekiti wa chama ambaye ndiye Rais. Hii ina maana kwamba, Lowassa anaweza kuwa Rais kabla ya 2015
Page+1.jpg

maghamba wana mambo!
 
ikionekana hoteli quality mjini- YA LOWASA
Likionekana Jengo quality mjini- YA LOWASA
Ikionekana biashara ya kulipa vizuri kiulaini - YA LOWASA
Richmond Bado ya Lowasa(Wakati kuna m2 alikuja kudai pesa zake akagoma kupigwa Picha
Madaktari wakigoma - NI LOWASA
Mgogoro ndani ya CCM- NI LOWASA

Jaribuni kuwa na Utu wa huruma

RA,EL na JK walimlipa pesa aje kugeresha waTz kwa kujifanya DOWANS yake. akawapa shart akija asipigwe picha maana utapeli wake utajajulikana akifuatiliwa.

Hao wote watatu ni BAD NEWS kwa taifa!
 
Yasemwayo yapo ili siwezi bisha....inasemekana LOWASSA anafanya juu chini kumkwamisha JK baadhi yawanamtandao wake wanathibitisha hilo....PINDA nae amekwisha lalamika kua kuna hujuma anafanyiwa na wanamtandao wa LOWASSA ili aonekane ovyo..Bungeni kashawanunua ata wale waliokua wanampinga yuwapi ANNE KILANGO kwisha nampiganaji mwingine aliekua kambi ya SITA nae ameanza kujisogeza kwa EL...LOWASSA amekua akiongoza uhasi live kwani amekua ata anapopata nafasi ya kualikwa makanisani amekua akimpiga vijembe live JK kua serikali lazima ishughulikie tatizo la ajira kwa vijana,mara serikali lazima iongeze mishahara kwa watumishi hiyi yote nikutaka kuungwa mkono kwa wasiomfahamu...LOWASSA huyuhuyu ambae ni mbunge tokea tunazaliwa mpaka sasa kwanini asitoe ushauri huo BUNGENI wa kupandishwa kwa mishahara au yeye sio ktk kundi la ndiooooooooooooo? Ni hivi majuzi tu SUMAYE ameligundua hilo kua kama JK akiendelea kucheka na hawa mafisadi nchi itamshinda kabisaaa kwani LOWASSA tiari kashaandaaa uasi ktk NEC na baadhi ya wana CCM...Jiulize migogoro ya ARUSHA ya CCM mbona yupo kimyaaa as if sio MP kutoka Mkoa huo? Wako wapi wakina BEATRICE SHELUKINDO ambao wanamtumikia EL mpaka juzi wakataka wafanye UASI ila dili lao likashitukiwa nani ambaye hakujua the source behind and why these presons only? So ata mjina atafahamu tu kua LOWASSA ana consipiracy za uhaini mpaka NEC imebidi iitishe kikao ivi karibuni.....JAMANI HIZI PESA ZA LOWASSA ZITATUUA....TUTAMKUMBUKA NYERERE
 
Bro I'm sorry! dont need your respect simply because I have to aligned with doctors claim..This kind of unsuspected interstellar law doesn't work with me so take back your respect.

Mkuu, if those doctors value their service in dollars why in the hell did they signed the contact? wewe umeshaambiwa utapewa dollar 900 kwa nini umechukua kazi ile as if value of serving life..sasa mimi au Lowassa kutokuwa madaktari ndio inamwondoa ktk kuelewa matatizo ya madaktari, halafu the same doctors ask and expect the govenment to solve their problems..hao huko walikuiwa madaktari au?

Hii akili ya Kibongo kufikiria kwamba matatizo ya daktari anayajua daktari, hivyo waziri wa Afya lazima awe daktari humuoni kama ni ujinga mkubwa kuamini admin pia inahusiana na Udaktari..U may call me names lakini haiondoi ukweli kwamba wewe daktari bingwa ulienda kuomba elimu ukapewa bure kisha ukaambiwa kazi yako malipo ya mshahara wako ni huu, hali yetu ktk hospitali zetu ni hizi na unajua matatizo yote kabla hujaingiza mguu wako, ukubali na kuweka saini kukubali mashatri hayo... Umefanya kazi huoni mafao jikate!...Badala ya kupanga kwa pamoja walk out ungeweza kabisa kwenda kutafuta kazi private Hospitals au kuacha profession hiyo mbona sisi tumeacha profession zetu tunabeba mabox? ndio Ubepari huo mkuu wangu. Mbebwe kwa sababu ati mmesoma!

Kibaya zaidi hamuwezi kushinikizwa kuwaacha wagonjwa kama humanshield ili matakwa yenu yasiklilizwe hii sio Iraq wala Afghanstan. Mnaua watu makusiudi kwa sababu mnadai haki zenu wakati mahakama zipo, bunge lipo, rais yupo kwa nini msiingia Ikulu bila kualikwa.. na tumewasikia toka mwanzo mkibadilisha madai kila siku pale mnapoona mnakosea mnarekebisha kesho. Mwanzo wa madai yenu ilikuwa posho za vikao kama wabunge, tulipowasema mkabadilisha kuwa hali ya kazi.. Wewe mwajiriwa hutaki mazingira hayo acha lakini sio kumwacha mgonjwa asitibiwe. Nimefiwa na jamaa yangu kutokana na mgomo huu hivyo hata wewe hujui uchungu wa kuondokewa na jamaa yako wakati angeweza kabisa kuponeshwa ati sababu ya kudai haki yako! siwaungi mkono nyie wala hiyo serikali maana nyote mnachokitaka ni kodi ya mwananchi kuingia mifukoni mwenu.
Hii ni nooo! noo! huwezi kuyarudisha maisha yake kwa thamani yoyote ya fedha inayoipata.. Mkuu niheshimu usiniheshimu hainipunguzii kitu.
Huwa unanishangaza sana na arguments zako kuhusu doctors and their just ended strike.......sometimes its intolerable not to answer you...because you are always disgracing Drs....what can i say simply.....Wewe uliacha profession yako ukakimbilia canada kubeba box.....kama we mzalendo wa kweli mbona hukubaki uipiganie na kuitetea profession yako????waache madaktari bana vipi we!!wao madaktari pamoja na mazingira na maslahi duni wamebaki TZ wakifanya kazi kwa profession zao(kutibu)leo wanadai haki zao na kutetea fani yao we yakuumia nini????we umeona kukimbia profession yako na kubeba mabox ng'ambo ndio uzalendo kwa nchi yako???what the hell are you talking bwana ah!!waache watu wenye akili zao watetee fani zao bwana,we endelea kubeba mabox na kupiga siasa za fimbo ya mbali haiui nyoka.......come back to TZ and face the reality brother ndo uweze kutukana watu na profession zao......
 
Tutasingizia Lowassa leo, kesho tutasema Dr Slaa, ni ukweli masilahi ya watumishi yapo chini, mimi nawapongeza madaktari wame subutu, hao waheshiwa tuwaache, karne ya leo siyo ya kupelekwa pelekwa 2015 tufanye maamuzi sahihi.
 
Mkuu Huwezi Kuzungumzia UHARAMU wa MOU hala Ukaunyamazia UHAHALI wa Morogoro Muslim University (MUM) Ambayo Serikali iliwapa Waislam Pasipo hata kuingia nayo MOU yeyote. Lakini mbona sisikii Wakristo wakilalamika hilo? Mkuu Mkandara vipi Ndugu yangu?
Mkuu hapa tunazungumzia tatizo la AFYA na mgomo wa madaktari. Sikuandika lolote kuhusu MuO hadi mjinga mmoja alipoandika kwamba sina lolote kumlalamikia Lowasssa isipokuwa vita yangu ni MuO. Kuna ukweli ambao nimeeleza ktk mada nyinginezo lakini wamenivuta huku ili tu waonyeshe nina chuki na Wakristu japokuwa lengo langu ni kuzungumzia Udini ulovyoshamiri Tanzania.

Tatizo langu ni Lowassa na kweli napinga muafaka wa MoU, au mfumo mzima wa Elimu na Afya nchini, hivyo kwa serikali kuwazawadia waislaam chuo huoni aibu hata kusema hivyo... yaani waislaam wamepewa chuo ili iweje? kama sii kufuta aibu ya kuonyesha kuna uuwiano fulani tk maamuzin yao jambo ambalo halikutakiwa kuwepo toka mwanzo..Nambie wewe kwa nini rais Mkapa aliwazawadia waislaam chuo kama sii kutokana na kelele zao kuhusu muafaka wa MuO..na mijinga ile ikakubali kwa sababu wao wenyewe wanataka utengano kutokana na udini waliokuwa nao. Kwa hali iliyopo kanisa wasiporidhika na ruzuku watawashawishi wananchi wapingane na mgombea na waislaam vile vile wanatumia fursa hizi kumchagua kiongozi.. Je, hamuoni kama tunatenganishwa?..

Mimi nataka mfumo mzima wa ELIMU na AFYA uwe chini ya serikali yenyewe kutoa huduma kwa wananchi na sii ubia baina ya serikali na vyombo vya dini ambavyo vinaweza ku lobby na hata kusababisha uchaguzi wa kiongozi kutokana na interest zao. Leo hii ubia baina ya serikali na kanisa unachangia sana ktk migogoro inayotokea na Lowassa anatumiwa, hilo ninalo hakika sasa huyu jamaa kama hakubali kwa sababu nazungumzia dini yake na abakie hivyo...Hakuna tofauti na Muafaka wa CCM na CUF ambao una lengo moja tu la kuwatuliza Wazanzibar wakati CCM pamoja nakutokubalika Zanzibar waendelee kutawala..

Lakini ajabu ni kwamba mkristu huyo huyo ukimuuliza kuhusu muafaka wa CCM na CUF anayaona mabaya yake lakini inapofikia muafaka wa MuO na CSSC hakubali sawa na Mzanzibar mfuasi wa CUF. Lakini ukitazama nje ya box utagundua kwamba CCM inatuchezea akili sisi wote, na wale wanaoshangilia haya ni wabinafsi toka mwanzon maana sioni sababu kabisa ya kusea CSSC inafanya kazi vizuri hali tumeona mgomo kama huu na matokeo ya shule. Katika mahesabu yao walichotaka kuonyesha ni ubovu wa serikali ya JK ktk kitu ambacho wamekishika wao..

Je, Lowassa ana mkono ndani ya mgogoro wa Madaktari?.. hizi ni taarifa zilizosambaa mapema hata kabla mgomo wenyewe. Ikiwa tatizo lilikuwa toka wizarani, madaktari wangeweza kumwona PM, bunge, mahakama na hata rais maana alitembelea Muhimbili wala haikuwa muda mrefu ulopita. Na zaidi ya hapo kuna wabunge kama marehemu alifikia hata kukusanya kero za wananchi, hii inaonyesha zilikuwepo njiia nyingi sana za kufikisha malalamiko yao kabla ya kuanza mgomo ambao walisubiri JK meondoka nchini.. Wee nambie kuna mtu hapa JF alijua lolote kuhusu madaktari hawa kuanzisha mgomo?

Hata Chadema walienda kutaka kujua shida zao ina maana hakuna mbunge aliyejua matatizo yao kabla ya mgomo.. kwa nini ilikuwa siri ikiwa hawajalipwa mshahara miezi miwili?..tungesikia kwanza madai yakiendeshwa halafu ndio mgomo lakini ghafla tu bin vuuu mgomo huo!..na wakidai Posho baada ya wabunge kupewa posho, leo wanageuka na kusema hadithi nyingine kibao.


Mkuu wangu sisi wote tunaupinga utawala wa JK na CCM lakini wanapotokea watu kuanza kutumiwa na hawa jamaa inabidi tuzungumze ukweli na kwa bahati mbaya sana mimi huandika vitu ambavyo watu hawapendi kuvisoma japokuwa ni ukweli kwa sababu wengi wao ni WANAFIKI... Hivyo hainipi taabu kabisa maadam ujumbe wangu umefika... na wanafiki wanatukana kwa kila matusi wayajuayo kwa sababu nimewagusa. Kama sii kweli haya matusi yote ya nini wakati wanajua jambo niloandika halina ukweli?..
 
Huwa unanishangaza sana na arguments zako kuhusu doctors and their just ended strike.......sometimes its intolerable not to answer you...because you are always disgracing Drs....what can i say simply.....Wewe uliacha profession yako ukakimbilia canada kubeba box.....kama we mzalendo wa kweli mbona hukubaki uipiganie na kuitetea profession yako????waache madaktari bana vipi we!!wao madaktari pamoja na mazingira na maslahi duni wamebaki TZ wakifanya kazi kwa profession zao(kutibu)leo wanadai haki zao na kutetea fani yao we yakuumia nini????we umeona kukimbia profession yako na kubeba mabox ng'ambo ndio uzalendo kwa nchi yako???what the hell are you talking bwana ah!!waache watu wenye akili zao watetee fani zao bwana,we endelea kubeba mabox na kupiga siasa za fimbo ya mbali haiui nyoka.......come back to TZ and face the reality brother ndo uweze kutukana watu na profession zao......
Hii ni dunia ya Utandawazi mkuu wangu unaitafuta riziki sehemu zote inapopatikana. Elimu niliyosoma ni kunisaidia mimi kupambanua vitu na sii kutafutia ajira. Nilisoma sii kutafuta ajira, wewe ndio umesoma ili uajiriwe kutokana na zile siasa za Ujamaa na Kujitegemea. Namshukuru mungu nabeba box kazi ambayo imenifundisha mengi nje kabisa tena toka chini na kuongeza ujuzi wa kazi zaidi ya moja..
 
Tutasingizia Lowassa leo, kesho tutasema Dr Slaa, ni ukweli masilahi ya watumishi yapo chini, mimi nawapongeza madaktari wame subutu, hao waheshiwa tuwaache, karne ya leo siyo ya kupelekwa pelekwa 2015 tufanye maamuzi sahihi.

Kwa hiyo tunaserikali ngapi?
 
Hivi Mhariri wa DIRA kweli amefanya udadisi wa kutosha kabla ya kuruhusu kuchapwa kwa habari hiyo? Isijekuwa ni habari imedakwa toka kwenye mitandao na Mwandishi akaichukua kichwa2 na kumpelekea Mahariri kwa mbwembwe ili ipambe na kuuza gazeti lake? Kesho tusisikie amefikishwa mbele ya Kamati ya Maadili ya MCT na kutakiwa kuomba radhi mara lukuki vinginevyo DIRA limlipe Bwana Mamvi mabilioni ya hela ya madafu.

imwan
 
Hivi Mhariri wa DIRA kweli amefanya udadisi wa kutosha kabla ya kuruhusu kuchapwa kwa habari hiyo? Isijekuwa ni habari imedakwa toka kwenye mitandao na Mwandishi akaichukua kichwa2 na kumpelekea Mahariri kwa mbwembwe ili ipambe na kuuza gazeti lake? Kesho tusisikie amefikishwa mbele ya Kamati ya Maadili ya MCT na kutakiwa kuomba radhi mara lukuki vinginevyo DIRA limlipe Bwana Mamvi mabilioni ya hela ya madafu.

imwan
Mkuu jiulize Lowassa ni mbunge tu hana nafasi yoyote ndani ya serikali yetu, kwa nini hadi leo anakuwa na sauti kubwa na mkono kila mahala. halafu watu mnakubali kwamba Lowassa anautafuta urais kwa njia zote iweje asijihusishe na maswala mazito kama haya lakini wepesi kukubali Sitta, Membe au Dr.Slaa wanapojaribu kujipanga wao inakuwa ni makosa na utasikia muda wa propaganda za uchaguzi bado..

Jamani Tanzania yetu hakuna siri, watu ni wanafiki na hawaaminiki na wapo jamaa wanachukua bila kuficha toka kwa Lowassa na wanajisifiwa kwamba serikali haiwezi kuwafanya kitu as long as Lowassa yupo..Hawa husema mambo hata kabla hayajatokea na kama wewe daktari na hukubali taarifa kama hizi ina maana haupo ktk payroll umefuata mkumbo tu japokuwa madai umeyaona ni ya msingi.
Na wanasema wazi JK hawezi kumfanya kitu EL, kesha wekwa mfukoni na kuna serikali mbili zinatuendesha sasa hivi, ni chaguo lako! sasa mnachotetea hapa ni kutoelewa siasa za Bongo. Nashukuru sana Pasco aliweza kunifumbua macho ktk ile mada ya EL rais wa 2015 tujipange naye hapo ndipo nilipogundua mengi na ya kusikitisha taifa letu linapoelekea...
 
siasa za bongo bwana,full propaganda..sisi tuligoma kutokana na upumbavu wa wateuliwa wa baba mwanaasha,mambo ya lowasa yanaingiaje??
 
Back
Top Bottom