Mmiliki Palm beach kumburuza Tibaijuka

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Mmiliki Palm beach kumburuza Tibaijuka
Wednesday, 22 December 2010 20:24

Nora Damian
MMILIKI wa kiwanja kilicho jirani na Hoteli ya Palm Beach ambacho ukuta wake umevunjwa, Taher Muccadam, amesema anarudi tena mahakamani kudai fidia na atahakikisha haki yake inatambuliwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Muccadam alisema amesikitishwa na kitendo hicho, kwani yeye ni mmiliki halali wa kiwanja hicho.

“Makucha aliyoyaonyesha Waziri (Anna) Tibaijuka ni dharau kubwa kwa amri iliyotolewa na Mahakama, sisi tulitegemea yeye angekuwa mstari wa mbele kufuata na kusimamia sheria,” alisema Muccadam na kuongeza kuwa:
“Kama hakuridhika na maamuzi ya Mahakama Kuu, angerudi mahakamani kuomba mahakama itengue uamuzi wake sio kunyata na kuvizia muda wa usiku kuvunja sheria.”

Mmiliki huyo alisema, kitendo hicho kimedhalilisha majaji, mahakimu na wananchi kwani, hawatakuwa na imani na mahakama katika utoaji haki.
Alisema anaamini atakaporudi mahakamani haki itatendeka na atalipwa fidia kutokana na uamuzi uliofanywa na serikali.
Muccadam alinukuu kifungu namba 107 cha Katiba, ambacho kinazungumzia utoaji haki na kusema, Waziri Tibaijuka amedharau na amepiga teke katiba ya nchi aliyoapa kuilinda.

“Katiba ya Jamuhuri ya Muungano inasema, mamlaka ya utoaji haki itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya Mahakama Zanzibar na kwa hiyo hakuna chombo cha serikali wala Bunge au Baraza la Wawakilishi kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki,” alisema Muccadam akinukuu kifungu hicho.

Alisema alipewa vibali vya kujenga uzio na jingo la ghorofa kumi baada ya kufuata taratibu.
Juzi usiku, serikali ilivunja uzio uliokuwa umejengwa katika kiwanja hicho na uzio mwingine uliojengwa jirani na Hospitali ya Aga Khan.
Kazi ya kuvunja ukuta huo ilifanywa majira ya saa 1:00 usiku na tingatinga la Halmashauri ya Manispaa ya Ilala chini ya ulinzi mkali.

Mmiliki huyo tayari alikuwa ametoa notisi ya siku saba kwa Profesa Tibaijuka kumtaka amuombe radhi na kumlipa fidia ya Sh2 bilioni kwa madai kuwa, amemdhalilisha kwa kusema alikipata kiwanja hicho kwa njia ya rushwa.
Kiwanja hicho namba 1006 kilicho Upanga jirani na Hoteli ya Palm Beach, ni kati ya viwanja ambavyo Profesa Tibaijuka alisema maeneo ya wazi na kwamba haviruhusiwi kuwa makazi.

Kwa mujibu wa Muccadam, kiwanja hicho kilikuwa kinamilikiwa kwa hati namba 186164/25 iliyotolewa Januari Mosi, 1975 kwa wamiliki wa kwanza ambao ni Shantaben Narottambahi Patel na Nilaben Girishumar Patel.
Alisema kiwanja hicho kilimilikishwa na Manispaa ya Ilala na miliki hiyo ilidumu kwa miaka 99, kabla yeye hajakinunua mwaka 2000.
 
"Katiba ya Jamuhuri ya Muungano inasema, mamlaka ya utoaji haki itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya Mahakama Zanzibar na kwa hiyo hakuna chombo cha serikali wala Bunge au Baraza la Wawakilishi kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki," alisema Muccadam akinukuu kifungu hicho.

Yeye akadai fidia lakini katiba hiyo hiyo imemwezesha Raisi wa Jamhuri ya Muungano kuwa ni mmiliki wa Ardhi yote kwa niaba ya nchi hii. Hivyo kama anaweza kukupa kiwanja anaweza kukunyang'anya ili mraadi akulipe fidia na ndivyo sheria ya ardhi isemavyo..................kwa hiyo suala la kuwa yeye ndiye mmiliki halali wa kiwanja hicho halina msingi wa kisheria.....................
 
Yeye akadai fidia lakini katiba hiyo hiyo imemwezesha Raisi wa Jamhuri ya Muungano kuwa ni mmiliki wa Ardhi yote kwa niaba ya nchi hii. Hivyo kama anaweza kukupa kiwanja anaweza kukunyang'anya ili mraadi akulipe fidia na ndivyo sheria ya ardhi isemavyo..................kwa hiyo suala la kuwa yeye ndiye mmiliki halali wa kiwanja hicho halina msingi wa kisheria.....................

Kama hajui amuulize aliyekuwa mmiliki wa Drive In Cinema
 
kama serikali imeweza kutumia machinery zake kuwadhulumu wananchi walio wengi haki zao iweje ishindwe kutumia machinery hizo hizo kwa kumdhulumu individual

Teh Teh
 
Mmiliki Palm Beach kurudi mahakamani


Na Grace Michael

SIKU moja baada ya kutekelezwa kwa agizo la Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka la kuvunja uzio uliowekwa katika eneo la wazi kwenye kiwanja namba 1006 kilichopo Palm Beach, Dar es Salaam, anayedai
mmiliki wa eneo hilo, Bw. Taher Muccadam ameendelea kuweka msimamo wake wa kurudi mahakamani.

Bw. Muccadam ambaye kabla ya kuvunjwa kwa ukuta huo alijigamba kumburuta mahakamani, Prof. Tibaijuka kwa madai kuwa kutekelezwa kwa agizo lake ni ukiukwaji wa amri ambayo iliwahi kutolewa na mahakama kuwa yeye ndiye mmiliki wa eneo hilo.

Hata hivyo, wakati akijigamba kwenda mahakamani, waziri huyo alimjibu kwa kusisitiza msimamo wake wa kutekeleza agizo alilolitoa wakati akitembelea maeneo ya wazi ya jiji la Dar es Salaam Desemba 14, mwaka huu, kuwa lazima maeneo hayo yaachwe na kuwekwa bustani, ili kila Mtanzania aweze kufurahia.

"Mahakama zipo kwa ajili ya watu wote, hata serikali nayo pia inaweza ikashtakiwa, hivyo kama ana vielelezo vya kiwanja hicho na kama anayo hati ya kiwanja hicho awahi mahakamani tutakutana. Sikukurupuka kufanya hayo maamuzi kwa kuwa nimepitia faili la kiwanja hicho na kama anayo hati basi ni feki," alikaririwa Prof. Tibaijuka wakati akizungumza na Majira kuhusu kusudio la mlalamikaji huyo la kwenda mahakamani.

Akizungumza jana na Majira, Bw. Muccadam alisema kuwa kuvunjwa kwa ukuta katika kiwanja chake ni kielelezo cha kutoheshimiwa kwa amri zinazotolewa na mahakama, hivyo anatarajia kurejea huko kwa ajili ya kutafuta haki ya kiwanja chake.

"Nitakwenda mahakamani kwa ajili ya kudai fidia...nilimilikishwa kiwanja hicho kihalali na nilikuwa na kibali cha kujenga jengo la gorofa 10 hivyo makucha aliyoonesha Tibaijuka ni kudharau mhimili wa mahakama," alisema Bw. Muccadam.

Mbali na hilo pia alilalamikia hatua ya kuvunjwa kwa ukuta huo nyakati za usiku lalamiko ambalo linazua maswali mengi kwa kuwa ukuta huo nao unadaiwa kujengwa usiku kama ulivyovunjwa.Katika ziara ya Prof. Tibaijuka alimuru pia kuvunjwa kwa uzio uliojengwa katika eneo la wazi lililopo Ocean Road lakini pia alisisitiza kuwa hakuna mtu atakayeweza kutumia maeneo nje ya matumizi yanayoonekana ndani ya ramani.

Historia ya eneo la Palm Beach ilionesha kuwa mgogoro huo ulifikia hatua ya kufikishwa mahakamani lakini awali kilibatilishwa rasmi na Rais Mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa mwaka 2002 na kufutwa umiliki wa hati ya kiwanja hicho na kuwa katika matumizi ya umma.

Hata hivyo, baada ya kutekelezwa kwa amri ya Waziri Tibaijuka wananchi wameridhishwa na hatua hiyo na kuwataka watendaji mbalimbali ndani ya wizara hiyo kumpa ushirikiano wa kutosha ili aweze kutimiza malengo yake na kuifanya ardhi kutumika kama ilivyokusudiwa.

 
Back
Top Bottom