Mmemsikia Kikwete......?!

Wa mmoja

Member
Aug 4, 2009
99
0
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?
 
kwani nchi zilizoendelea wanafanya nini? Watu wanakufa saana. Zichukuliwe hatua sasa. Vyuo binafsi vimeshindwa kusomesha madereva, labda serikali iboreshe VETA na watu wakasome huko. Suala la kunyang'anya leseni ni jema kabisa kuna watu wanaamka mayatima kwa sababu ya uzembe wa mtu mmoja, miundo mbinu inaharibiwa, watu wanapata ulemavu, insurance company zinafilisika. No way lazima kupambana na madereva na ikibidi wanyang'anywe leseni
 
Last edited:
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?

Na anayeingiza nchi kwenye mikataba mibovu inayoumiza mamilioni ya wananchi je afanywe nini, au amefanywa nini?

Je kuna Dereva anaepanga kuua kwa kudhamiria?
Lakini mambo ya kifisadi yote yanapangwa vizuuri mezani, watu wanabipiana wee, hadi wakubaliane dau! , je wao wafanyweje?

Mi nakwambia, sheria hizi za jinai zinawalenga watu wadogo!

Hiyo ndo jino kwa jino au tit for tat kwa watu wa hali ya chini!

Shauri zenu, chekeni nae!
 
Kwani ukisikia kazi nyingine unadhani ni ujambazi tu? Watu wanaweza kwenda kufanya kazi nyingine nje ya ujambazi. Huyo anaeacha udereva anaenda kuwa jambazi ujue hata kabla hiyo kazi alikuwa anaifanya au alikuwa anataka kuifanya.

Hatuwezi kuendelea kuvumilia watu wanaangamia kwa ajali kila kukicha. Madereva ni moja ya sababu za ajali na wadhibitiwe.
 
Na anayeingiza nchi kwenye mikataba mibovu inayoumiza mamilioni ya wananchi je afanywe nini, au amefanywa nini?

Je kuna Dereva anaepanga kuua kwa kudhamiria?
Lakini mambo ya kifisadi yote yanapangwa vizuuri mezani, watu wanabipiana wee, hadi wakubaliane dau! , je wao wafanyweje?

Mi nakwambia, sheria hizi za jinai zinawalenga watu wadogo!

Hiyo ndo jino kwa jino au tit for tat kwa watu wa hali ya chini!

Shauri zenu, chekeni nae!

Ni kweli ndugu yangu mbona watuhumiw wa richmond anawachekea tu? Kwa nini asiwanyang'anye leseni ya kazi (kuwafukuza kazi)? Niliwahi kutembelea Norway lakini cha ajabu wakati nasafiri kwenye basi dereva alikuwa ana hakikisha havuki speed 80km/hr na wala hatukuwa na askari ktk basi. Nilimuuliza nilipofika kwa nini hawezi kwenda zaidi ya speed hiyo akasema gharama atakayolipa akikamatwa ni kubwa bora achelewe njiani.

Sisi hapa TZ tunachekesha tu eti utakuta traffic pollice wapo kwenye basi kumdhibiti dereva, huu ni ujinga!! weka sheria kwamba "over speedig faini yake ni US $ 500 na kunyang'anywa leseni" uone kama mtu atathubutu. Kwa sababu Norway kwa mwaka 2007, faini ilikuwa NOK 300 na kunyang'anywa leseni.
 
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?


Mimi kwa mawazo yangu hii imekaa sawa ila sasa kusema kwamba wakafanye kazi nyingine ina maana wanakuwa hawanamashtaka ama hapa sijaelewa vilevile nafikiri kumyang'anya mtu leseni naona ni poa zaidi na kama ndio wataingia kwenye ujambazi basi polisi wafanye kazi yao.
 
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?

Hata ikiwezekana nani wa kusimamia hiyo sheria?....naamini kabisa sheria zilizopo zikisimamiwa kwa ukamilifu hii itapungua kwa silimia kubwa sana....

mpaka siku siasa itakapo acha kuingilia kila jambo ndo tutaona maendeleo...vinginevyo kufa kama kawaida tu....kisha gov itatoa rambi rambi.
 
Hapa ni kuvifuta vyuo vya udereva na kuanzisha kitengo cha udereva ndani ya TANROADS kiwe na examiners wao waliobobea.

Polisi isijihusishe na utoaji wa leseni bali leseni itolewe chini ya uangalizi mkubwa wa Mamlaka ya barabara ambao ni Tanroads. Kwa hiyo TANROADS iwe ni mamlaka moja yenye mtandao mkubwa kwani barabara zinajengwa na wao na ndo watakaoweza kujua thamani za ujenzi wa bara*2. Na leseni ziwe za kutambulika kwa komputer ziwe za kadi.

Polisi tutakutana nao kwenye ukaguzi na kunyanganyana hizo leseni barabarani.

Mheshimiwa JK kama tunaweza kugharamia vitambulisho vya taifa je ni hizo leseni ambazo kila mtu atalazimika kulipia ndiyo aipate??
 
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?

Huku ndiyo kufanya maamuzi ya juu juu yale yale ya uswahili. Kwanza inatakiwa kuangalia pande zote, sababu na uawezekano gani upo wa ku-monitor tabia za madereva wanapokuwa barabarani. 1. Kuna haja ya kuhakikisha kuwa watoa leseni wanazitoa baada ya kuridhika kuwa dereva amepata mafunzo ya kutosha na anapata leseni yenye uzito wake.
2. Polisi wa barabarani wanatakiwa nao wawajibishwe kuwa wamechukua hatua gani za kuhakikisha madereva wanakuwa "monitored" ili kupunguza hizi ajali
3. Ndipo adhabu kali iwekwe ikiambatana na kushitakiwa, kufungwa na kunyanganywa leseni ya kuendesha magari ya abiria. Aachiwe ya kuendesha tractor tu au lori kutegemeana na uamuzi wa mahakama.

Lakini muhimu zaidi ya yote ni kuhakikisha kuwa wanapata mafunzo ya kutosha na motisha iwe ni kupanda kiwango na mishahara kutokana na takwimu ya miaka ya kazi na namba ya abiria-kms aliobeba na kutembea. Maamuzi ya juu juu hayatatui matatizo kwenye jamii. Hii inaonekana kama ni wazo lilitokea kwenye mazishi ya aliyekumbwa na mauti kwenye ajali.
 
Kasema kweli madereva wanajifanya wako juu ya sheria wanastaili kupewa adhabu kali sana nakumbuka hapa DSM pale mahakama ya kivukoni kulikuwa na hakimu ambaye yeye kila mwenye kosa la barabarani alimfunga mwezi mpaka mitatu mbona alipunguza sana ajali hapa dar
 
Last edited:
Ni kweli ndugu yangu mbona watuhumiw wa richmond anawachekea tu? Kwa nini asiwanyang'anye leseni ya kazi (kuwafukuza kazi)? Niliwahi kutembelea Norway lakini cha ajabu wakati nasafiri kwenye basi dereva alikuwa ana hakikisha havuki speed 80km/hr na wala hatukuwa na askari ktk basi. Nilimuuliza nilipofika kwa nini hawezi kwenda zaidi ya speed hiyo akasema gharama atakayolipa akikamatwa ni kubwa bora achelewe njiani.

Sisi hapa TZ tunachekesha tu eti utakuta traffic pollice wapo kwenye basi kumdhibiti dereva, huu ni ujinga!! weka sheria kwamba "over speedig faini yake ni US $ 500 na kunyang'anywa leseni" uone kama mtu atathubutu. Kwa sababu Norway kwa mwaka 2007, faini ilikuwa NOK 300 na kunyang'anywa leseni.

Tatizo lingine linakuja kwamba hawa hawa madereva nasikia huwa wanapewa allowance na maboss wao kama watalifikisha gari mapema na lifike salama...!This means that,dereva atashawishika kulikimbiza gari ili mradi afike mapema ili apate allowance.
Sasa hii si inachangia kuongezeka kwa ajali?
 
Ni kweli ndugu yangu mbona watuhumiw wa richmond anawachekea tu? Kwa nini asiwanyang'anye leseni ya kazi (kuwafukuza kazi)? Niliwahi kutembelea Norway lakini cha ajabu wakati nasafiri kwenye basi dereva alikuwa ana hakikisha havuki speed 80km/hr na wala hatukuwa na askari ktk basi. Nilimuuliza nilipofika kwa nini hawezi kwenda zaidi ya speed hiyo akasema gharama atakayolipa akikamatwa ni kubwa bora achelewe njiani.

Sisi hapa TZ tunachekesha tu eti utakuta traffic pollice wapo kwenye basi kumdhibiti dereva, huu ni ujinga!! weka sheria kwamba "over speedig faini yake ni US $ 500 na kunyang'anywa leseni" uone kama mtu atathubutu. Kwa sababu Norway kwa mwaka 2007, faini ilikuwa NOK 300 na kunyang'anywa leseni.

Nilitembelea Poland Warsaw, ni kwamba ukifanya kosa hasa la uendeshaji mmbovu ( over speed limit) ukapata ajali au kamera ikakupiga utakapokea barua kutoka posta, hukumu zilishatolewa na zilishaandikwa vitabuni wewe cha kufanya unatangulia magereza kwa kuhudhuria kifungo chako jela na jina lako tayari lilishakutangulia mwanangu.

Kwa Australia, kwanza unajidhalilisha pili, unalipa faini ya dola kuanzia 200 hadi 1000 average.

Huwa kuna matatu kwa wakati mmoja-unaporwa leseni, unalipa faini na unatumikia jela kwa muda wa mwaka mmoja na ukitoka haurhusiwi kuendesha gari ya aina yoyote ile baada ya kutoka jela kwa muda miezi sita hadi mwaka. Hata kama umeipata leseni ile na huwezi kuipata kwani you are rrecorded.

Dereva wa basi wanaheshimika sana ni kazi nzuri mno wanavyosema, they are enjoying alot wanawapenda abiria wao, wanawasalimia wanapoingia kwenye basi mwanangu utafurahi.Wanamnyenyekea abiria aje tena asafiri kwa basi, asipande ndege au treni.

Walahi bongo bus drivers ana wenge la kufa mtu, hasira matusi, anatukana duu! nimechoka!
 
jamani kwani ulaya wanafanya nini ukisababisha ajari mara tau. wanakunyanganya leseni ambayo ni ghali sana kuipata, uanrudi chuo kuisotea tena wakiwa na maanaa kuwa inawezekana ukawa hujafahamu baadhi ya sheria. hiyo itapunguza sana ajari. tusichanganye makosa, na kusema kwa sababu kosa fulani limetendeka basi menigine yote yatatuliwe kwa njia moja. sio kweli, yanayowezekana, kwa wakati tulionao tuyafanyie kazi leo, kama hili.
 
Ni wakati upi kauli za JK zilishawahi kutekelezwa? Hiyo ni funika kombe mwanaharamu apite... Kwani taztizo la ajali za barabarani ni Madereva tu? Haya mabasi mbona yana ratiba kabisa zimepangwa kwamba kutoka kituo "A" mpaka kituo "B" ni muda "t". Mona haya magari yote yamewekewa "stcikers" kwamba yanastahili kutembea barabarani?

Hiyo kauli ni yale yale tu ya kila kukicha!
 
Wa mmoja;544440]Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria...
Hapo ndipo huwa napata shida sana. Hiyo ni kauli ya rais wa nchi mwenye dhamani ya maisha ya watu karibia milioni 40? Wanaharakati wanasema namna hiyo; PM, mawaziri na viongozi wengine wa serikali nao hivyo hivyo. Hivi nani kwenye nchi hii anaweza kutoa kauli yenye uzito sawa na dhamani aliyopewa? Asipopatikana huyo tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu!!

...kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
J...
Simple solution to complex issues! Utadhani kwamba hatujui wenzetu wanafanyaje? Tuna macho lakini hatuoni, tuna masikio lakini hatusikii..!! Sasa kwa nini tunafuja hela za umma bure kutembea huku na kule kama hatuwezi kujifunza kitu? Hii inanikumbusha katuni za "ZERO".
 
Last edited:
Huku ndiyo kufanya maamuzi ya juu juu yale yale ya uswahili. Kwanza inatakiwa kuangalia pande zote, sababu na uawezekano gani upo wa ku-monitor tabia za madereva wanapokuwa barabarani. 1. Kuna haja ya kuhakikisha kuwa watoa leseni wanazitoa baada ya kuridhika kuwa dereva amepata mafunzo ya kutosha na anapata leseni yenye uzito wake.
2. Polisi wa barabarani wanatakiwa nao wawajibishwe kuwa wamechukua hatua gani za kuhakikisha madereva wanakuwa "monitored" ili kupunguza hizi ajali
3. Ndipo adhabu kali iwekwe ikiambatana na kushitakiwa, kufungwa na kunyanganywa leseni ya kuendesha magari ya abiria. Aachiwe ya kuendesha tractor tu au lori kutegemeana na uamuzi wa mahakama.

Lakini muhimu zaidi ya yote ni kuhakikisha kuwa wanapata mafunzo ya kutosha na motisha iwe ni kupanda kiwango na mishahara kutokana na takwimu ya miaka ya kazi na namba ya abiria-kms aliobeba na kutembea. Maamuzi ya juu juu hayatatui matatizo kwenye jamii. Hii inaonekana kama ni wazo lilitokea kwenye mazishi ya aliyekumbwa na mauti kwenye ajali.

Unajua factors za ajali ni nyingi tu including kuhakikisha enforcements za sheria barabarani kwa traffic police (sio kuchukua rushwa tu na kuachia walevi nk.), pia factors zingine ni kama road designs za bongo ambazo kwenye steep condition hazi allow extra climbing lanes for slow traffic kuwesha gari zingine ku overtake badala ya kuslow smooth movement of traffic, kama ambavyo huku Southern Africa barabara nyingi wanafanya na inasaidia sana kuepuka ajali za overtaking!
 
Mheshimiwa anasema Wizara ya Miundo Mbinu ikiwezekana ibadilishe sheria kwamba dereva atayesababisha ajali na kuua abiria anyang'anywe leseni,akatafute kazi nyngne ya kufanya!!!
Jamani wana JF hii si inaweza ikaongeza majambazi nchini?
Nyi mnaionaje hii kitu?


Kuwanyang'anya leseni mimi sioni kama ni issue kubwa sana kwa dereva wa Tanzania. Sijui kama Bw JK amewahi kujiuliza hizo leseni wanazipataje maana kwa Tanzania asilimia kubwa unapata kwanza leseni alafu ndio unajifunza gari.
Nionavyo mimi sasa, hata ukichukua leseni kwa kuwa mfumo wa ufuatiliaji hauko vizuri, dereva anaweza akapata leseni nyingine na kuendesha gari kama kawaida alafu leseni haindeshi gari kwa Tanzania, gari anaendesha mtu ndio maana utakuta miji kama Dar Es Salaam watu wengi wanaendesha magari bila lesini kitu ambacho ni tofauti na miji mikubwa ya nchi nyingine.
 
Na anayeingiza nchi kwenye mikataba mibovu inayoumiza mamilioni ya wananchi je afanywe nini, au amefanywa nini?

Je kuna Dereva anaepanga kuua kwa kudhamiria?
Lakini mambo ya kifisadi yote yanapangwa vizuuri mezani, watu wanabipiana wee, hadi wakubaliane dau! , je wao wafanyweje?

BRAVO
`nyani haoni kundule`
 
We have to understand that life is unreplaceable and/or irreparable, this must be fully settle in the minds of drivers. When you cause an accident which expires life, you must understand that the one you killed is a father or mother or uncle or etc of somebody, and this person may be is the pillar of the family. By killing such a person, you have killed and distroy the whole family, in its entirety. As such, the GOV must put into place traffic laws that will be harsh to reckless drivers and insurance companies that insured the driver/car.

To my opinion, Mr. President is correct when he said whatever he said regarding drivers who are killers. Let them go and find another jobs, to wit.
 
Back
Top Bottom