Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Kijana mmoja wa kimasai Loning'o alikuwa anamsindikiza rafiki yake Seng'ata kusubiri usafiri wa kwenda Arusha mjini. wakiwa barabarani ikatokea Landrover station wagoni ikasimama na dereve akakubali kumchukua Seng'ata kwa sababu ya haraka Seng'ata akapanda garini akiwa amechukua na fimbo ya rafiki yake Loning'o na gari ilipoanza kuondoka tu akakumbuka kuwa amechukua fimbo ya rafikiye kwa hiyo alichofanya ni kurusha ile fimbo kwa kuvunja kioo cha nyuma cha gari. Dereve ikabidi asimamishe gari na kumuuliza masai vipi mbona amevunja kioo cha gari, masai akajibu " rafiki nilikuwa napeana fimbo ya Loning'o najua nilichukua kwa makosa" ...Dereve akawa mkali sasa ndio univunjie kioo cha gari??