"MLOKOLE" ananitia majaribuni!

Wana JF

Kuna dada wa 'Kilokole' ananisumbua sana. Alianza kwa kuninunulia Biblia ndogo ya mfukoni na kunishawishi niache dhehebu langu la Kikatoliki. Yeye anasema ameoneshwa katika maono kuwa napaswa kubadilika kabla ya mwaka huu kuisha na Mungu amwemwahidi 'kupanda cheo na kupata faraja' iwapo nitamkubalia ombi lake.



Kama haitoshi, kila siku lazima anitumie meseji za neno la Mungu na nyimbo za injili.

Waungwana nishaurini, nifanyeje?


Wanikumbusha rafiki yangu, kitambo kidogo. 'Jamaa hakuwa mkristo, lakini kajitupa sana kwa Mtawa (Sister), rafiki yangu kajifanya ameokoka...ikifika jumapili, Biblia ya kizungu kwapa la Right, Biblia ya Kiswahili kwapa la Left. Alipomkamata huyo Mtawa, kajaza Boli, alafu akamuoa...akarudi kwenye dini yake..Laaahhha. Akawa akijipiga kifua mbele yetu.....Shemegi yenu huyu, nilimnyanganya YESU!!!!!!, Nikakubali, kweli IBILISI ni MTU!!!!
 
Kwani haya madhehebu yaliyoanza zamani nayo si yalianzishwa na watu tu kama wa waleo !jifunze historia wewe! AU UNATAKA WAANGLIKANA wakasirike tukikumbushana hapa! Mpe ushauri mzuri! Inawezekan huyo dada ni mlokelo kweli!si wakristo wametumwa kuhubiri injili kwa mataifa yote!

Watu walioanzisha madhehebu zamani hawakuwa na malengo ya kitapeli na kugeuza imani kama biashara kama hawa wa sasa walivyo. So ishu sio kuanzisha dhehebu, ishu ni malengo ya dhehebu yanafichwa.
Pili, imani ndio hubeba maisha ya mtu. Kwanin aje mtu wa pili ageuze imani yako???!! Hao wazazi waliokulelea na imani uliyonayo unaona walikosea????!! Kwani imani aliyonayo sasa ni feki??? Una uhakika huko anakoshawishiwa aingie ndo kuna neema zaid ya huku alipo sasa??? Acha kucheza na maisha ya watu wewe!
 
Originally Posted by Jaba-li
Ndugu yangu, kubadili imani kwa ushawishi wa mtu mwingine ndio mwanzo wa kuyumba kwa mipango na mambo yako mengi ktk maisha yako, na hasa kuingia ktk madhehebu yaliyoibuka kipindi hiki. Mengi ya madhehebu haya hayana tofauti na makampuni ya biashara au magenge ya utapeli. Kama una mali unaweza kujikuta unafilisika. Watakwambia achana na mambo ya dunia (kama wale Wasabato Masalia), toa mali zako kwa mungu, yesu anakaribia kurudi. Chunga sana kijana
Hapo ni kama kufananisha katoliki na wana maombi wa father mkwera.Ila hata kama dhehebu limeanza leo sio baya ikiwa wako ndani ya neno la Mungu(Biblia)
 
Nenda naye taratibu kama kakupenda ipo siku utagundua kwa matendo yake na maneno yake.. Cha muhimu kuwa mpole ili usiharibu.

Good luck Bandugu...
 
Wana JF

Kuna dada wa 'Kilokole' ananisumbua sana. Alianza kwa kuninunulia Biblia ndogo ya mfukoni na kunishawishi niache dhehebu langu la Kikatoliki. Yeye anasema ameoneshwa katika maono kuwa napaswa kubadilika kabla ya mwaka huu kuisha na Mungu amwemwahidi 'kupanda cheo na kupata faraja' iwapo nitamkubalia ombi lake.

Kama haitoshi, kila siku lazima anitumie meseji za neno la Mungu na nyimbo za injili.

Waungwana nishaurini, nifanyeje?
Futa kwanza huo usemi wako kwenye red. Katoliki sio dhehebu bali makanisa mengine yote ya Kikristu ndio madhehebu kwa sababu yalijimega kutoka Katoliki, Kwa hiyo Kanisa katoliki sio dhehebu. Umenipata hapo?

Haya turudi kwenye mada yako.
Kwanini huyo mlokole anakufanyia hivyo? Yawezekana mwenendo wako sio mzuri ndio maana anajaribu kukuokoa,
Au la pengine amekuzimikia na ndio maana anajaribu kwa kila njia uingie laini,
Halafu sio lazima uhame dini yako umfuate yeye, au ukiona vipi aja asali katoliki kwa wale Kalismatiki(walokole wakatoliki)
 
Mkuu usitoke kundini, atakuwa amekuzimikia tu, mchape huyo nanihiii zimemzidia tu, ana hamu ya ku-do, baada ya kuchapa mlete kwenye church letu la ukweli(red color).

Hii sio Crap kabisa unajua.
Ila hilo church lenu la ukweli ambalo biblia na nyimbo za Mungu ni dhambi, na majaribu,
Lakini hio red hapo juu ndo utakatifu.
Afadhali nisiende kanisani nikasali tu mwenyewe kuliko kuingia kwene kanisa kama hilo kama lipo.

Ni mim LD
 
Futa kwanza huo usemi wako kwenye red. Katoliki sio dhehebu bali makanisa mengine yote ya Kikristu ndio madhehebu kwa sababu yalijimega kutoka Katoliki, Kwa hiyo Kanisa katoliki sio dhehebu. Umenipata hapo?

Haya turudi kwenye mada yako.
Kwanini huyo mlokole anakufanyia hivyo? Yawezekana mwenendo wako sio mzuri ndio maana anajaribu kukuokoa,
Au la pengine amekuzimikia na ndio maana anajaribu kwa kila njia uingie laini,
Halafu sio lazima uhame dini yako umfuate yeye, au ukiona vipi aja asali katoliki kwa wale Kalismatiki(walokole wakatoliki)

Aisee kashasema, biblia, nyimbo za Mungu ni majaribu kwake,
Unadhani hata hio karismatiki ina msaada kwake kweli.

Lakini tunaokolewa kwa Neema, wakati ukifika ataelewa tu.
 
wewe upo gizani naamini nia yake ni kutaka kukuweka palipo na njia ya wokovu.... Mpe nafasi mbele ya MUNGU kila kitu kinawezekana...MUngu anakupenda
 
Wanikumbusha rafiki yangu, kitambo kidogo. 'Jamaa hakuwa mkristo, lakini kajitupa sana kwa Mtawa (Sister), rafiki yangu kajifanya ameokoka...ikifika jumapili, Biblia ya kizungu kwapa la Right, Biblia ya Kiswahili kwapa la Left. Alipomkamata huyo Mtawa, kajaza Boli, alafu akamuoa...akarudi kwenye dini yake..Laaahhha. Akawa akijipiga kifua mbele yetu.....Shemegi yenu huyu, nilimnyanganya YESU!!!!!!, Nikakubali, kweli IBILISI ni MTU!!!!

mmh
 
Wana JF

Kuna dada wa 'Kilokole' ananisumbua sana. Alianza kwa kuninunulia Biblia ndogo ya mfukoni na kunishawishi niache dhehebu langu la Kikatoliki. Yeye anasema ameoneshwa katika maono kuwa napaswa kubadilika kabla ya mwaka huu kuisha na Mungu amwemwahidi 'kupanda cheo na kupata faraja' iwapo nitamkubalia ombi lake.

Kama haitoshi, kila siku lazima anitumie meseji za neno la Mungu na nyimbo za injili.

Waungwana nishaurini, nifanyeje?
majaribu hapa yako wapi?
 
Aisee kashasema, biblia, nyimbo za Mungu ni majaribu kwake,
Unadhani hata hio karismatiki ina msaada kwake kweli.

Lakini tunaokolewa kwa Neema, wakati ukifika ataelewa tu.

LD umenisingizia, wala sijasema kuwa Biblia na nyimbo ni majaribu. Mimi nina Biblia kazini, kwenye gari na nyumbani. Ninachokiona ni majaribu ni yeye kunifuata kwa mwonekano wa kunitaka kimapenzi hali akijua mimi nina mke.
 
Wana JF

Kuna dada wa 'Kilokole' ananisumbua sana. Alianza kwa kuninunulia Biblia ndogo ya mfukoni na kunishawishi niache dhehebu langu la Kikatoliki. Yeye anasema ameoneshwa katika maono kuwa napaswa kubadilika kabla ya mwaka huu kuisha na Mungu amwemwahidi 'kupanda cheo na kupata faraja' iwapo nitamkubalia ombi lake.i

Kama haitoshi, kila siku lazima anitumie meseji za neno la Mungu na nyimbo za injili.

Waungwana nishaurini, nifanyeje?


Kaka inaelekea ngono imekukaa sana taswirani oga maji baridi sana uchanjamshe akili
 
Ni mapema mno kuhukumu maamuzi yake, na pia ni fikra potofu kufikiria anakutaka kimapenzi it may be other side of the Coin.Mungu anakuhitaji sana na anaweza kutumia watumishi wake awe wa kike au wa kiume.Una bahati sana unarishwa neno na Mungu kila siku lets take positive side not always negative side.But kama ataleta za kihivyo ndo ulete mada tukushauri but as for now cjaona kibaya
 
wewe upo gizani naamini nia yake ni kutaka kukuweka palipo na njia ya wokovu.... Mpe nafasi mbele ya MUNGU kila kitu kinawezekana...MUngu anakupenda

Shindwa kabisa na ulegee. Kwani njia niliyomo ni ya motoni? Kwa nini hafanyi kwa watu wengine ambao hata si Wakristu? Ndiyo Mungu ananipenda, lakini sio kwa kupitia kwa dada huyo.
 
LD umenisingizia, wala sijasema kuwa Biblia na nyimbo ni majaribu. Mimi nina Biblia kazini, kwenye gari na nyumbani. Ninachokiona ni majaribu ni yeye kunifuata kwa mwonekano wa kunitaka kimapenzi hali akijua mimi nina mke.

Mi naona hujajieleza vizuri aisee, na kama una mke unashindwa nn kuitetea nafsi yako. Mi nlijua na wewe ni mtafutaji so umekutana na huyo kakuambia uokoke muoane, unaona majaribu. Lakini sema kweli kakuambia muache mkeo umuoe yeye?? Halafu nisamehe kwa kukusingizia.
 
Mkuu,

Itikia wito huo...
wakati wa shida utapata mtu wa kukuimbia na kukuliwaza...kwa kutumia neno la bwana.
Bora nyote wakristo hakuna tabu, jumapili moja kanisa katoliki, jumapili nyengine unaenda kanisa la dada..
Usiogope mkuu, Mungu yuko pia huko kanisani kwa dada...
Biblia na msg za neno la mungu ni zawadi nzuri, mkuu, Ushukuru sana kwa bahati uliyoipata, usone kuwa ni "usumbufu".
 
Mkuu,

Itikia wito huo...
wakati wa shida utapata mtu wa kukuimbia na kukuliwaza...kwa kutumia neno la bwana.
Bora nyote wakristo hakuna tabu, jumapili moja kanisa katoliki, jumapili nyengine unaenda kanisa la dada..
Usiogope mkuu, Mungu yuko pia huko kanisani kwa dada...
Biblia na msg za neno la mungu ni zawadi nzuri, mkuu, Ushukuru sana kwa bahati uliyoipata, usone kuwa ni "usumbufu".

Mkuu,

Mungu yupo makanisa yote, hata huko alipo yupo. Sasa ulazima wa kwenda anakosali dada ni upi? Au kuna lingine zaidi ya kusali? Akijitokeza dada mwingine wa dhehebu tofauti nako aende?? Akijitokeza mwingine na mwingine aende kote huko?? Ya nini kuhangaika huku na kule? Atulie ktk kanisa lake, na wokovu ni matendo, sio kusema tu NIMEOKOKA. Mtu anaokoka kutokana na matendo yake, na sio dhehebu lake. Hivyo hata wakatoliki wanaokoka thru matendo yao.
Kwa kumalizia nasisitiza jamaa abaki anakosali, kusoma bible, wokovu, n.k vyote atafanya akiwa RC.
 
Back
Top Bottom