Mliooa mlipata wapi wake zenu?

Kilaza Flani

Member
Oct 27, 2011
61
2
micharuko kila sehemu, ata hakuna pa kutokea!! sijui mi ndo nna gundu.. au ndo hali ilivyo ila lile neno ambalo lipo kwenye kiapo na linasisitizwa sana 'uvumilivu' linachukua nafasi yake!!
aise wake walishaisha
 
Wewe una gundu.

Jichunguze :tabia/fikra/hobbies/muelekeo wa maisha/unavyojionyesha au onekana, chunguza vigezo unavyotumia kutafuta/chagua mpenzi, chunguza matarajio yako kama yanaendana na eneo unalowinda n.k

Ningekua mwanaume na nimeoa ningekwambia pa kwenda
 
Wewe utakua ndio wale wakaka ambao hutoka na ladies, akidhania kua siku akitaka kuoa ataselect toka kwenye shelve..... Ukisahau kabisa kua wadada wa kulala nao ni wengi wa kila sampuli na kila kona; ila wale ambao ni worth it kujenga nao mahusiano ni adimu. Ukisahau kabisa kujiandaa kua walau two years before hujaoa jiandae kuanza kutafta a partner ambae utaona atafaa kua mke. Saizi unataka kuoa ndio unakuta kumbe sio lelemama wala sio mchezo, wadada wa kuoa hawapo.... wapo almost absent.... na bahati mbaya saana upo pressured by the fact kua sasa it is time. Nikwambie kweli kabisa kazi unayo, hivo brace your self.....

USHAURI.

Unataka mke wa kuoa yatakiwa umakini sababu ndoa bana is for life.... inatakiwa utulize akili na huyo mdogo wako pia umtulize na kikubwa I am genuienly telling you usimsahau kumshirikisha mwenyezi Mungu. Punguza kidogo vigezo, vya the type of woman you want,... Naamini kabisa una vigezo na kama wachukua list ya vigezo vyako kama njia ya kumpata unae ona ana qualify utakesha. Enways nakutakia kila la kheri katika kumpata....
 
Mshirikishe Mungu katika hatua hii ya kumtafuta mke wa kuoa maana mke sio nyanya ambazo unaweza kwenda soko lolote na kuchagua nyanya kwa muuzaji yyote unayekutana nae
Mke ni mtu ambaye ni muhimu sana kwako na mtu ambaye ije mvua liwepo jua usiku na mchana sometime mtakuwa wote na mtashare mengi so unatakiwa kuwa makini sana kwenye uchaguzi wako
Sio kweli kwamba wengi ni mcharuko ila may be wewe mwenyewe hujatulia na ndo maana kila unayempata anafanana na wewe
Jipe muda na tulia kwenye safari hii ya kumtafuta mwenza
 
Kilaza,

Ndugu yangu mke huwa hatafutwi, yani inatokea tu una date mtu hadi unaona mmh hapa sasa sina ujanja.

Mwenzako mimi nilikuwa nimemaliza chuo nipo kitaa sina kazi full kujirusha tuu na washikaji naanza starehe Alhamisi namaliza Jumapili na sitoki club had nisikie swalaaa swalaa lol...kipindi hiko sina hata mpango wa kuoa mtu akisema swala la ndoa namuona mshamba and thats when i met MRS Right.

Nilikuwa na mshikaji tunatoka usiku one akapigiwa simu na cousin yake binti aliyekuwa anasoma chuo Dsm akiomba twende tuka wa pick hostel coz nae alikuwa na shosti wake wangependa kwenda out. Mshikaji alichomoa,lakini nikamsihi tukawachukue after all itakuwa poa kuwa na company. That night nili dance sana na cousin yake mshikaji huku jicho langu lipo kwa shosti wake na cousin. Maana alikuwa anang'aa hadi balaa.Offcoz mshikaji alikuwa ana dance na shosti mtu ambaye ndio my waifu wangu kwa sasa. After hapo tuka date kwa takriban miaka 4 alikuwa akitaja swala la ndoa ananitibua lakini finally nikaoa huyo huyo.
 
kaka shukuru unapata kugundua kuwa wenzio unaokuwa nao sio waaminifu!! kuna watu hawakugundua hayo mapema, au waligundua ila wakalazimisha kuingia kwenye ndoa, wakazaa na kuanza maisha kwenye ndoa zao, saizi wanaonja shubiri (chungu) kwa maisha magumu ya ndoa... naomba nikutie moyo mkuu kuwa "mke bora hutoka kwa bwana (muumba)". Ukiona hivyo ujue bado muumba hajakutengea wako!!!

ILA...ILA.... kama nawe umekuwa ukiwatendea wenziwako ndivyo sivyo, inawezekana muumba anafanya malipizi kwa mabaya hayo uliyotenda maana "Muosha Huoshwa", kama ndivyo, tubu mrudie muumba na omba misamaha kwa wabaya wako na halafu mpigie magoti muumba wako na omba mke bora, atakupa nakuambia...
 
Ikifika siku Mungu atatuma malaika uitaona anakuonyesha huyu ndo mke wako.

Lakini wewe hutamuona malaika.

 
Kwanza jiulize ulishajitambua ni mwanamke wa aina gani unamtaka,
Coz kuna baadhi ya wavulana japo wanakuwa wanona ni wanaume ukimuliza aina ya mke anayetaka hizo sifa anazotaja mpaka aibu kwa uankuta kabase kwenye sifa za nje ambazo ni ngumu kwa mtu mmoja kuwa nazo zote labda mpaka kutoa oda kwa mungu amtengenezee,so kumpata inakuwa ishu,
Nakushauri tuliza akili,mke sio sura wala umbo,mshirikishe mungu ktk kumtafuta utampata tu coz kila mtu kaumbiwa mtu wake,
Jiweke km mwanaume alietayari kuwa baba wa familia sio ujiweke kivulana utaishia kupata visichana mcharuko,
Hata ukimpata anayefanania kuwa mke uwe na subira na mvumilivu kwan wengi huwa hawakurupuki kukukubali ni lzm auone userious wako,pia angalia namna unavowaaprochi,ulimi wako ndio silaha pekee hata km utakuwa na mwonekano wa aina gani!
Epuka kutumie pesa km ushawishi wakati wa kujieleza ni sumu kali kwa wadada walio makin,japo wengi hawaamin hili.
 
Ila kweli mkuu wanawake wengi nimcharuko lakini siyo wote wewe jitaidi kutafuta kanisani kwako na pia umuombe mungu
 
Leo hii ukiniuliza nilimpataje mama Ngina hata sikumbuki...................... haya mambo huwa yanatokea Automatikale.
Hahaha wacha weee, mbona mimi namkumbuka mama Ali nilipata wapi....yani kipendo changu nakumbuka mpaa nguo alio vaa na saa ngapi nilimuona na alikuwa wapi...usisikie ukipenda mpaa unapata akili usahau kabisa :biggrin:
 
Back
Top Bottom