Mlinzi wa Mbowe azua kasheshe CCM Arusha

KIGENE

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,552
813





amka2.gif
MLINZI binafsi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amezua balaa kubwa kwa Chama cha Mapinduzi mkoani Arusha kutokana na sura yake kufafanishwa na ile ya Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) wilayani Arumeru, Boniface Mangaya Laizer, na hivyo kusimamishwa uongozi.
Laizer ambaye ni rafiki mkubwa wa kada wa CHADEMA mkoani Arusha, Ally Bananga, aliyejiengua CCM mapema mwaka huu, amedaiwa kuonekana kwenye picha gazetini akiwa na viongozi wa CHADEMA wakati wa operesheni ya chama hicho katika mikoa ya kusini hivi karibuni.
Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Boniface alisema kuwa ameshangazwa na tuhuma hizo alizoziita kuwa ni mizengwe akidai kwamba hata huyo mlinzi wa Mbowe, Zakaria Swai, anayefafanishwa naye hamfahamu.
“Mimi sijawahi kuhudhuria mkutano wowote wa CHADEMA katika mikoa ya kusini na tuhuma hizo zilipoibuliwa nikalazimika kumtafuta huyo mlinzi ili nimfahamu. Katika picha iliyochapwa na gazeti moja la kila siku la Juni mosi mwaka huu, anaonekana Bananga akiwa na Mbowe na viongozi wengine na mlinzi huyo akiwa nyuma amevalia mawani meusi, sasa huyo watamfananishaje na mimi na kunisimamisha?” alisema.
Katika barua ya kujulishwa kusimamishwa kwake yenye kumb. Na. CM/AR/S/K. 13/3/Vol. V/233 ya Oktoba mosi, mwaka huu, ikiwa imeandikwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, mwenyekiti huyo anajulishwa kuwa anasimamishwa kutokana na tuhuma za usaliti.
“ Tuhuma zinazokukabili za kiitikadi na usaliti ni nzito ambazo zinakuondolea sifa za kuwa kiongozi. Kamati ya siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa iliyokutana kuanzia Septemba 27-29, mwaka huu, ilitafakari kwa kina tuhuma zinazokukabili na kwa Mamlaka iliyonayo kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2007- Ibara ya 96 (7) iliazimia kukusimamisha uongozi,” ilisomeka barua hiyo.
Chatanda katika barua hiyo anaongeza kuwa Boniface anajulishwa rasmi kwamba kuanzia sasa amesimamishwa uongozi hadi hapo mamlaka yenye uwezo juu yake ya kikatiba itakapoamua vinginevyo.
Hata hivyo, Boniface ambaye ameibuka na ushindi mkubwa katika uchaguzi uliomalizika hivi karibuni, alisema kuwa amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa UVCCM wilayani humo kwa taratibu zote za chama na hivyo akashangaa uamuzi huo umetoka wapi.
Alisema kuwa wapiga kura wake pia wameshangazwa na uamuzi huo aliodai kuwa ni mkakati wa viongozi wa mkoa kupandikiza kiongozi wanayemtaka wao awe mwenyekiti wa UVCCM wilayani Arumeru.
Naye rafiki yake wa karibu, Bananga, alizungumzia sakata hilo akisema huo ni ushuhuda tosha kuwa Chatanda baada ya kumaliza kutimiza azma yake ya kuvuruga vyama vya upinzani mkoani humo sasa dhambi hiyo imemrudia na kuanza kukibomoa chama chake.
“Mimi Boniface ni rafiki yangu wa karibu tangu nikiwa CCM hadi sasa, ila kutokana na CCM kutapatapa na makundi yao Arusha wanadhani ninamtumia kama pandikizi kuwabomoa. Anayeonekana kwenye ile picha si Boniface bali ni Swai mlinzi wa Mbowe,” alisema.
Bananga ambaye alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Arusha na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa kupitia mkoa huo, aliongeza kuwa Chatanda ni janga la kitaifa kwani amevuruga upinzani Arusha na sasa amegeukia chama chake.
Source:Tanzania Daima



 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom