SEAL Team 6
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 655
- 118
Bunge limeelezwa kwamba, ni jambo la kushangaza sana kuona mlima Kilimanjaro umetapakaa vinyesi vya wazungu na wale wapambe wao ( pouters). Akichangia katika hotuma ya Wizara ya MALIASILI na UTALII mheshimiwa Mbowe aliweka hilo hadharani, kwamba TANAPA licha ya kukusanya $40 Milion lakini wameshindwa kujenga vyoo kwa ajili ya watalii wanaopanda Mlima huo. Ameshangaa sana kwamba hizo hela huwa zinakwenda wapi? Hii imesababisha Watanzania wanaoishi kuuzunguka milima Kilimanjaro wanatumia maji yaliyo changanyikana na vinyesi vya wazungu. Ameahidi kumpatia mheshimiwa Waziri MAIGE ushahidi ili ajionee mwenyewe tani na tani za vinyesi zinavyochafua mazingira ya mlima huo.
Tujiulize ni viongozi wangapi wa Serikali yetu walishapanda mlima huo, inawezekana kabisa miongoni mwa tani hizo zimo za viongozi hao.
Tujiulize ni viongozi wangapi wa Serikali yetu walishapanda mlima huo, inawezekana kabisa miongoni mwa tani hizo zimo za viongozi hao.