kasyabone tall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2009
- 254
- 59
UPELELEZI wa kesi inayomkabili mlemavu Anney Anney (58), ya kumkashifu Rais Jakaya Kikwete, umekamika na itaanza kusikilizwa kwa mshitakiwa kusomewa maelezo ya awali, Septemba 30.
Kesi hiyo ipo kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, chini ya Mwendesha Mashitaka Mkuu wilayani hapo, Mrakibu wa Polisi, Naima Mwanga.
Akiwasilisha ombi la kutaka kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo, Mwendesha Mashitaka, Mrakibu wa Polisi, Naima, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikilizwa.
Hakimu Maweda alikubali ombi la mwendesha mashitaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Septemba 30 wakati mtuhumiwa ataendelea kubaki rumande kwa kukosa dhamana.
Mshitakiwa huyo mkazi wa Arusha, anadaiwa kumkashifu Rais Kikwete, Julai 23, mwaka huu kwenye viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam, kwa kuandika ujumbe kwenye bango, hali ambayo ingeweza kuhatarisha amani ya nchi.
Mtu huyu alikuwa akitumia uhuru wake wa kufikisha ujumbe kwa rais, sijui kama rais analijua hili au ndio wapambe wamelivalia njuga kujipendekeza kwa rais. Mbona wale vijana walioandama na mabango ya kusema serikali ya kishikaji hawakuchukuliwa hatua? au kwa sababu ni wasomi wanajua sheria. tunaomba mashirika ya kutetea haki za binadamu tumtetee mlemavu huyu. eti anahatarisha amani ya nchi, mbona wengi wanatoa kauli za kuhatarisha amani ya nchi hawashitakiwi?, au sheria inachukua mkondo wake kwa mlemavu tu. hivi kipimo gani kinachotumiwa kupima kuhatarisha amani ya nchi au mtu yeyote asipopendezwa na ujumbe anapakazia kuatarisha amani ya nchi?
Kesi hiyo ipo kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, chini ya Mwendesha Mashitaka Mkuu wilayani hapo, Mrakibu wa Polisi, Naima Mwanga.
Akiwasilisha ombi la kutaka kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo, Mwendesha Mashitaka, Mrakibu wa Polisi, Naima, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikilizwa.
Hakimu Maweda alikubali ombi la mwendesha mashitaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Septemba 30 wakati mtuhumiwa ataendelea kubaki rumande kwa kukosa dhamana.
Mshitakiwa huyo mkazi wa Arusha, anadaiwa kumkashifu Rais Kikwete, Julai 23, mwaka huu kwenye viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam, kwa kuandika ujumbe kwenye bango, hali ambayo ingeweza kuhatarisha amani ya nchi.
Mtu huyu alikuwa akitumia uhuru wake wa kufikisha ujumbe kwa rais, sijui kama rais analijua hili au ndio wapambe wamelivalia njuga kujipendekeza kwa rais. Mbona wale vijana walioandama na mabango ya kusema serikali ya kishikaji hawakuchukuliwa hatua? au kwa sababu ni wasomi wanajua sheria. tunaomba mashirika ya kutetea haki za binadamu tumtetee mlemavu huyu. eti anahatarisha amani ya nchi, mbona wengi wanatoa kauli za kuhatarisha amani ya nchi hawashitakiwi?, au sheria inachukua mkondo wake kwa mlemavu tu. hivi kipimo gani kinachotumiwa kupima kuhatarisha amani ya nchi au mtu yeyote asipopendezwa na ujumbe anapakazia kuatarisha amani ya nchi?