Esperance
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 364
- 84
Wanajamvi kwa muda nimekuwa nikiumizwa na hili jambo. Mama mkwe wangu ni kama mke mwenzangu. Mume wangu anapanga budget na mama, kila kitu ni mama. juz kachukua mkopo bank nusu kampa mama afanye miradi. Nimejaribu kushare na familia mama kaja juu yeye ndio kamsomesha anastahil kuenziwa. Mume hashauriki bila kumshirikisha mamake. Hapa ana miez 6 tunakaa nae. Ni vurugu. Ushauri wandugu.