Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 875
- 960
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Salum Hapi leo usiku ametembelea hospitali ya Mwananyamala kujionea utoaji wa huduma hasa wakati wa usiku.
Hapi ambaye alitinga hospitali hapo kama mgonjwa wa kawaida akivalia kofia ya mkeka alitembelea mapokezi, vyumba vya daktari na baadae kumshtukiza kiongozi wa madaktari kwa usiku huo ofisini kwake akimuelekeza kumtembeza sehemu mbalimbali za hospitali hiyo ambayo Mkuu wa wilaya alitaka kuziona.
Mh. Hapi alitembelea wodi ya watoto, wanaume, wodi ya kina mama, wodi ya dharura (emergency) na kumalizia chumba cha kuhifadhia maiti (mortuary) ambako alizungumza na wagonjwa, kuwajulia hali na kujionea changamoto zinazowakabili.
Akiwa chumba cha kuhifadhia maiti Mh. Hapi alifanya mazungumzo na mhifadhi maiti na kujua changamoto zinazoikabili ofisi yake.
Hospitali ya Mwananyamala inatajwa kuwa na changamoto nyingi za utoaji huduma hali inayosababisha malalamiko ya mara kwa mara ya wananchi.
Hapi ambaye alitinga hospitali hapo kama mgonjwa wa kawaida akivalia kofia ya mkeka alitembelea mapokezi, vyumba vya daktari na baadae kumshtukiza kiongozi wa madaktari kwa usiku huo ofisini kwake akimuelekeza kumtembeza sehemu mbalimbali za hospitali hiyo ambayo Mkuu wa wilaya alitaka kuziona.
Mh. Hapi alitembelea wodi ya watoto, wanaume, wodi ya kina mama, wodi ya dharura (emergency) na kumalizia chumba cha kuhifadhia maiti (mortuary) ambako alizungumza na wagonjwa, kuwajulia hali na kujionea changamoto zinazowakabili.
Akiwa chumba cha kuhifadhia maiti Mh. Hapi alifanya mazungumzo na mhifadhi maiti na kujua changamoto zinazoikabili ofisi yake.
Hospitali ya Mwananyamala inatajwa kuwa na changamoto nyingi za utoaji huduma hali inayosababisha malalamiko ya mara kwa mara ya wananchi.