engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Mkuu wa Wilaya ya Singida Pascal Mabiti akizungumza na wananchi wa Kata Mpya ya Lighwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Paschal Kulwa Mabiti ameahidi kupambana na Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu, kutokana na kile alichodai kuwa Mbunge huyo amewadanganya wananchi wasichangie fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo lake.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi kwenye sherehe za uzinduzi wa Kata mpya ya Lighwa, Tarafa ya Mungaa katika halmashauri ya Wilaya ya Singida
Kauli hiyo ya Bw. Mabiti imekuja baada ya risala ya wananchi kumwomba awasaidie katika kutatua tatizo la Mbunge huyo kuwalaghai wananchi wasichangie miradi mbalimbalai ya maendeleo inayotekelezwa na serikali katika jimbo hilo.
Katika risala hiyo, wananchi pia wameiomba serikali kuwapatia msaada wa chakula ili kukabiliana na tishio la njaa, wajengewe ofisi ya kata, huduma ya maji safi kwa kuchimbiwa visima virefu na kukarabati bwawa kwa ajili ya matumizi ya mifugo yao.
Amesema kuwa tabia ya Mbunge huyo kuwadanganya wananchi wasichangie miradi ya maendeleo kwa kuwa serikali inazo fedha za kutosha, haitavumiliwa na yeyote atakayepuuzia agizo hilo kuanzia sasa atashughulikiwa kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Mabiti amesema wananchi wa Jimbo hilo wamekatazwa kutoa michango ikiwemo ushuru na ujenzi wa Sekondari, wakati kila mzazi au mlezi hutakiwa achangie Sh.500 kwa mwezi, kwa ajili ya posho ya mlinzi, mpishi, kuni na maji, huku Shirika la Chakula Duniani (WFP) lenyewe hugharamia chakula mchana kwa shule zote za msingi.
Akijibu maombi hayo, Mabiti ameahidi serikali kutoa msaada wa kutosha wa chakula kwenye eneo hilo lililoathiriwa na mvua chache msimu uliopita, lakini amesisitiza kuwa chakula hicho kitasambazwa na watendaji wa kata na vijiji pekee, wakati wanasiasa hawataruhusiwa kujihusisha nacho.
Amesema kata hiyo bado ni Mpya na ipo nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na maeneo mengine, hivyo zinahitajika juhudi kubwa kutoka kwa wananchi ili wajikwamue hapo walipo, ili baadaye iweze kukidhi mahitaji na huduma zingine muhimu.
Kuhusu maombi ya bwawa, maji na ofisi ya kata, Mabiti ameiagiza kamati ya maendeleo ya kata chini ya diwani wake kukutana haraka kuandaa mikakati ya kutekeleza miradi hiyo, ili wananchi wachangie kwa kufuata utaratibu uliozoeleka wa kipaumbele cha kwanza, kulingana na mahitaji yao.
Mapema akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida Celestine Yunde alisema kata hiyo ni kati ya kata 19 mpya zilizotangazwa na serikali mwaka jana na kuifanya wilaya hiyo kuwa na jumla ya kata 47.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Paschal Kulwa Mabiti ameahidi kupambana na Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu, kutokana na kile alichodai kuwa Mbunge huyo amewadanganya wananchi wasichangie fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo lake.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi kwenye sherehe za uzinduzi wa Kata mpya ya Lighwa, Tarafa ya Mungaa katika halmashauri ya Wilaya ya Singida
Kauli hiyo ya Bw. Mabiti imekuja baada ya risala ya wananchi kumwomba awasaidie katika kutatua tatizo la Mbunge huyo kuwalaghai wananchi wasichangie miradi mbalimbalai ya maendeleo inayotekelezwa na serikali katika jimbo hilo.
Katika risala hiyo, wananchi pia wameiomba serikali kuwapatia msaada wa chakula ili kukabiliana na tishio la njaa, wajengewe ofisi ya kata, huduma ya maji safi kwa kuchimbiwa visima virefu na kukarabati bwawa kwa ajili ya matumizi ya mifugo yao.
Amesema kuwa tabia ya Mbunge huyo kuwadanganya wananchi wasichangie miradi ya maendeleo kwa kuwa serikali inazo fedha za kutosha, haitavumiliwa na yeyote atakayepuuzia agizo hilo kuanzia sasa atashughulikiwa kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Mabiti amesema wananchi wa Jimbo hilo wamekatazwa kutoa michango ikiwemo ushuru na ujenzi wa Sekondari, wakati kila mzazi au mlezi hutakiwa achangie Sh.500 kwa mwezi, kwa ajili ya posho ya mlinzi, mpishi, kuni na maji, huku Shirika la Chakula Duniani (WFP) lenyewe hugharamia chakula mchana kwa shule zote za msingi.
Akijibu maombi hayo, Mabiti ameahidi serikali kutoa msaada wa kutosha wa chakula kwenye eneo hilo lililoathiriwa na mvua chache msimu uliopita, lakini amesisitiza kuwa chakula hicho kitasambazwa na watendaji wa kata na vijiji pekee, wakati wanasiasa hawataruhusiwa kujihusisha nacho.
Amesema kata hiyo bado ni Mpya na ipo nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na maeneo mengine, hivyo zinahitajika juhudi kubwa kutoka kwa wananchi ili wajikwamue hapo walipo, ili baadaye iweze kukidhi mahitaji na huduma zingine muhimu.
Kuhusu maombi ya bwawa, maji na ofisi ya kata, Mabiti ameiagiza kamati ya maendeleo ya kata chini ya diwani wake kukutana haraka kuandaa mikakati ya kutekeleza miradi hiyo, ili wananchi wachangie kwa kufuata utaratibu uliozoeleka wa kipaumbele cha kwanza, kulingana na mahitaji yao.
Mapema akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida Celestine Yunde alisema kata hiyo ni kati ya kata 19 mpya zilizotangazwa na serikali mwaka jana na kuifanya wilaya hiyo kuwa na jumla ya kata 47.