Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,066
- 4,085
MKUU wa Shule ya Sekondari ya Matimila Isdory Mrema (45) iliyopo mkoani Ruvuma amejiua kwa kujinyonga baada ya kukamatwa na kisha kuachiwa kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa dada yake .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda amesema tukio hilo lilitokea jana saa 1:00 asubuhi ambapo mwalimu huyo alikutwa akiwa amejinyonga katika nyumba yake ya Mahenge Mabatini mjini Songea kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuona aibu kutokana na kitendo alichofanya.
Alisema, Mwalimu huyo alikamatwa juzi baada ya kudaiwa kuwa alimbaka mwanafunzi wa Chuo Kikuu Mlimani (22) jina limehifadhiwa ambaye ni mtoto wa dada yake ambaye alifika mjini Songea kwa ajili ya kufanya mazoezi na kufikia nyumbani kwa mjomba wake.
Alisema, mwalimu huyo ambaye mara baada ya kutiwa mbaroni aliachiwa huru 22 Agosti mwaka huu baada ya kupewa dhamana, lakini aliamua kujiua baada ya kuona aibu kutokana na mpwaye kulipoti polisi na kueleza tukio zima lilivyotokea hali ambayo ilimsababisha aamue kujiua.
Mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya mkoa wa Ruvuma na hakuna mtu yoyote ambaye anashikiliwa kuhusiana na kifo hicho.
Wakati huo huo, baadhi ya wananchi wa manispaa ya Songea wameelezea kusikitishwa kwao na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambavyo vinaendelea mkoani Ruvuma.
Source:- MWANANCHI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda amesema tukio hilo lilitokea jana saa 1:00 asubuhi ambapo mwalimu huyo alikutwa akiwa amejinyonga katika nyumba yake ya Mahenge Mabatini mjini Songea kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuona aibu kutokana na kitendo alichofanya.
Alisema, Mwalimu huyo alikamatwa juzi baada ya kudaiwa kuwa alimbaka mwanafunzi wa Chuo Kikuu Mlimani (22) jina limehifadhiwa ambaye ni mtoto wa dada yake ambaye alifika mjini Songea kwa ajili ya kufanya mazoezi na kufikia nyumbani kwa mjomba wake.
Alisema, mwalimu huyo ambaye mara baada ya kutiwa mbaroni aliachiwa huru 22 Agosti mwaka huu baada ya kupewa dhamana, lakini aliamua kujiua baada ya kuona aibu kutokana na mpwaye kulipoti polisi na kueleza tukio zima lilivyotokea hali ambayo ilimsababisha aamue kujiua.
Mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya mkoa wa Ruvuma na hakuna mtu yoyote ambaye anashikiliwa kuhusiana na kifo hicho.
Wakati huo huo, baadhi ya wananchi wa manispaa ya Songea wameelezea kusikitishwa kwao na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambavyo vinaendelea mkoani Ruvuma.
Source:- MWANANCHI