Mkuu wa Polisi hivi Jeshi la polisi halina risasi za rubber? Watatuua hadi tuishe, Tuamke Jamani

Duduwasha

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
5,703
3,653
Huwa nasikitika sana na kupatwa na huruma nikisikia mpigania haki kauawa na risasi za Moto na Jeshi la Usalama wa raia la polisi. Tunasikia Nchi nyingi huwa wanatuliza Ghasia kwa silaha baridi au risasi za Rubber.

Iweje kwetu Kila ghasia tunasikia polisi Wameua Raia? Siku tutamalizwa wote tuamke, kamanda Mkuu unahitajika kuwajika kwa hili. Watanzania tutapata wasi wasi kuwa mnatumiwa na sio mnafuata Sheria. Au Ndio mambo ya Kupeana vyeo bila ujuzi wa Kazi?

Sorry Mkuu wa polisi uwe na huruma na wewe utahukumiwa na muumba wako.
 
Polisi wa tanzania hawajui hayo wao wamefunzwa kuua tu. Uhai kwao si kitu maana watanganyika wote ni wanyama tu wakiwemo na mama zao.
 
Asilimia sabini ya polisi ni form four failures na darasa la saba waliopewa vyeti vya ndugu zao unategemea nini???
 
Jibu la hili ni kuunda kitu kinachoitwa police complaints commission, nchi nyingi nyingine zinacho. Kazi yake ni kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi dhidi ya polisi na kuchukua hatua kama kumfuka kazi polisi husika, kumpeleka mahakamani, kumshusha cheo nk. Tanzania hatuna kitu hicho, na tutakwisha, polisi watatumaliza. Inakuwaje polisi wauwe wao, wapokee hongo wao, majambazi wao, wanyang'anyi wao nk; hawawezi hao kujichunguza na kujichukulia hatua. Sasa hivi wao polisi ndiyo wauwaji wakubwa; watu wanaouwawa na polisi wanazidi wanakufa kwa UKIMWI. Tuamke jamani, hasa tunapojadili Katiba mpya!
 
Back
Top Bottom