bi mkora
JF-Expert Member
- Jun 1, 2011
- 259
- 113
Jana jioni mkuu wa mkoa wa Arusha alifanya kipindi maalumu kaitka Radio Triple A arusha na kusisitiza kuwa wananchi tuwe na amani na kuwa leo hakutakua na mgomo wa daladala. Mkuu huyu wa mkoa wa Arusha hakutupa angalizo lolote kuhusiana na mgomo huu na akatuahidi kuwepo kwa usafiri na amani kwa ujumla chini ya usimamizi wa OCD Zuberi.
Leo hali imekua tofauti na ahadi za Mkuu wa Mkoa huu wa Arusha alizozitoa jana, Wakazi wa Arusha leo hii tumetaabika kwa kukosa usafiri, wafanyakazi tumechelewa kazini, wanafunzi wamegahiri kwenda shule kwani muda mrefu wameutumia kutembea kwa miguu. Daladala nyingi zimepigwa mawe maeneo ya kwa moromboo, esso,mianzini, sanawari na sehemu kadha wa kadha.
Amani aliyeihubiri Mkuu wa Mkoa wa Arusha haijafanikiwa kama alivyotuahidi.Uharibifu wa mali hasa daladala na kuchelewa kwa shuhuli za kila siku za Arusha inadhihirisha hii nguvu ya umma inakaribia kuwashinda na kuishia kuwakamata wapiga debe na madereva.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha naomba unitake radhi kwa kunipa ahadi ya uongo jana na kunifanya nipate adhima katika siku yangu.
Leo hali imekua tofauti na ahadi za Mkuu wa Mkoa huu wa Arusha alizozitoa jana, Wakazi wa Arusha leo hii tumetaabika kwa kukosa usafiri, wafanyakazi tumechelewa kazini, wanafunzi wamegahiri kwenda shule kwani muda mrefu wameutumia kutembea kwa miguu. Daladala nyingi zimepigwa mawe maeneo ya kwa moromboo, esso,mianzini, sanawari na sehemu kadha wa kadha.
Amani aliyeihubiri Mkuu wa Mkoa wa Arusha haijafanikiwa kama alivyotuahidi.Uharibifu wa mali hasa daladala na kuchelewa kwa shuhuli za kila siku za Arusha inadhihirisha hii nguvu ya umma inakaribia kuwashinda na kuishia kuwakamata wapiga debe na madereva.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha naomba unitake radhi kwa kunipa ahadi ya uongo jana na kunifanya nipate adhima katika siku yangu.