Mkutano wa wawekezaji - Rukwa

tatizo tunasubiri watawala walete mageuzi na kubadili katiba ili kubadilisha hali hii, hicho hakiwezekani ndugu yangu!!!
Kwa nini tusubirie wjukuu watuone na wakati sisi ndio tunaishi sasa na hatujafa bado!?
Badala ya kufa 'kibudu' na kuacha aibu ya kuishi ni kwa nini tusife na kuacha heshima nyuma!!???
"Tunaweza kufanya chochote kuweka sawa mambo" ...ndiyo sentensi ya kufanyia kazi!

Kwani bado wewe unawaamini (kwenye red hapo)

Sasa Mkuu tutafanyaje? (hapo kwenye red). Inabidi kuwaamini tu hivyo hivyo labda watakuja kubadilika? Juzi nikamsikiliza bwana mmoja ameletwa kwenye mdahalo wa umeme, haki ya nani ilikuwa ni aibu! Eti Engineer lakini hawezi kujieleza? Aaaaaagh! Yaani kwa kweli TZ tuna laana! Angalia wanasheria wanavyotuangusha na mikataba mibovu mibovu, njoo kwa wanauchumi, nenda kwa madaktari wa binadamu, tazama walimu. Kila sekta uozo mtupu, sasa tutatoka kweli?

Kuna mwaka niliwahi kusoma utafiti uliofanywa kwenye nchi za EAC (wakati huo zikiwa nchi 3), ikaonekana TZ wanajua kupanga mipango ila utekelezaji ni 0, Kenya hawajui kupanga, ila hata kile kibovu wanachokipanga wanajua kutekeleza, Uganda yenyewe ilionekana ni wazuri kwa ku-copy and paste na kile walichoiba kutoka kwingine wanakitekeleza kwa ufasaha.

Hebu wasomi wetu watuokoe na hili janga. Mawaziri kwenye vikao kazi yao ni kuchapa usingizi tuuuuuuu! Hawaji na mbinu mbadala za kuiokoa nchi na huu umasikini. Kama wakulima wetu wadogo wagekuwa wanatusikia tungeking'oa hiki chama madarakani tukajaribu na gari jingine maana hawa naona uwezo wao wa kufikiri umefikia kikomo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
This is whats goin on and its a shame that it is done with our own leaders

http://media.oaklandinstitute.org/sites/oaklandinstitute.org/files/OI_AgriSol_Brief.pdf

As an individual Simba akipata 1% from such investment ni pesa kubwa sana lakini akumbuke ni watanzania wangapi ambao amewanyima haki yao hiyo kama yake ya kupata the same value as he is going to get as an individual.

Hii ndiyo aina ya watu tulionao Tanzania ambao ukiwaambiwa wazawa wame nyang'anywa haki yao kupitia matumbo yao wanasema tunavuruga amani ya taifa, ila yeye kula share kubwa hivyo comperatively ya wazawa siyo kuvuruga amani wakati anajua through this a millions of children are going to die because of lack of martenity and child care kimya kimya bila sauti zao kusikika! Tukipiga kelele tukawa na confrontations za hapa na pale only 1000 perhaps kwa ukorofi wa ma bwanyenye are going to loose their lives; sipendi vita lakini inapobidi kupigana kwaajili ya wanyonge am ready to die! Daudi hakuona shida kutokuthamini maisha yake kwakumkabili Goliath kwani alijua ajapo upoteza Mungu aweza mrudishia huo na zaidi heshima mbinguni na dunia....Yeye amekuwa mfano kwetu sote ambao kwaasili ni wa uzao wake.

Come on my people dont be deceived by these mbwa mwitu waliovaa ngozi za kondoo huku wakitutangazia amani wakati mikono yao imejaa damu za wanawake na watoto wasio na hatia. Sasa tujiulize kifo cha mtu aliyekufa bila kupiga kelele ni sawa lakini cha yule anayepiga kelele si sawa? Amani watoayo wanadamu ndivyo ilivyo ole ni kwao maana damu ya hao iko milangoni mwao ikidai kisasi naye malaika wa utungu yuko tayari kutimiza wajibu wake!
 
Kwani sisi hatuwezi kuwa wakulima wakubwa ama mpaka awe foreigner? Acheni utumwa wa akili jamani....kuna technology gan ya kwenye kilimo ambayo hatuna wataalamu Tanzania? Kwa taarifa yako hakuna fani yenye wasomi wengi nchini kama kilimo tena kwenye kila fani au una dhani watu wakisema capital wanamaanisha pesa? Basi kama ndivyo wachukue hao wataalamu geuza value zao kwenye pesa; chukua ardhi iweke kwenye fedha na labor iliyopo alafu rudi hapa kutuambia ni kiasi gani cha dollar utuambie hatuna capital. Botswana ambayo inaendelea kupaa kwaajili ya kilimo na madini ilikuwa inatumia wataalamu wetu wa Kilimo na mpaka leo wengine bado wapo huko. Tatizo letu kubwa ni la uongozi na sera zake no more no less!

We upo safi, mawazo yako burudani sana
 
Sasa Mkuu tutafanyaje? (hapo kwenye red). Inabidi kuwaamini tu hivyo hivyo labda watakuja kubadilika? Juzi nikamsikiliza bwana mmoja ameletwa kwenye mdahalo wa umeme, haki ya nani ilikuwa ni aibu! Eti Engineer lakini hawezi kujieleza? Aaaaaagh! Yaani kwa kweli TZ tuna laana! Angalia wanasheria wanavyotuangusha na mikataba mibovu mibovu, njoo kwa wanauchumi, nenda kwa madaktari wa binadamu, tazama walimu. Kila sekta uozo mtupu, sasa tutatoka kweli?

Kuna mwaka niliwahi kusoma utafiti uliofanywa kwenye nchi za EAC (wakati huo zikiwa nchi 3), ikaonekana TZ wanajua kupanga mipango ila utekelezaji ni 0, Kenya hawajui kupanga, ila hata kile kibovu wanachokipanga wanajua kutekeleza, Uganda yenyewe ilionekana ni wazuri kwa ku-copy and paste na kile walichoiba kutoka kwingine wanakitekeleza kwa ufasaha.

Hebu wasomi wetu watuokoe na hili janga. Mawaziri kwenye vikao kazi yao ni kuchapa usingizi tuuuuuuu! Hawaji na mbinu mbadala za kuiokoa nchi na huu umasikini. Kama wakulima wetu wadogo wagekuwa wanatusikia tungeking'oa hiki chama madarakani tukajaribu na gari jingine maana hawa naona uwezo wao wa kufikiri umefikia kikomo.

Siyo kweli kwamba wataalamu wa Tanzania ni wabovu katika utekelezaji bali walio wengi wanaendeshwa na wanasiasa na viongozi wanafiki so wanapokuja public hawaji kitaalamu bali kisiasa maana wasipofanya hivyo huishia kuwa victim and most have suffered the consequences ndiyo maana wanaamua kunyamaza maana kwa bahati mbaya jamii yetu haijui kuunga mkono wazalendo bali mafisadi....Angalia hapa JF mafisadi wanavyo tetewa kwa garama yeyote ile huku wazalendo wakisulubiwa kila iitwapo leo....

Nafahamu a number of capable citizens ambao wameachwa nakuambulia kuwa watu wasioheshimika mbele ya jamii na familia zao mf. ni saga la wizara ya maliasili wengi wa walioshikia bango misitu isiuzwe walipelekwa wengine wamekuwa wakuu wa vyuo visivyo na wanafunzi...Wataalamu wame nyanyaswa ki psychology sana na wanasiasa na baadhi ya viongozi affiliated to magamba kiasi ambacho wengine wakiona hawathubutu kunyanyua mdomo wala kutumia taaluma zao ipasavyo maana cost ya kufanya hivyo ni kubwa...Ndipo napo uliza basi hata vyombo vyetu vya usalama huwa vinalinda usalama ama ujambazi? So sad!
 
KIKWETE; kigoma airport will be the hub for the great lakes regions...the constructor has already been secured and he is mobilizing equipments to start the construction!
ule mpango wa kuifanya KG kuwa dubai upo mbioni
 
MH,kikwete antoa hotuba yake kwenye mkutano wa kupata fursa za uwekezaji katika mikoa ya kigoma ,Rukwa na katavi lakini kwa kujua kuwa hii ni nafasi ya kuwa fanya watanzania wengi wa maeneo husika kujua nafasi yao kwenye uwekezaji unaotakiwa kufanyika kwenye maeneo yao je kutumia lugha ya kiingereza eti sababuwawekezaji wengi ni wageni na mabalozi hawatendei haki watanzania wengi jifunze mh

jk
wewe usiwe mnafiki jk aliongea kiingereza na pia akaonge Kwa Kiswahili.sasa wewe ulitaka wale wawekezaji wamsikilize Kwa lugha gani? Nyie Ndiyo mnaorudisha nyuma maendeleo yetu
 
wewe usiwe mnafiki jk aliongea kiingereza na pia akaonge Kwa Kiswahili.sasa wewe ulitaka wale wawekezaji wamsikilize Kwa lugha gani? Nyie Ndiyo mnaorudisha nyuma maendeleo yetu

Mkuu maendeleo gani na nyie kina nani...? kabla sijaanza kubisha naomba kwanza unijuze huenda wewe ndio unakuja kuchota ardhi kwa manufaa yako na corporation yako.
 
Bila shaka wengi wetu hatujui mazingira hasa ya nchi yetu na watu wetu. Ni watanzania hawa hawa, ambao wakipelekewa vyandarua wao wanavulia samaki. Ni watanzania hawa hawa wanao vyua samaki kwa kutumia sumu na mabomu huku wakijua inathiri siyo tu mazingira bali hata afya zao na watoto wao. Ni watanzania hawa hawa ambao wameua mashirika ya umma. ni watanzania hao hao ambao wameua vyama vya ushirika, na Ni watanzania hawa hawa ambao wamekaa na ardhi yooooote hii yenye rutuba siku zote bila kuanzisha kilimo cha kisasa. Niwatanzania hawa hawa ambao wanapewa elfu 10 na kuachia vyocha ya pembejeo. Ni watanzania hawa hawa ambao wanauza shahada ya kupigia kurakwa Tsh 5,000

Hawa ndo watanzinia ambao mnataka serikali iwasaidie ili wawe na kilimo cha kisasa. Watanzania wengi walioko vijijini siyo kwamba wanashindwa kulima kwa kisasa wakiamua. Tatizo la watu wetu ni fikra na siyo mitaji wala uwezeshwaji. Wanacho hitaji ni Elimu.

Na serikali tangu uhuru imekua ikitoe elimu ya kilimo cha kisasa, majarida yameandikwa, vipindi vya radio kila wiki vipo, hadi kitengo maalumu cha kutoa elimu ya kilimo cha kisasa kilianzishwa na kimefanya kazi nzuri. Lakini tatizo ni fikra, watu hawabadiliki. Wazee wakivuna mazao hawaonekani nyumbani hadi fedha ziishe, badala ya kuendeleza kilimo wengine wanaoa wake wa 3 n.k

Ninachosema njia zote mbili ni muhimu katika kuendeleza kilimo..yani kuleta wawekezaji wakubwa katika kilimo na kuwezesha wakulima wadogo wadogo. Na hili linafanyika. Pembejeo za ruzuku zinatolewa, wataalamu wa kilimo (maafisa ugani) sasa wameajiriwa kwa kila kata na kila wilaya imenunua matreka kwa ajili ya kuwakopesha wakulima wazawa. Kwa hiyo yote mawili yana nafasi yake.

Vile vile hakuna mkulima mzawa ambaye amewahi kuomba ardhi ya kilimo akanyimwa. wengi wenu hapo Dar mna mashamba mkoa wa pwani na sehumu nyingine, je ni nani analima kila mwaka hata ekari 10 tu? Mnacho taka ni kushikiria ardhi bila kuitumia ili akitokea mwekezaji nyie mumuuzie.

Mashamba makubwa yatatoa ajira, yataongeza export na kuongeza chakula. Moja ya sababu zilizofanya mikoa ya kasikazini kupiga hatua kubwa yamaendeleo ukilinganisha na mikoa mingine ni uwepo wa mashamba makubwa. Mashamba ya Ngano, mashamba ya miti na mahindi na maharage. Iringa pale shamba moja tu la miti la sao hill limefanya maisha ya watu wengi yaboreke. Tuache siasa tujaribu kuwa realistic. Tuache kusikiliza wanasiasa wanaotupotosha badala yake tutumie fikra zetu wenyewe.

I 100% support initiatives za mtoto wa mkulima.
 
Bila shaka wengi wetu hatujui mazingira hasa ya nchi yetu na watu wetu. Ni watanzania hawa hawa, ambao wakipelekewa vyandarua wao wanavulia samaki. Ni watanzania hawa hawa wanao vyua samaki kwa kutumia sumu na mabomu huku wakijua inathiri siyo tu mazingira bali hata afya zao na watoto wao. Ni watanzania hawa hawa ambao wameua mashirika ya umma. ni watanzania hao hao ambao wameua vyama vya ushirika, na Ni watanzania hawa hawa ambao wamekaa na ardhi yooooote hii yenye rutuba siku zote bila kuanzisha kilimo cha kisasa. Niwatanzania hawa hawa ambao wanapewa elfu 10 na kuachia vyocha ya pembejeo. Ni watanzania hawa hawa ambao wanauza shahada ya kupigia kurakwa Tsh 5,000

Mkuu you are missing the plot...!!!, hivi ni watanzania, yaani wakulima ndio waliua vyama vya ushirika, Mkuu ni kwamba hata hiki kilimo kikubwa ni kwamba corporation chache ndio itakifanya ila tofauti ni kwamba watachukua profit kubwa na mara nyingi kwenda kufanya processing huko kwao sasa ni kipi kinashindikana kuunda board / ushirika ambao utakuwepo kwa niaba ya wananchi na kila mwananchi anajua kwamba hili ni shamba letu hivyo basi hii venture itakuwa sio profit based bali service based yaani faida yote itarudishwa kwenye jamii kuendeleza jamii husika na kutoa misaada.., kumbuka pia mpaka sasa hatujashindwa kujilisha ni hao hao watanzania unaosema wenye fikra mbovu ndio wameweza kutulisha tena kwa jembe la mkono tatizo serikali imeshindwa kuleta miundo mbinu ya kutosha hadi mazao yanaozea kwenye mashamba

Hawa ndo watanzinia ambao mnataka serikali iwasaidie ili wawe na kilimo cha kisasa. Watanzania wengi walioko vijijini siyo kwamba wanashindwa kulima kwa kisasa wakiamua. Tatizo la watu wetu ni fikra na siyo mitaji wala uwezeshwaji. Wanacho hitaji ni Elimu.

Mwenye kazi ya kutoa elimu ni nani...?

Alafu narudia tena mambo ya kila mtu kufanya issue kivyake hayafai ni kwamba maeneo makubwa yakichukuliwa na kulimwa kisasa na sio serikali kuwezesha mtu mmoja mmoja bali kama wakitengeneza vyama vya ushirika na kuvipa uwezo na pesa ya kununua machinery za kisasa zinaweza kuzalisha surplus ambao inaweza kuuzwa hata nje kwa faida ya community nzima na nchi (tofauti na wawekezaje watachukua a large chunk of profit na mkulima sidhani kama ataweza ku-compete kwa mazao na hawa watu)

Na serikali tangu uhuru imekua ikitoe elimu ya kilimo cha kisasa, majarida yameandikwa, vipindi vya radio kila wiki vipo, hadi kitengo maalumu cha kutoa elimu ya kilimo cha kisasa kilianzishwa na kimefanya kazi nzuri. Lakini tatizo ni fikra, watu hawabadiliki. Wazee wakivuna mazao hawaonekani nyumbani hadi fedha ziishe, badala ya kuendeleza kilimo wengine wanaoa wake wa 3 n.k

Mkuu unatangaza kilimo cha kisasa alafu unatoa power tillers.., huwezi kumlaumu mkulima mdogo wakati ameweza kutulisha mpaka leo kwa kutumia jembe la mkono na kupinda mgongo wake mpaka amepata kilema cha maisha, unataka fikra zibadilike vipi waende benki wakaibe ili wanunua ma-trekta.., mkuu kama nilivyosema inabidi kutengeneza vyama vya ushirika na ku-inject capital kubwa ili vilime kwa manufaa ya jamii yote husika na kupeleka viwanda vya kusindika huko huko bush ili kuongeza ajira huko na kuongeza value na kuhakikisha kuna usafiri wa kutoka huko mpaka sokoni

Ninachosema njia zote mbili ni muhimu katika kuendeleza kilimo..yani kuleta wawekezaji wakubwa katika kilimo na kuwezesha wakulima wadogo wadogo. Na hili linafanyika. Pembejeo za ruzuku zinatolewa, wataalamu wa kilimo (maafisa ugani) sasa wameajiriwa kwa kila kata na kila wilaya imenunua matreka kwa ajili ya kuwakopesha wakulima wazawa. Kwa hiyo yote mawili yana nafasi yake.
Mkuu acha kujidanganya hata marekani na nchi zote kubwa hakuna nafasi ya mkulima mdogo wakija wakulima wakubwa its simple mathematics hawa wakulima wakubwa wanaweza wakatoa mazao at a lower cost na mwisho wa siku waka-offer at a lower price.., mkulima mdogo atakufa a natural death..., na kumbuka mimi sisemi tubaki na wakulima wadogo bali nasema hao wakulima wakubwa (wawekezaji) viwe vyama vya ushirika kwa manufaa ya wananchi wote wenye ardhi yao kwa faida yao.., Nchi nyingi ni kwamba 10% ndio inalisha 90% sasa hiyo 10% badala ya kuwa foreigner kwanini isiwe vyama vya ushirika vinavyomilikiwa na vipo kwa faida ya wananchi wote..?


Vile vile hakuna mkulima mzawa ambaye amewahi kuomba ardhi ya kilimo akanyimwa. wengi wenu hapo Dar mna mashamba mkoa wa pwani na sehumu nyingine, je ni nani analima kila mwaka hata ekari 10 tu? Mnacho taka ni kushikiria ardhi bila kuitumia ili akitokea mwekezaji nyie mumuuzie.
Mkuu wachukue ardhi walime kwa kutumia nini..?, power tillers au waende msituni walime ambapo hakuna barabara nani atakaeleta mazao sokoni au waache ngedere ndio wayale..., Think Mkuu hiyo ardhi yote ingechukuliwa na vyama vya ushirika sidhani kama mgesema kwamba elimu, na afya bure haviwezekani na vile vile tungeacha kwenda kutembeza bakuli nje.., pia tungeweza kutoa welfare kwa wazee wetu na watu ambao hawana kazi na usitegemee hawa wawekezaji watakubali pesa zao zifanye kazi za charity

Mashamba makubwa yatatoa ajira, yataongeza export na kuongeza chakula. Moja ya sababu zilizofanya mikoa ya kasikazini kupiga hatua kubwa yamaendeleo ukilinganisha na mikoa mingine ni uwepo wa mashamba makubwa. Mashamba ya Ngano, mashamba ya miti na mahindi na maharage. Iringa pale shamba moja tu la miti la sao hill limefanya maisha ya watu wengi yaboreke. Tuache siasa tujaribu kuwa realistic. Tuache kusikiliza wanasiasa wanaotupotosha badala yake tutumie fikra zetu wenyewe.

I 100% support initiatives za mtoto wa mkulima.

Mkuu wewe ndio tumia fikra zako mwenyewe na acha hizi propaganda.., hizi ajira zinazoongezeka ni zipi za kubadilisha oils kwenye tractor..., mkuu acha kutafuta short cuts kwenye hizo export zikiongezeka Tanzania itapata % ngapi, hivi niambie ni nini ambacho anafanya huyo mwekezaji vyama vya ushirika vinashindwa na kubaki na 100% ya profits ? na ni nani amekwambia tunakosa chakula sasa hivi sababu hakuna wakulima wanaozalisha..? issue ni kwamba hakuna miundombinu (hata reli wameshaiua..) ya kuleta chakula sokoni mpaka mazao yanaozea mashambani..

Mkuu acha kabisa hizo porojo kama unataka ukweli kaangalia so called small farmers in UK na USA they are non existent na wengine inabidi wauze ardhi zao sababu they can't compete tena washukuru Mungu wengine huko wana welfare huko Bongo kila mtu atakufa kifo chake na umasikini, wakati kama ingekuwa ni vyama vya ushirika vingehakikisha kila mtu anapata gunia za mahindi hata kama hana pesa au ana pesa kidogo sababu mali ni ya kwao mali ya ushirika
 
  • Thanks
Reactions: Ame

Similar Discussions

Back
Top Bottom