Mkutano wa Mwakyembe na Hoja za Mgongano wa Maslahi

Wakuu kifupi Mwakyembe amesema YEYE alishajiondoa kwenye kampuni kama mwana hisa lakini yeye pamoja na wabunge wengi wanaiunga mkono kampuni hii na wanaendelea mpaka sasa kuwa interested nayo kwani ni ya wazalendo na haijawahi kupata mkopo toka benki yoyote japo ni ya wazawa.

Nadhani kwa sasa niwaachie uwanja wakuu... Am around

Mkuu Ivisible,

Kwanza asante sana kwa kutupasha hii press conference ya mheshimiwa.

Kama waandishi wa Tanzania wanajua kwenda chini kufuatilia info, huenda hili jambo likazua mambo mengine kibao.

Kama mheshimiwa ka transfer hizo shares zake inatakiwa awe amelipa pesa nyingi kweli kwenye hiyo process, kwa mtaji wa karibu bilioni 2, huenda ikawa mamilioni. Bila kufanya hayo malipo, hata ukirudisha hizo form zinakuwa hazina maana na bado unaendelea kuwa mmiliki wa shares hizo. Kama nakumbuka vizuri inatakiwa kulipa TRA 1% ya thamani ya shares kabla ya BRELA kuhalalisha hiyo transfer. I hope Dr. alifanya hivyo.

Labda mnaojua sheria ya kuuza au ku transfer shares ikoje naomba tuelemisheni zaidi.
 
Kweli tutaona na kusikia mengi mwaka huu.. mpaka huyo tembo CCM aanguke chali na kumen'genyuka vipande vipande patakuwa hapatoshi!
 
Watanzania si wajinga TENA!! Hatutalazimishwa kuoga maji machafu na walio wachafu!Zitto kaoga maji machafu aliopewa na wachafu.Mwakyembe katu usiyaoge maji hayo!
 
KWA HIVYO KULINGANA NA UNAVYOTUSHUSHIA, GAZETI HALIKUSEMA UONGO BALI MAONI YA MWANDISHI YA HILI LA CONFLICT OF INTEREST NDIYO TATIZO.

Sioni ubaya uliofanyika hapa kwani mwandishi ana hiari na mtizamo wa jambo na wananchi pia wana hiyari ya kuyatilia maanani maoni ya mwandishi au la. HOLA za nini? Mbona tunasoma udaku na tukaupalilia itakuwa hili la kujuulisha Wananchi kuwa Shujaa wao nae anainterest na suala la kuuzia umeme TANESCO?

Kwanini tunakuwa defensive sana kwa kuambiwa tunamiliki hichi au hichi wakati ni jambo la kawaida kwa Tanzania hii kwa Wakubwa kumiliki makampuni na vitega uchumi tele huku tukuhibiriwa sisi wa kawaida hali ngumu za maisha.?

Sishangai wakubwa wetu kumiliki vitega uchumi lakini kinachonipa kichefuchefu ni kuwa mtu mpaka awe Mbunge au Waziri ndio afanye miradi, hii inasababishwa na nini? Pengine mpaka uwepo Bungeni ndio upate kibali cha kuingia hili daraja la watega uchumi. Ndio Maana watu kama Mwakyembe hawakuwa na makampuni kama haya mpaka wameingia Bungeni. Sasa watu kama hawa wakianza kuzozana kwa wao sawa kwani ni vita yao lakini sisi wananchi wa kawaida hatuna faida yoyote kwani mwisho wa siku wao wanalindana.Angalia Rostam hivi, Mwakyembe hivi lakini wote wako Bungeni chini ya CCM na hakuna hatuwa yoyote inayochukuliwa.

Mtizamo wangu kwa hili ni kuwa ni vizuri tujuulishwe tu juu ya hawa viongozi wetu na kwa vile uchaguzi ujao wa CCM wananchi ndio waamuzi basi hapo ndio tutakuwa wahusika lakini sasa tunatumika kuwapa kipato waandishi tu.
 
Anasema:

Dhamira ya kampuni ile ni kuzalisha umeme wa Megawati 1800 na hakuna kampuni hata moja kwa Tanzania itaweza.

Na anasisitiza ziangaliwe annual returns za kampuni hiyo za mwaka 2007/08 tutagundua kuwa shares zilishakuwa transfered siku nyingi.

Ameulizwa kuwa ametoa tuhuma kadhaa kwa RA na wote wawili ni wajumbe wa NEC... Haoni kama baadae itakuwa tatizo?

Kajibu: Hilo swali angeulizwa Rostam, kwakuwa yeye ndo anayefanya kuchafua wenzake na anajua siku si nyingi mambo yake (RA) yatalipuka tu.

Conference imeisha wakuu

Asante Mkuu kwa updates na kuwasilisha, sasa tumngojee RA na vibaraka wake watoe majibu yao. Long live JF, Daima mbele!
 
Wakuu kifupi Mwakyembe amesema YEYE alishajiondoa kwenye kampuni kama mwana hisa lakini yeye pamoja na wabunge wengi wanaiunga mkono kampuni hii na wanaendelea mpaka sasa kuwa interested nayo kwani ni ya wazalendo na haijawahi kupata mkopo toka benki yoyote japo ni ya wazawa.

Nadhani kwa sasa niwaachie uwanja wakuu... Am around

safi sana invisible kwa kutumegea yaliyojiri
 
Mkuu Ivisible,

Kwanza asante sana kwa kutupasha hii press conference ya mheshimiwa.

Kama waandishi wa Tanzania wanajua kwenda chini kufuatilia info, huenda hili jambo likazua mambo mengine kibao.

Kama mheshimiwa ka transfaer hizo shares zake inatakiwa awe amelipa pesa nyingi kweli kwenye hiyo process, kwa mtaji wa karibu bilioni 2, huenda ikawa mamilioni. Bila kufanya hayo malipo, hata ukirudisha hizo form zinakuwa hazina maana na bado unaendelea kuwa mmiliki wa shares hizo.

Labda mnaojua sheria ya kuuza au ku transfer shares ikoje naomba tuelemisheni zaidi.

jambo hili halihitaji darubini kujua kati ya mwakyembe na rostam nani fisadi cha msingi ni tutafakari jinsi ya kupambana na na mafisadi wanaoliangamiza taifa including rostam. wote walioisafisha richmond/dowans ndo tunawahisi ni mafisadi akiwemo (Dk. EH) lakini mwakyembe hana chembe ya ufisadi tunaoulalamikia.
 
jambo hili halihitaji darubini kujua kati ya mwakyembe na rostam nani fisadi cha msingi ni tutafakari jinsi ya kupambana na na mafisadi wanaoliangamiza taifa including rostam. wote walioisafisha richmond/dowans ndo tunawahisi ni mafisadi akiwemo (Dk. EH) lakini mwakyembe hana chembe ya ufisadi tunaoulalamikia.


Ufisadi kwako ni nini??
 
Asante mkuu Inv. kwa kutuhabarisha. Km Dr Mwakyembe ameamua kum-site moja kwa moja RA,kunauwezekano mkubwa RA na wenzie kujibu. Hapo ndipo yatajulikana mengi. Ninahisi akina RA na wenzie watakuja na hoja ambazo bila shaka zitakuwa ni zakuwazamisha zaidi kwa sababu wanajisafisha kwa maji taka!!
 
Sishangai wakubwa wetu kumiliki vitega uchumi lakini kinachonipa kichefuchefu ni kuwa mtu mpaka awe Mbunge au Waziri ndio afanye miradi, hii inasababishwa na nini? Pengine mpaka uwepo Bungeni ndio upate kibali cha kuingia hili daraja la watega uchumi. Ndio Maana watu kama Mwakyembe hawakuwa na makampuni kama haya mpaka wameingia Bungeni...

Nadhani hapa kuna umuhimu kwa serikali kuharakisha utekelezaji wa agizo la Kikwete la kutunga sheria ambayo itazuia wafanyabiashara kujihusisha na masuala ya siasa.
 
Anasema: "Sina mkataba na Bunge. Nina profession yangu na natamani mambo mengi kama mtanzania."

Please help me to understand cause I am totally confused, what did he mean by Sina Mkataba na Bunge ? Also what can we infer from this statement ?
 
Mkuu Ivisible,
Kama mheshimiwa ka transfer hizo shares zake inatakiwa awe amelipa pesa nyingi kweli kwenye hiyo process, kwa mtaji wa karibu bilioni 2, huenda ikawa mamilioni. Bila kufanya hayo malipo, hata ukirudisha hizo form zinakuwa hazina maana na bado unaendelea kuwa mmiliki wa shares hizo. Kama nakumbuka vizuri inatakiwa kulipa TRA 1% ya thamani ya shares kabla ya BRELA kuhalalisha hiyo transfer. I hope Dr. alifanya hivyo.zaidi.
The issue here ni kwamba kasema hizo shares have been transferred. The whole process of the transfer and how he has approached it is an entirely personal matter with his accountant or however he chooses to do it with. If you have been involved in these things, am sure you know there are many ways available to disposing of shares. So What is the reason for your speculation? Are you implying that he has lied about the transfer?
 
Ingawa sijapata kwa undani kilichojiri kwenye Press briefing (zaidi ya abstracts za Inv) naona Mwakyembe hajatutendea haki kwa sababu nilitarajia jambo kubwa atyakalolionyesha ni jinsi ambavyo hakuwa na conflict of interest wakati anashughyulikia suala la Richmond.
Lakini, kujikita kwake kumshambulia Rostam, inaonyesha jinsi gani ambavyo nchi hii inaharibiwa na wanasiasa wafanyabiashara.
 
Invissible naku salute mkuu kwa kutuhabarisha,Mwakiembe asitake kutufanya watanzania hatuna akili ww mwenyewe ulitupostia hapa document zake brella zinaonyesha kuwa mpaka jully 2007 alikuwa bado ni share holder wa hii kampuni..

Ifike mahali tusichezewe akili kiasi hichi ukiangalia kikao cha board ya hii kampuni ya mwakiembe hizo share anazo mpaka 3rd board meeting alokaa na yeye kupongezwa na bado kulifanyaika re allotment of shares na mwaky alichukua share 15 zikiwa na lengo la kuongeza mtaji wa 10bn ambao kikao chao cha April cha board kiliamua.

Lakini hiyo hoja ni utoto kama ali transfer 2006>2007 alitransfer share zipi zile 1400 or za tbc 1998 or za mecco cha kushangaza waandishi hawajauliza hili swali JF ni sehem Takatifu ambayo hujadili vitu kwa mantiki.

Najiuliza kama hoja yake ya kuuza share or kutransfer je alilipa kodi zetu stahili kuna 10 parcent capital gain tax na 1 parcent stamp duty je hizi alilipa mpaka jully 2007 document halali zinaonyesha kuwa jamaa alikuwa share holder.

Nikiwa katika korido za BRELA leo nimeona wabunge wawili wote wakikimbiza kutafuta Faili za Hii kampuni ya mwakiemnbe na pia ofisi ya bunge ikiwa inalitafuta hili faili najiuliza wapambe wa mwakiembe wanataka hili faili la nini kwa taarifa mbunge mmoja ni mwakiembe mwenyewe huyo mwingine ni wa upinzani.

Mwakiembe ameshambulia kampuni ya New Habari kuwa ni RA huyu jamaa ndo maana pale chuo alikuwa ni Mmoja wa wahadhiri wabovu hakuna document inayo onyesha kuwa RA ana hisa Habari Corporation,sasa anap[osema RA anamchafua kwa magazetio yake ni hoja ya kitoto,nilitegemea angekuja kutueleza why haku decleare intrest ameshindwa na kuleta utoto kuwa mbona waandishi wana magazeti na bado ni waajiriwa kwa hiyo tuhalalishe uovu kwa kuwa flani kafanya maovu,

Kwakweli Tabia ya wanasiasa kukimbilia Personallty badala ya kujibu hoja ni mbaya sana mtu akitofautiana na Mwaky,Sita,SELELLII,na wenzie basi kanunuliwa au ni Fisadi,hapa tulimtuhumu zito kwa kuwa kajenga hoja yake why we should buy Dowans badala ya kujibu hoja wanasiasa,na hata hapa JF tuligeuka wote kumshambulia kuwa kanunuliwa for god sake ni hatari kuendesha Nchi au wananchi kuwa na Mawazo kuwa yoyote mwenye Msimamo wake tofauti na wengine basi anatumika.

Mwisho na decleare my position kuwa mm ni mwana CCM na ktk hili naungana na zito kwa HOJA na si Itikadi,Mwakiembe natofautiana nae kwa HOJA,MAADILI,ila Naungana nae kwa ITIKADI ya Chama ingawa yeye yupo CCM inayoendeshwa kwa hisia zaidi na personality ,wakati mm nipo CCM inayoa amini ktk hoja
 
Ingawa sijapata kwa undani kilichojiri kwenye Press briefing (zaidi ya abstracts za Inv) naona Mwakyembe hajatutendea haki kwa sababu nilitarajia jambo kubwa atyakalolionyesha ni jinsi ambavyo hakuwa na conflict of interest wakati anashughyulikia suala la Richmond.
Lakini, kujikita kwake kumshambulia Rostam, inaonyesha jinsi gani ambavyo nchi hii inaharibiwa na wanasiasa wafanyabiashara.
Kujitoa kwenye hio kampuni by transfreing his shares ndio kung'amua na kujitoa kwenye wingu la conflict of interest .
 
yaah ndugu zanguni;naona yale maombi ya yabesi yanaanza kufanya kazi;waheshimiwa mabibi na mabwana kumekuwa na wingu la watu wengi kuamini kwamba hawa hawa viongozi wanawekwa na mungu,na wapo wanaoamini wanawekwa na uchawi..nk
Nimefurahi kuona mambo haya ,kabla ya hapo ewe inviscible mungu akubariki kwa hili
nafikiri hakuna kitu cha kushangaza zaidi ya kumtukuza mungu kwa kuonyesha utukufu wake kupitia viongozi. aliowaweka,ni wachache sana ambao walikuwa wanaamini ipo siku viongozi wa ccm wataanza kuelezana ukweli mbele ya comference...lakini kama unnasoma biblia inasema mungu yeye huwa anaonyesha mwanzo kutoka mwisho.yaani kabla ya mtu kujua mwisho wake mungu anaonyesha tangu mwanzo..ni wengi wasioamini hili lakini haya mambo mungu aliyaweka wazi na anayajua...mwakyembe anaanza tu lakini mambo mengi ya ajabu mbele ya watanzania yanakwenda kutokea na hapo ndipo watakapoamini mungu wa JF si mungu wa kuchezea.....wakati ester alipokuwa na mfalme akaletewa malalamiko kwamba kuna barua imeaandikwa kuwaua wayahudi..lakini walichofanya wajomba zake baada ya kumwambia easter, awaombee msamaha kwa mfalme wasiuwawe.easter akajibu niko mbali na mfalme sijui nitaanzaje..ndipo mjomba wake modekai akamwambia kama unashindwa kutuombea tusiuwawe mungu atanyanyua mtu mwingine na kwa imani tuliokuwa nayo hakika hakuna atakaekufa;mungu akampa nguvu easter akamweleza nifanyeje akasema usisaini pia yule alietoa agizo niletewe kichwa chake..ooohhhh haleluya mungu akaonekana na hakuna waliouwa...lakini yote ni maombi yakina modekai...sasa basi nirudi kwenye mada
Utaona mwakyembe anafanya kama mzaha.atakuja mwingine tena na tena....iwapo mimi na wewe tutawaombea mungu wafungue siri chafo walizokaa nazo juu ya nchi yetu miaka yote
 
Tupo pamoja mkuu. Nilikuwa najaribu kuandika yale ambayo nilionelea ni vema kuwafahamisha. Mengine tutaangalia waandishi wetu nyumbani wataandikaje.

Tutaendelea kuwategemea haohao kama sasa hivi tulivyokutegemea wewe kutuletea hizi habari.
La kutia maanani ni kuwa wewe na wao kila mmoja ana msimamo wake na ataripoti kwa angle anayotaka yeye ila tustamiliane tu kwani kwa bahati mbaya hiyo Press conference hatukuisikia bali umekuwa ikitupa clips ambazo ulihisi tutaridhika nazo. Kwa hili Mkuu nawe unakuwa mwandishi hivyo pia una intirest zako.
 
Back
Top Bottom