Mkutano wa madaktari NSSF Water Front

Wakuu yeyote mwenye ndugu kwenye hizo hospitali tajwa aanze kuscramble for plan B maana sioni mtu wa kubadisha upepo huu wa madk kwa haraka, ukizingatia issue za arumeru bado zinakaba.
 
KIKAO NDO KINA ANZA Dr. Namala ameonge na anasisitiza kikao kiwe brief na detail, Dr. ulimboka kaongea amekwisha toa muhtasari wa mkutano wa tarehe 9/2/2012.

Dr. Namala anasisitiza sababu zilizosababisha kuhitilafiana/kutokukubaliana na meza ya majdiliano ya serikali. Madaktari wanatoa michango yao.

Kikinuka nitawajulisha


Kwa ufupi madaktari wamekubaliana kuipa serikali mpaka jumatano saa mbili usiku Bwana Mponda na Naibu wake Lucy wawe wameondoka pale wizara ya afya ili waweze kukaa meza mmoja na serikali kutatua mgogoro wao.
Serikali ikishindwa kufanya hivyo basi mgomo utanza jumatano,madaktari wametumia busara kubwa sana katika mkutano wao wa leo,lakini inaonekana ofisi ya waziri mkuu na chombo kimoja cha habari vinatumika vibaya kuupotosha umma wa Tanzania.
My take: serikali ifanye jitihada ya kuwaondoa hawa waliotuhumiwa ili wananchi wasije pata madhara tena kama mgomo ulio pita
Mungu ibariki Tanzania na watu wake

Ni jumatano saa mbili asubuhi ndg..
Ila taarifa kamili itatolewa kwenye vyombo vya Habari na uongozi wa madaktari ..
 
swali lingekua hivi JK anasubiri nini kuwaondoa??
Mkuu ni kweli kwamba JK amechelewa sana kuwatimua lakini ni uungwana kwa mwanasiasa kupima na kujiuzulu pale mambo yanapoharibika chini yako. Na mbaya zaidi jambo lenyewe linapohusu sekta muhimu ktk taifa kama Afya. Kuna watu wengine ambao wanapaswa kuachia ngazi ni Mwandosya na Dr. Mwakyembe kwa misingi ya kiafya. Wawaachie hizi nafasi wenye nguvu ya mwili na afya njema wafanye kazi za wananchi muhimu serikali iendelee kuwahudumia mpaka wakipona.
 
Mpaka kieleweke, mawaziri wamekalia siasa tu, hakuna kuleta siasa kwenye taaluma za watu hapa.
 
Nahisi kama kuna sinema inataka kuanza hapa.
hebu ngoja nikae vizuri...

HII NDIYO TABIA YA WATANZANIA WENGI hata jambo serious linaonekana kama usanii! tedo BADIRIKA tafadhali, kikinuka uwe tayari kuichukulia hatua serikali ya mafisadi!
 
Hadi leo mshahara bado..! Poleni
Namsikitikia sana JK kwani huyu jamaa hayuko serious na kitu chochote. Hata madr waliposema wafukuzwe hao jamaa bado alikuwa anadhani ni utani na kuja kuendelea kudanganya wanachi kuwa anajali hali ya nchi kumbe alikimbilia ughaibuni. Shauei yenu huenda jamaa limeshapata uraia wa nchi za nje ili akimbie mambo yakiharibika. JK si mtu!
 
Umesema vyema mkuu madaktari hawataki siasa wala hawapo kwa ajili ya kumtukana kiongozi yeyote wa serikali,sas kuna watu wanaleta matusi ambayo yataharibu maana kuu ya huu mjadala
Hoja tu mkuu.
 
Mkuu kimbunga pole kwa matatizo yanayokusibu...kuongea ukweli ni matusi?
Mkuu wangu ukweli unenwe tu hata kama unauma lakini matusi pia yaepukwe. Mkuu wangu unazikumbuka zile sheria 40 za kikandamizaji ambazo Jaji Nyalali alisema zifutwe? Hivi zilishafutwa au bado zipo na zinaweza tumika wakati wowote? Unazifahamu mkuu wangu?
 
Jamani ivi bado hamfaamu kua jk hana maamuzi yeyote kwenye serekali yake!!mwacheni ****** wawa2,pakitokea jambo arakaaraka ana safari ya ughaibuni.
 
Any way!lets wait!ila nilihuzunishwa xana na madhila yaliyowapata watz wenzangu,madaktari walipogoma wenzetu walikufa xana
 
Hivi Mponda mmoja ni sawa na raia wangapi wa Tanzania?
Nawapongeza Madaktari kwa kutumia vyema usomi wao kushinikiza kuondoa watendaji wabovu katika Mawaziri wa JK.
JK anajulikana kuwa hana uwezo wa kumwondoa mtendaji yeyote mbovu kwenye serikali yake, na historia inajua hilo.
Shime, makundi mengine yaige mfano wa madaktari kuondoa kansa serikalini, maana tuliyemwamini ni mtu wa mizaha na vicheko.
 
Back
Top Bottom