KiuyaJibu
JF-Expert Member
- Aug 29, 2007
- 841
- 175
Mkutano wa International Monetary Fund(IMF) yaani shirika la fedha duniani unafanyika jiji Dar es salaam,Tanzania kesho tarehe 10.03.2009 ambapo utawashirikisha mawaziri wa fedha na magavana wa benki kuu za Afrika.
Wakati mkutano huo unafanyika,taarifa zilizopatikana zinaonyesha kwamba Policy Support Instruments zilizomo ndani ya IMF ndiyo hizo hizo zilizomo katika mpango/programme ya MKUKUTA ndani ya serikali ya Tanzania na mpango huo ambao uko katika utekelezaji wake;binafsi na baadhi ya watu wameanza kuutilia mashaka baada ya kugundulika sera zimehamishwa kama zilivyo katika makablasha ya IMF. Wakati serikali(TZ) inadai kwamba hiyo ni sera ya nchi!
Mojawapo ya udhaifu huo ni kudai uchumi wa Tanzania umeendelea kukua kwa asilimia saba(7%) tokea mwaka 2000;wakati hali halisi ya maisha ya Watanzania haiendani na ukuaji wa uchumi wenyewe.Takwimu zinaonyesha kwa kipindi chote hicho maskini wameongezeka kutoka million 11-12 hivi sasa.Na shutuma zinaonyesha kwamba yote hiyo ni kutokana na serikali kukubaliana na kupangiwa utekelezaji wa masuala ya kiuchumi na IMF; kwa upande mwingine inawezekana pia viongozi wetu wanaogopa kusema ukweli wa hali halisi na matatizo tuliyonayo katika nchi yetu.Hii inamaanisha kuna upotoshwaji wa taarifa,ukizingatia IMF yenyewe haifanyi kazi ndani ya serikali husika wao ni wageni lakini kama tukisimama katika ukweli kwa pande zote mbili inaonyesha kutakuwa na hali nzuri tofauti na ilivyo sasa.
Au kuifukuza IMF isishiriki katika kutupangia mambo ya kufanya na kuyatekeleza kama ilivyofanya nchi ya Zambia,ambayo sasa imepata ahueni baada ya kulikacha shirika hili la kimataifa.
Hebu semeni wenyewe tunafaidika vipi kama kuna nchi zinalikacha shirika hili halafu sisi bado tunalikumbatia na umaskini unaongezeka ukilinganisha na hizo nchi nyingine!?
Wakati mkutano huo unafanyika,taarifa zilizopatikana zinaonyesha kwamba Policy Support Instruments zilizomo ndani ya IMF ndiyo hizo hizo zilizomo katika mpango/programme ya MKUKUTA ndani ya serikali ya Tanzania na mpango huo ambao uko katika utekelezaji wake;binafsi na baadhi ya watu wameanza kuutilia mashaka baada ya kugundulika sera zimehamishwa kama zilivyo katika makablasha ya IMF. Wakati serikali(TZ) inadai kwamba hiyo ni sera ya nchi!
Mojawapo ya udhaifu huo ni kudai uchumi wa Tanzania umeendelea kukua kwa asilimia saba(7%) tokea mwaka 2000;wakati hali halisi ya maisha ya Watanzania haiendani na ukuaji wa uchumi wenyewe.Takwimu zinaonyesha kwa kipindi chote hicho maskini wameongezeka kutoka million 11-12 hivi sasa.Na shutuma zinaonyesha kwamba yote hiyo ni kutokana na serikali kukubaliana na kupangiwa utekelezaji wa masuala ya kiuchumi na IMF; kwa upande mwingine inawezekana pia viongozi wetu wanaogopa kusema ukweli wa hali halisi na matatizo tuliyonayo katika nchi yetu.Hii inamaanisha kuna upotoshwaji wa taarifa,ukizingatia IMF yenyewe haifanyi kazi ndani ya serikali husika wao ni wageni lakini kama tukisimama katika ukweli kwa pande zote mbili inaonyesha kutakuwa na hali nzuri tofauti na ilivyo sasa.
Au kuifukuza IMF isishiriki katika kutupangia mambo ya kufanya na kuyatekeleza kama ilivyofanya nchi ya Zambia,ambayo sasa imepata ahueni baada ya kulikacha shirika hili la kimataifa.
Hebu semeni wenyewe tunafaidika vipi kama kuna nchi zinalikacha shirika hili halafu sisi bado tunalikumbatia na umaskini unaongezeka ukilinganisha na hizo nchi nyingine!?
Last edited by a moderator: