Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Leo unaanza mkutano unaowakutanisha makandarasi wa aina zote katika ukuumbi wa Karimjee jijini Dar es Salamu!
Tutawaletea hatua kwa hatua mkutano huo utakavyo kuwa ukienda!
UPDATES:
Mada kuu zitakazojadiliwa hapa ni:
1) Utendaji kazi wa CRB
2) Utendaji kazi wa Makandarasi wa Kizalendo
3) Utendaji kazi wa makandarasi wa kigeni
Eng Mhegi: Mwaka jana tumefuta makandarasi 330
Eng Mhegi: Makandarasi wapya waliosajiliwa mwaka jana ni 460
Jumla ya makandarasi wazalendo waliopo hai hivi sasa ni 6630
UPDATES:
Eng Consolata Ngimbwa: Kuanzia mwaka ujao tunataka makandarasi wa kigeni wote wasipewa usajili wa kudumu na watasajiliwa tz wakiwa na mradi tu, ili kuwalinda makandarasi wa zalendo!
UPDATES:
Waziri Magufu: Sekta hii ya ukandarasi inatengeneza ajira kubwa sana kwa watanzania, hivyo muithamini sana
UPDATES:
Waziri Magufuli: Mradi mkubwa zaidi unaofanywa na makandarasi wa zalendo walioungana ni wa Daraja la Mbutu Igunga la 13bilioni
Waziri Magufuli: Madeni yote mnayoidai mtalipwa kabli ya bajeti ya mwezi ujao pesa tumesha pata wiki ijayo tutazishika rasmi
Na mkandarasi yoyote mwenye tabia ya kudai variation tutamuweke kwenye mabano kwakuwa wote mnatambua hali ya serikali yetu!
Tumefanya hivyo kwakuwa tumeshusha cost per km kutoka 1.4Bilion hadi 741iMilion
Lazima muijali nchi yenu na muipende pia kazi yenu! Nyinyi ni wazalendo!
Waziri amemaliza kutoa hotuba yake na kukabidhi vyeti kwa makandarasi wapya na waliopanda madaraja!
UPDATES:
Arch: Frola Mombeki:
CRB kazi yake kuu ni: (1)Kusajiri makandarasi (2)Kusimamia makandarasi na (3)Kuendeleza Makandarasi
Sasa anaanza kutoa mada Eng P.Ncheya:
Kabla hujaingia kwenye biasha yoyote Tanzania ni lazima usajiliwe na BRELA!
Na kwenu ninyi makandarasi ni muhimu mhakikishe mnapeleka Annual Returns huko BRELA, hii itawasaidia hata mkihitaji mikopo ktk mabenki
UPDATES:
Makandarasi wengi wa ndani mnakumbana na matatizo makubwa sana hasa upataji wa tenda,
Mfano:
Unaweza kutenda tenda ya 1.2bilion lakini ukakumbana na masharti yasemayo kuwa ulete turn over ya 2.4bil ya miaka mitano mfurulizo, wakati mradi huo unatakiwa kufanywa na mkandarasi wa daraja la 4,
Ukweli ni kuwa haiwezekani kwa mkandarasi wa daraja la nne kwa na turn over ya 2.4bilion ya miaka mitano mfurulizo!
UPDATES:
Sasa anaanza kutoa mada Eng Julius Kabyemera
Makandarasi ni lazima mzingatie afya na usalama wa wafanyakazi wenu
UPDATES:
Mbunge wa Morogoro mashariki: Mimi kama mbunge na mkandarasi nitaishauri serikali kuwa miradi ya kuanzia 10 bilioni ifanywe na makandarasi wazalendo tu, ili kuhakikisha mabilioni ya fedha yanayochotwa na wageni kwenda nje!
Kuna miradi ambayo ni Usalama wa Taifa haitakiwi kufanywa na wageni, mfano: Bank kuu, na maeneo nyeti ya serikali yafanywe na WAZALENDO tu kulinusuru taifa!
UPDATES:
Wakala wa usalama na afya mahali pakazi (OSHA)
Wanasisitiza umuhomu wa usalama na afya mahali pa kazi, na wadau wakuu wake ni Mteje, Mkandarasi, CRB na OSHA yenyewe,
Mteja (client) ndie anaetakiwa kugharamia Usalama na Afya site na kulipa faini zote ikiwa OSHA watabaini ukiukwakwaji wa sheria za OSHA!
UPDATES:
Eng Mwaisemba:
Consultants waandae certificates kwa wakati ikiwa mkanarasi ameshamaliza kazi yake na kukaguliwa,
UPDATES:
Eng Yericko Nyerere:
Faini za OSHA zinamuumiza mkandarasi kwa kuwa japo sheria inamtaka mteja ndie alipe lakini bado mpaka sasa mkandarasi ndie anaelipa faini hizi!
OSHA waangalie namna nzuri ya kuwaelimisha makandarasi na jamii kwa ujumla ili kuepuka dhana iliyojijenga kwao kuwa FAINI ndio suluhisho la tatizo hili!
Sisi Makandarasi tunapomalizaliza mkutano huu tutoke na maazimio ya pamoja juu ya OSHA.
UPDATES:
Eng W. Mataka
Tatizo lingine linatukumba ma Sub Contractor kwakuwa hatulipwi na Man Contractor kama mikataba yetu ilivyo,
Mda wote Man Contractor utamsikia akisema bado hajalipwa, hivyo inatuwia vigumu sana kutekeleza matakwa ya sheria ya OSHA!
Mkutano kwa leo umehitimishwa, utaendelea kesho kuanzia saa mbili kamili asubuhi!
Ondoa shaka mkuu, timu ya YECCO (T) LTD itakuwa eneo la tukio kuanzia saa mbili asubuhi kukupa yanayojiri hatua kwa hatua,Mkuu ni imani yangu hata kesho utatupa updates, kwani tungependa sana kuwepo hapo lkn kwasababu zilizo nje ya uwezo wangu nimeshindwa.