Chilisosi
JF-Expert Member
- Oct 19, 2008
- 3,051
- 747
Viongozi mbali mbali wa CCM tawi la UK wameaanza kuhaha baada ya kuona spidi ya Chadema imeshika kasi UK. inasemekana CCM kuwa makao makuu wamewaagiza waandae nyama choma / berbercue siku ya mkutano ili wajaribu walau kurudisha baadhi ya wanachama ambao tayari wameishahamia chadema. Leo viongozi mbali mbali waliokuwa wamelala walikurupuka na kuanza kuwapigia simu baadhi ya wabongo wakillalamika kuwa kwa nini wamewahama. mwenyekiti wa CCM UK Maina Owino alijaribu kuwapigia simu baadhi ya wabongo na kwa bahati mbaya kumbe alikuwa anawapigia watu ambao sasa ni wanachama wa chadema wakaaanza kumcheka.