MKUTANO WA CHADEMA BUKOBA MJINI kata Ya RWAMISHENI

Mkuu, ikiwezekana tuwekee na picha. Tueleze anasema nini Mh mbunge.
 
Diwani wa kata hii kupitia Cdm anaelezea baadhi ya mambo anayoyafanya ili kuleta maendeleo ktk kata hii, CCM imekua ikiwaonea madiwani wa chadema ,huku mstahiki Meya wa Bukoba mjini akifanya maamuzi ya kuwagandamiza madiwani wa chadema. Mh. Diwani anawaomba wananchi wa kata ya Rwami kuhudhuria vikao vya madiwani ili kujionea vioja hvyo. Wageni waalikwa ni Mbunge vti maalum Mama Conchesta, Katibu wa wilaya Victor Shelegei , waheshimiwa Madiwani, wenyevti wa mitaa na viongozi wengine wa CDM.

Mkuu, utupiamo na picha!?
 
Kwa hali isiyo ya kawaida, wakati mh. Mzungumzaji mkuu Mama Conchesta akijianda kuongea Tanesco wamekata umeme na mkutano kusimama kwa mda, lkn sasa umerudi na makamanda wanaendelea kuporomosha sera. Nawasilisha
Hata Ukonga wamefanya hivyo hivyo muda mfupi uliopita.
Wakati wa uchaguzi mkuu 2010, Mh. John Mnyika alikuwa akihutubia Kimara Dar pia Tanesco walizima umeme, nikaenda kufata jenereta kutoka kwenye saluni yangu pale karibu, tukaunganisha umeme mkutano ukaendelea.

Dr. Slaa pia waliwahi kumzimia umeme kule Mbeya. Hizo ndo fitna za magamba.

Tahadhali:
Chadema wanapotaka kufanya mkutano wowote wa hadhara wahakikishe kuwa chanzo mbadala cha umeme kinakuwepo eneo la tukio ili kuweza kupambana na vifitna vidogovidogo kama hivi.
 
Mimi nampongeza sana diwani kwa kupeleka m4c kwa wananchi huko Rwamishenyi! Nampongeza sana mbunge kwa kuongeza hamasa! Nampongeza sana sana mtoa uzi kwa kutuletea habari. Ingawa upo pekeyako lakini ujumbe unafika! Mimi natumia simu lakini kaelimu kangu ka engineering kananisaidia kuweza kupiga picha na ku upload. Japo hujaweza lakini si haba.
Peoples power!!!!!!!!?
 
Naona Mh. Victor Shelejei katibu wa CDM wilaya, anaeleza uongo ulienezwa na CCM kupitia redio yao kua Mbunge kagasheki kajenga rami sokoni wakati rami hyo haijaonekana. Makamanda wengine waliopo mkutanoni nisaidieni kutupia picha.
Mambo mengine wananchi huwa wanapenda kuongopewa. Kwani hiyo rami inakaa chumbani kwa huyo kagasheki? Inahitaji elimu kiasi gani kuitambua barabara iliyojengwa kwa rami. Au neno rami ni neno la kilugha ambalo mimi sielewi maana yake.
 
Watu ni wengi mno na kwa kua mkutano unafanyika karibu na barabara kuu iendayo Uganda magari yanashwa kupita kwani watu wamejaa hadi barabarani. Lakini wananchi ni watulivu na wanajitahdi kuruhus magari kupita japo kwa shida. Sitoweza kutupia picha kwa kua naumia cmu.
Wakumbusheni wale ambao hawajajiandikisha kwenye daftari la wapiga kura wafanye hivyo muda utakapofika, hali kadhalika wale ambao wanahitaji kurekebisha taarifa zao nao wafanye hivyo pindi muda utakapofika. Wakifanya hivyo tutakuwa na uhakika wa kura zao.
 
Popote ulipo kwenye shuguri za kitaifa Mh. Wilfred Lwakatare Mkurugenzi wa ulinzi Taifa vijana wako wanafanya kazi kweli kweli, Mama Cochesta Mbunge ndio anaongea na kumlaumu Meya wa mji kwa kumzushia uwongo unaopaswa kusemwa na mwenyekiti wa kitongoji. Anasema eti yeye alienda World Bank na kuzuia shuguli za maendeleo, huu ni uzushi unaopaswa kupuuzwa. Anasema yeye katumwa na CDM kutumikia wana Bk. Huku akieleza jinsi wabunge wa CDM wanavyo umizwa na ubadhilifu unaofanywa na CCM. Anasema hawatakaa kimya mpaka kieleweke. Mkutano inabidi uishe saa 12 jioni lkn waongeaji walikua ni wengi mno na sasa mama Conchesta ndio mzungumzaji wa mwisho. Meya wa Bukoba mjini ndio amekua topic ya leo kwani anahujumu viongozi wa CDM.
 
Weka picha mkuu, mkutano mwisho saa ngapi?

nguvu ya uma haina mwisho kwa sababu katiba ya nchi inatamka kuwa wananchi ndiyo mwisho wa mamlaka yote,ccm wakitakakufanya mkutano hawaombi kibali polisi lakini nguvu ya uma mnalazimisha iombe kibali hata kama katiba haitamki nivyo.

tutaikomboa tanzania kwa kuanzia na walioamka na kumalizia waliolala.

peoplesssssssssssssssssssssssssss!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom