Mkurugenzi wa ufundi yuko kama picha

rodrick alexander

JF-Expert Member
Feb 12, 2012
15,188
20,153
Juzi vimetoka viwango vya fifa na tanzania imeendelea kuporomoka na moja ya sababu ya kuporomoka ni timu yetu ya taifa kutocheza mechi za kimataifa mara kwa mara.
Kuanzia jana tumeshuhudia timu za mataifa mbalimbali wakicheza ama mechi za kimashindano au za kirafiki lakini sisi tupo dunia nyingine mkurugenzi wa ufundi ambaye anapaswa kujua kalenda ya fifa na pia kuitafutia timu yetu mechi ya kirafiki amekaa kimya.
Lawama zangu nazielekeza kwake kwani yeye ndiye mhusika mkuu wa kiufundi wa timu halafu timu ikifanya vibaya tunaanza kutafuta sababu mara kocha hafai,tunahitaji makocha wazawa lakini tatizo kubwa ni la kwake kwani ameshindwa kuwajibika na ukichulia juzi juzi wamesaini mkataba mkubwa na tbl.
Labda aelewi nini faida ya kuwa kwenye kiwango kizuri tunapokuwa kwenye kiwango kizuri tunakuwa tunaepuka kupangwa na timu ngumu kwenye michuano ya kutafuta naafasi ama ya afrika au dunia pia tunaepuka kuwepo kwenye mechi za mchujo.
Mwisho namtahadhalisha tenga ataondoka bila kitu cha kujivunia.
 
kwa watu wenye akili kama brazil hawasumbui vichwa kwa hizo takwimu coz hazipo accurate na wala hazisaidii kitu:flypig:
 
kwa watu wenye akili kama brazil hawasumbui vichwa kwa hizo takwimu coz hazipo accurate na wala hazisaidii kitu:flypig:
Hatuwezi kujilinganisha na brazil kwani ni timu yenye uwezo wa kuifunga timu yoyte duniani je sisis tuna uwezo huo?ndio maana tunaona kama tunaonewa pale tunapopangwa kila mara na timu zenye viwango vya juu Afrika
 
Back
Top Bottom