kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro limepitisha uamuzi wa kuwalipia ada wanafunzi 8,528 wa shule za sekondari za kata katika manispaa hiyo.
Uamuzi huo uliopitishwa juzi na baraza hilo linaloongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umepingwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Bernadette Kinabo.
Kinabo amelitaka Baraza la Madiwani kutekeleza sera za maendeleo za Serikali iliyopo madarakani katika miradi ya elimu akisema badala ya halmashauri hiyo kuwasomesha wanafunzi hao, ni bora fedha hizo zikaelekezwa kwenye utekelezaji wa sera za Serikali kwa kujenga maabara na maktaba katika shule zinazotarajiwa kuanzishwa kidato cha tano na sita mwaka huu.
Katika kikao maalumu cha kupitisha bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka 2011/12 kilichofanyika juzi mjini Moshi, Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhari Michael alisema kila mwanafunzi anahitajika kulipiwa ada ya Sh 20,000 kwa mwaka mmoja hali ambayo itafanya jumla ya Sh milioni 170 kutumika kwa ajili hiyo.
Michael ambaye ni Diwani wa Kata ya Bomambuzi (Chadema), alisema licha ya kuwajibika kulipa ada, wazazi wengi wanakabiliwa na changamoto ya kuchelewesha kulipa michango ya zaidi ya Sh 240,000 kwa ajili ya chakula, mishahara, walinzi na wapishi.
Alisema wamefanikiwa kuokoa zaidi ya Sh milioni 351 kutoka katika vyanzo mbali mbali vya mapato ya halmashauri hiyo na kwamba sehemu ya fedha hizo zitatumika kuwalipia ada wanafunzi wote.
Alisema, zitatumika pia kuongeza vyoo katika baadhi ya shule za sekondari zinazokabiliwa na upungufu wa vyoo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri katika kupinga uamuzi huo, alisema, Halmashauri inakabiliwa na upungufu wa milioni 136/- katika bajeti yake ya elimu ya sekondari.
Ni bora Baraza hili likaelekeza matumizi ya fedha hizo katika kutekeleza sera ya elimu ikiwa ndio sera ya Serikali iliyopo madarakani .
Kinabo alisema, wakati Serikali inawalipia watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu, kwa wanafunzi ambao wazazi wao wana uwezo , ni bora wakabeba jukumu wenyewe kuwasomesha.
Uamuzi huo uliopitishwa juzi na baraza hilo linaloongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umepingwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Bernadette Kinabo.
Kinabo amelitaka Baraza la Madiwani kutekeleza sera za maendeleo za Serikali iliyopo madarakani katika miradi ya elimu akisema badala ya halmashauri hiyo kuwasomesha wanafunzi hao, ni bora fedha hizo zikaelekezwa kwenye utekelezaji wa sera za Serikali kwa kujenga maabara na maktaba katika shule zinazotarajiwa kuanzishwa kidato cha tano na sita mwaka huu.
Katika kikao maalumu cha kupitisha bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka 2011/12 kilichofanyika juzi mjini Moshi, Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhari Michael alisema kila mwanafunzi anahitajika kulipiwa ada ya Sh 20,000 kwa mwaka mmoja hali ambayo itafanya jumla ya Sh milioni 170 kutumika kwa ajili hiyo.
Michael ambaye ni Diwani wa Kata ya Bomambuzi (Chadema), alisema licha ya kuwajibika kulipa ada, wazazi wengi wanakabiliwa na changamoto ya kuchelewesha kulipa michango ya zaidi ya Sh 240,000 kwa ajili ya chakula, mishahara, walinzi na wapishi.
Alisema wamefanikiwa kuokoa zaidi ya Sh milioni 351 kutoka katika vyanzo mbali mbali vya mapato ya halmashauri hiyo na kwamba sehemu ya fedha hizo zitatumika kuwalipia ada wanafunzi wote.
Alisema, zitatumika pia kuongeza vyoo katika baadhi ya shule za sekondari zinazokabiliwa na upungufu wa vyoo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri katika kupinga uamuzi huo, alisema, Halmashauri inakabiliwa na upungufu wa milioni 136/- katika bajeti yake ya elimu ya sekondari.
Ni bora Baraza hili likaelekeza matumizi ya fedha hizo katika kutekeleza sera ya elimu ikiwa ndio sera ya Serikali iliyopo madarakani .
Kinabo alisema, wakati Serikali inawalipia watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu, kwa wanafunzi ambao wazazi wao wana uwezo , ni bora wakabeba jukumu wenyewe kuwasomesha.