Mkulo, Maige, Ngeleja kikaangoni TAKUKURU

Kwanza, kama TAKUKURU inawachunguza kwa sababu ya kukutwa na magari tu basi itakuwa haijafanya kitu. Pili, naamini magari hayo ni tone tu katika bahari ya vitu walivyonavyo. Tatu, nawalaumu waandishi wetu wa Kitanzania kwa kutokuwa makini katika uchunguzi wao. Waandishi hawa wako wilayani, mikoani na nchi nzima kwa ujumla. Mtu anaiba, anajenga jumba kuuuuuuuuuuubwa lakini mwandishi anapita anachekelea, huenda anasuburi na yeye zamu yake ifike, aibe. Nyie waandishi investigative journalism mnayosema iko wapi? Mbona mnaweza kufanya investigative journalism hiyo kwa wacheza sinema na wanamiziki hapa Tanzania?
 
Mkuu, jamaa hatuhumiwi kwa kumiliki hayo magari, ila tuhuma ipo kwenye upatikanaji wa hayo magari
What? What's the difference? Rudia tena:"jamaa hatuhumiwi kwa kumiliki hayo magari, ila tuhuma ipo kwenye upatikanaji wa hayo magari..." What's the difference between tuhuma ya kumiliki magari na tuhuma ya kupata magari?

Tatizo na kinachotakiwa kujulikana, wamepata wapi hizo pesa?
Wewe nani kakuuliza umepata wapi hela za kununua hereni hizo za dhahabu na almasi ulizovaa hapo, una mshahara gani wewe Agyman? It is the height of absurdity to second guess people's integrity based on the property they own.

Mkullo alikuwa CEO wa the richest cooperation in the country ( wale wanaotujengea madaraja Kigamboni na ma strip malls ya Wamachinga Ilala), and next to BoT hakuna cooperation Tanzania inayotoa employee benefits kama NSSF
especially mikopo mikopo hii ya kiholela kununua magari, Chief Executive wa NSSF kumiliki ma VX is hardly surprising, jamaa alishakuwa filthy rich kihalali toka enzi za NSSF. Kihalali! Mnasema ana kipato gani? Kwa sheria na mfumo wa goverment administration ya Tanzania "mshahara" halali sio ule unaokuja mwisho wa mwezi tu. Marupurupu ya waziri wa fedha au Chief Executive wa NSSF akienda safari mara tatu tu ananunua Vogue! Kihalali!

Watanzania tunatakiwa tujijengee uwezo wa kuchunguza, kugundua, kushitaki na ku convict viongozi wachafu, sio kusema 'nimemwona mikocheni anaendesha Range Rover," that is incredibly absurd.

 
Wakuu,

Taarifa zilizopenya kwenye viunga hivi zinadai kuwa mawaziri walioachishwa kazi [Mkulo, Maige na Mzee wa Megawatts (Ngeleja)] wako kikaongoni Takukuru na kwamba kila siku lazima waripoti saa tatu asubuhi.

Inadaiwa Mkulo kakutwa na Vogue 2 na Land Cruiser 2 zote mpya hata nylon hazijatolewa kwenye magari yenyewe nyumbani kwake Mikocheni.

Mzee wa Megawatts (Ngeleja) kashfa yake ni ya zile Benz zake alizoleta na Air Cargo na madudu mengine wizarani.

Maige kauza Vitalu vya walafi serikalini kawazidi akili wenzake (isichukuliwe kama namtetea)

Habari zaidi zitafuatia...

We are still waiting Invisible kwa habari zaidi za hawa Mafisadi kama ulivyosema, au sijui ndio umeishia hapo. :photo:
 
Bwana Anh so you mean Mkulo alikuwa akifanya kitu kinaitwa PAC ie primitive accumulation of Capital kuanzia NSSF mpaka MOF
Basi atueleze ile 1.3billion imetumikaje just as spotted na CAG
 
tatizo la takukuru n ajk wao ni ajira ya Dr. Hosea............yawaje hadi leo yupo kazini? kama siyo kulinda ufisadi tu?
 
Kama kikaango chenyewe ni takukuru hapo hakuna kitu,hakuna kitakacho kaangwa hapo mtaambulia harufu tu ya uozo na uvundo,kwani siku zote walikuwa wapi?au ndio walikuwa wanajua lakini walikuwa wanaogopa kwa kuwa walikuwa wenzao ,wakicheza gofu pamoja pale Gymkhana,sasa kwa kuwa mkubwa kawatosa sasa ndo wanapata ujasiri wa kunfunga paka kengele,jamani takukuru ni ya vidagaa na si mapapa.Chenge sio huyo yupo ,mbona hatusikii cha Takukuru wala cha Mwendesha mashtaka Feleshi sijui Fenesi ,Chapa ng'ombe hawezi kumkaanga chapa ng'ombe jamani
 
Takukuru ivunjwe. Kwani hawana jipya bora mishahara ya Takukuru 2waongezee police na magereza kuliko kuwalipa wa2 waco na kazi.
 
What? What's the difference? Rudia tena:"jamaa hatuhumiwi kwa kumiliki hayo magari, ila tuhuma ipo kwenye upatikanaji wa hayo magari..." What's the difference between tuhuma ya kumiliki magari na tuhuma ya kupata magari?
Wewe nani kakuuliza umepata wapi hela za kununua hereni hizo za dhahabu na almasi ulizovaa hapo, una mshahara gani wewe Agyman? It is the height of absurdity to second guess people'
 
Tunasubiri matokeo, TAKUKURU hata si waamini....mwisho wa Siku watatuambia hawana hatia.
 
Watanzania hasa vijana, kwa ufahamu wangu na udadisi juu ya Politics, Power Strugle and Economy naomba nisimame kuhesabiwa miongoni mwa watakao dumu daima upande wa utetezi kwa Ezekiel Maige.

Mzimu mkubwa unaomwandama huyu Mtanzania si nyumba aliyonunua $0.7M cash au njia aliyotumia kupata hiyo pesa bali ujasiri wake kuvuluga syndicate ya waporaji wa maliasili zetu waliodumu kwenye sekta tangu miaka ya mwanzo wa 1960.

Na kubwa la pili ni malengo makubwa na dhamira ya dhati iliyokuwa ikijidhihirisha katika mafanikio yaliyokuwa yameanza kupatikana katika sekta ya Maliasili na Utalii. Maize asingeweza kuyafanya haya bila kuyagusa na kuyabatilisha maslahi makubwa na ya toka enzi ya wakubwa wa nchi hii. Wakubwa hao wengi wako nje ya serikali na hata nje ya nchi. Wananguvu za kubadilisha uongo kuwa ukweli na kinyume chake vilevile. Mwiko aliouvunja Maize ndo Ngeleja alidhani kwa kuuenzi nao watamuenzi kumbe haikuwa hivyo. Ngeleja hajavuluga maslahi ya mkubwa yeyote ila pale wao walipokula yeye kakomba mboga hadi kulamba mwiko.

Rai yangu kwa vijana wasimeze habari kama zinavyowekwa kwenye vyombo vya habari. Na katika yanayoitwa kashfa kuu kupitia kamati za Bunge msichukulie wajumbe kama Malaika na kudhani kila wanalotaarifu ndo ukweli. Hata marefa wana timu zao! Ukitaka kunielewa rejea mswada wa kuondoa kodi kwenye mafuta ya taa uone jinsi Bunge na Kamati zinavyotumika ki-udalali hata katika masuala nyeti.

Nikipata muda nitajitahidi nifumbue mafumbo zaidi labda vijana wenzangu mtanielewa. Hapa mimi si mjumbe wa Maige bali ni muathirika wa ukweli uliopindishwa. Kwa jinsi hii taifa litaendelea kuwakosa watu wenye maamuzi yenye manufaa kwa wananchi. Mbaya zaidi sijazisikia sauti za Wazawa ambao kwa hakika kabisa walipewa vitalu kwa mara ya kwanza toka Tanganyika huru. Simameni jamani, jitokezeni muuweke ukweli huu wazi na Watanzania wasiojua waelewe pumba na mchele.

Ni dhambi kubwa kumuacha Maige kujitetea mwenyewe kwa jambo alilolifanya kwa nia safi kuwanufaisha ninyi Wazawa.

Kwa kuwa umeamua kuwa mtetezi wa Maige labda unaweza kutueleza na hiyo nyumba aliyonunua kwa mapesa yote yale chanzo cha mapato kilikuwa ni nini? Kwa sababu maelezo yake kwamba ana gari 2 za mizigo ni kichekesho kitupu
 
Wakuu,

Taarifa zilizopenya kwenye viunga hivi zinadai kuwa mawaziri walioachishwa kazi [Mkulo, Maige na Mzee wa Megawatts (Ngeleja)] wako kikaongoni Takukuru na kwamba kila siku lazima waripoti saa tatu asubuhi.

Inadaiwa Mkulo kakutwa na Vogue 2 na Land Cruiser 2 zote mpya hata nylon hazijatolewa kwenye magari yenyewe nyumbani kwake Mikocheni.

Mzee wa Megawatts (Ngeleja) kashfa yake ni ya zile Benz zake alizoleta na Air Cargo na madudu mengine wizarani.

Maige kauza Vitalu vya walafi serikalini kawazidi akili wenzake (isichukuliwe kama namtetea)

Habari zaidi zitafuatia...

Inakuwaje lakini kwenye utawala wa Kikwete nafasi nyingi nyeti amewapa watu wenye kumbukumbu chafu mfano Mkulo kupewa wizara ya fedha ilhal huko nyuma aliipeleka PPF kwenye mauti.
 
Wakuu,

Taarifa zilizopenya kwenye viunga hivi zinadai kuwa mawaziri walioachishwa kazi [Mkulo, Maige na Mzee wa Megawatts (Ngeleja)] wako kikaongoni Takukuru na kwamba kila siku lazima waripoti saa tatu asubuhi.

Inadaiwa Mkulo kakutwa na Vogue 2 na Land Cruiser 2 zote mpya hata nylon hazijatolewa kwenye magari yenyewe nyumbani kwake Mikocheni.

Mzee wa Megawatts (Ngeleja) kashfa yake ni ya zile Benz zake alizoleta na Air Cargo na madudu mengine wizarani.

Maige kauza Vitalu vya walafi serikalini kawazidi akili wenzake (isichukuliwe kama namtetea)

Habari zaidi zitafuatia...

Kama ndio hivi basi wawe tayari kuwa 'mwakyembelized'!
 
Eti, haiwezekani wakatolewa hadharani kwa wananchi wenye hasira kali wakamaliza game? mbona vibaka wa simu na kuku huwa wanakutana na wananchi wenye hasira kali? hawa vipi hawaingii kwene category hii? laiti wezi wa kuku nao na wale wa simu wangekuwa wanachunguzwa na Takokuru haki ingepatikana bila ya ncha ya upanga
Mbona kama imekuwa sirisiri sana, ina maana hata watu wa magazeti hawaijainyaka hiyo!
 
Kwenye Serikali ya Tanzania, Wizara ya Malia Asili na Utalii ni Wizara ngumu sana labda hata kuliko Wizara ya Nishati na Madini! Kuna viwanda vya propaganda na ukweli-uowongo (true-Lies) vingi kuliko hata vile vinavyomilikiwa na Waislael ndani ya Serikali ya Marekani. Imekuwa bahati mbaya sana tunao watu wachache sana wenye uwezo wa kubaini mbivu na mbichi. Wengi wetu hata kumbukumbu hatuna kiasi kwamba technique moja inaweza kutumika kuwaadaa watu zaidi katika matukio zaidi ya kumi, wasigundue na bado wakasadiki!

Mazingira ya Balozi Kagasheki kujiuzuru hayatofautiani sana na ya Ezekiel Maige. Hili jambo la Kagasheki kuwa cornered ni suala lililokuwa wazi kabisa toka pale alipoanza kuwakosoa watendaji wake wakuu hadharani.

Watanzania hasa vijana, kwa ufahamu wangu na udadisi juu ya Politics, Power Strugle and Economy naomba nisimame kuhesabiwa miongoni mwa watakao dumu daima upande wa utetezi kwa Ezekiel Maige.

Mzimu mkubwa unaomwandama huyu Mtanzania si nyumba aliyonunua $0.7M cash au njia aliyotumia kupata hiyo pesa bali ujasiri wake kuvuluga syndicate ya waporaji wa maliasili zetu waliodumu kwenye sekta tangu miaka ya mwanzo wa 1960.

Na kubwa la pili ni malengo makubwa na dhamira ya dhati iliyokuwa ikijidhihirisha katika mafanikio yaliyokuwa yameanza kupatikana katika sekta ya Maliasili na Utalii. Maige asingeweza kuyafanya haya bila kuyagusa na kuyabatilisha maslahi makubwa na ya toka enzi ya wakubwa wa nchi hii. Wakubwa hao wengi wako nje ya serikali na hata nje ya nchi. Wananguvu za kubadilisha uongo kuwa ukweli na kinyume chake vilevile. Mwiko aliouvunja Maige ndo Ngeleja alidhani kwa kuuenzi nao watamuenzi kumbe haikuwa hivyo. Ngeleja hajavuluga maslahi ya mkubwa yeyote ila pale wao walipokula yeye kakomba mboga hadi kulamba mwiko.

Rai yangu kwa vijana wasimeze habari kama zinavyowekwa kwenye vyombo vya habari. Na katika yanayoitwa kashfa kuu kupitia kamati za Bunge msichukulie wajumbe kama Malaika na kudhani kila wanalotaarifu ndo ukweli. Hata marefa wana timu zao! Ukitaka kunielewa rejea mswada wa kuondoa kodi kwenye mafuta ya taa uone jinsi Bunge na Kamati zinavyotumika ki-udalali hata katika masuala nyeti.

Nikipata muda nitajitahidi nifumbue mafumbo zaidi labda vijana wenzangu mtanielewa. Hapa mimi si mjumbe wa Maige bali ni muathirika wa ukweli uliopindishwa. Kwa jinsi hii taifa litaendelea kuwakosa watu wenye maamuzi yenye manufaa kwa wananchi. Mbaya zaidi sijazisikia sauti za Wazawa ambao kwa hakika kabisa walipewa vitalu kwa mara ya kwanza toka Tanganyika huru. Simameni jamani, jitokezeni muuweke ukweli huu wazi na Watanzania wasiojua waelewe pumba na mchele.

Ni dhambi kubwa kumuacha Maige kujitetea mwenyewe kwa jambo alilolifanya kwa nia safi kuwanufaisha ninyi Wazawa.

cc: Pasco, Uswe, Gambas
 
Kwenye Serikali ya Tanzania, Wizara ya Malia Asili na Utalii ni Wizara ngumu sana labda hata kuliko Wizara ya Nishati na Madini! Kuna viwanda vya propaganda na ukweli-uowongo (true-Lies) vingi kuliko hata vile vinavyomilikiwa na Waislael ndani ya Serikali ya Marekani. Imekuwa bahati mbaya sana tunao watu wachache sana wenye uwezo wa kubaini mbivu na mbichi. Wengi wetu hata kumbukumbu hatuna kiasi kwamba technique moja inaweza kutumika kuwaadaa watu zaidi katika matukio zaidi ya kumi, wasigundue na bado wakasadiki!

Mazingira ya Balozi Kagasheki kujiuzuru hayatofautiani sana na ya Ezekiel Maige. Hili jambo la Kagasheki kuwa cornered ni suala lililokuwa wazi kabisa toka pale alipoanza kuwakosoa watendaji wake wakuu hadharani.



cc: Pasco, Uswe, Gambas


hiyo LIKE ni heshima kwako kutoka kwangu kwa mchango wako.

Vijana wengi, hawa ambao wanasoma headlines tu na kukimbilia ku-comment, hawaoni haya. ukisema chochote unaambiwa gamba, wakati wengine tuna kadi za CDM na wengi humu ni mashabiki tu, they dont read, they dont think na bado ni GTs
 
Back
Top Bottom