Mkulo anatuongopea?

Anywayz mkuu tunaweza pia kwenda na hiyo namba, assume kuna wafanyakazi 10,000 wanaopata hiyo av. ya mil. nne. Total hapo ni bilion 40.

Hao wanaobaki ukichukua hiyo bil. 200 ukagawa kwa 490,000 unapata 408,000 kila mtu way far from 135,000 wanayolipa kima cha chini na ambao watakuwa kama 80% ya wafanyakazi wote wa serikali. Kifupi ni kwamba hela nyingi kati ya hiyo itakuwa inaenda kwenye posho, na ni kakikundi labda 5% ndiyo wanafaidi. Tukirudi nyuma unakuta madai ya kina Mgaya yalikuwa sahihi kabisa!

dah...!!hesabu zako zinaleta mantiki.hizo pesa zingine wanapeleka wapi hawa watu?
 
Hata mimi ningeweza kumsaidia Zitto kwenye hilo. Kuna thread niliwahi kuweka hapa ya kuipongeza benki ya NMB kama miezi 3 iliyopita watu hawakuilewa vizuri. Serikali yetu ina OD facility ikae kimya tu itaumbuka.

Nakumbuka niliisoma na kutoa comment zangu ulieleza visuri sana.Tunaomba wahusika wailete
 
Naombeni namba ya JK nimpigie ili nimwambie aingie JF asome hizi hoja na kuzifanyia kazi dhidi ya MKULO!!
 
Jana kwenye hotuba yake Dodoma JK alidai kuna waziri alimpigia simu akimuuliza eti ananushe habari fulani baada ya Salva Rweyemamu kuitwanga barua hiyo wizara. Mie nadhani huyo waziri atakuwa Mkulo kwahiyo hakumwamini Salva hadi akamuuliza JK, na jana JK akaamua kumuumbua huyo waziri bila kumtaja jina, then baada ya hapo Bw MKULO akaamua kuitisha hiyo Press Conference kukanusha madai ya Zitto. But Zitto yuko sahihi 100%
 
Mkulo: Serikali haijafilisika

na Mwandishi wetu, Dodoma
Source: Hapa

WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, amesema serikali haijafilisika na haijawahi kukopa fedha kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake.

Mkulo alisema hayo mjini Dodoma jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akijibu tuhuma za Naibu Katibu Mkuu wa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto, aliyesema kuwa serikali imefilisika kiasi cha kukopa kwenye mabenki ya ndani kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake na wabunge.

"Napenda kutumia fursa hii kukanusha vikali madai hayo kuwa ni uongo mtupu na upotishaji unaofanywa kwa maksudi kwa lengo la kujitafutia umaarufu wa kisiasa… napenda kuwaeleza wananchi kuwa taarifa hizo si sahihi. Serikali inalipa watumishi wake mishahara kwa kutumia mapato yake ya ndani pia ina uwezo wa kugharamia shughuli zake nyingine ikiwemo kuendesha Bunge," alisema Mkulo.

Alisema mishahara ya watumishi wa serikali katika kipindi cha kuanzia Desemba hadi Aprili mwaka huu, makusanyo na mapato ya ndani ni malipo ya mishahara ya watumishi wa serikali.

Akifafanua hilo Mkulo alieleza kwamba Desemba mwaka jana serikali ilikusanya sh bilioni 594 ambapo kiasi cha sh bilioni 243.80 kilitumika kulipa mishahara na ziada ya sh bilioni 350.20 ilipatikana wakati Januari mwaka huu makusanyo yalikuwa sh bilioni 433.50 na mishahara iliyolipwa ni sh bilioni 240 huku ziada ya sh bilioni 193 ikiendelea kuwepo.

Mkulo aliendelea kufafanua kuwa Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 huku Machi serikali ikikusanya sh bilioni 567 na ikalipa mishahara sh bilioni 249 na kubaki na ziada ya sh bil. 317 wakati Aprili walikusanya sh bilioni 432 na ikalipa mishahara sh bilioni 246.70 na kubaki na ziada ya sh bilioni 185.40.

"Uchambuzi huu unaonyesha dhahiri kuwa serikali inayo mapato ya kutosha ambayo yanakidhi kulipa mishahara ya watumishi wa serikali kwa ukamilifu na tunayo ziada ya kutosha kugharamia shughuli nyingine za serikali… kwa kawaida serikali inatumia fedha taslimu kulipa gharama zake.

"…Kwa hiyo mapato ya Desemba yanalipa mishahara na matumizi ya Januari. Mapato ya Januari yanalipa matumizi ya Februari na kadhalika, kwa utaratibu huu hakuna hata mwezi mmoja ambao wafanyakazi wa serikali wamekosa mshahara.

"Wanaotoa uongo huo wanatafuta umaarufu wa kisiasa, wamekosa uzalendo kwa taifa lao," alisisitiza Mkulo na kuongeza kwamba posho mbalimbali za wabunge zimelipwa kwa wakati licha ya ongezeko la wawakilishi hao na kutaja stahili zao kuwa ni kwa ajili ya shughuli za kamati za Bunge, posho majimboni, mishahara na mafuta ya kila mwezi.

Aliongeza kuwa mwezi uliopita mishahara ya wabunge ilitolewa Aprili 22 mwaka huu na fedha kwa ajili ya posho mbalimbali nazo zimeshatolewa kwenye ofisi za Bunge. Hivyo alisisitiza na kuelewesha umma kuwa serikali haijashindwa kulipa mishahara ya wabunge na posho zao tofauti na taarifa zilizotolewa na Zitto akidai wabunge hawajalipwa.

Akizungumzia mikopo ya serikali na malengo yake, Mkulo alisema pamoja na kutumia mapato ya ndani kugharamia shughuli zake, hukopa kutoka vyanzo mbalimbali ili kugharamia shughuli za maendeleo. Mikopo hiyo inahusisha ile yenye masharti nafuu na kibiashara.

"Kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011 serikali ilipanga kukopa kiasi cha dola za Marekani milioni 525 ambapo kati hizo dola za Marekani 250 zitagharamia miuondombinu wakati kiasi cha dola za Marekani milioni 175 zitatumika kununua mitambo ya kufua umeme wenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 kwa ajili ya Dar es Salaam na megawati 60 kwa ajili ya Mwanza," alisema.

Mkulo alisema ameamua kutoa ufafanuzi huo ili kuonyesha kwa kifupi kuwa serikali ina uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, mishahara na gharama zote za kuendesha Bunge kutokana na mapato yake ya ndani. Sio kweli na ni upotoshaji wa makusudi wenye malengo ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa.

Alipoulizwa hatua gani atachukuliwa Zitto kutokana na kutoa taarifa za uongo kwa Watanzania, alijibu kuwa yeye alichofanya ni kueleza kile ambacho ndicho sahihi kwa serikali na kwamba wanaoweza kumchukulia hatua Zitto kwa kusema uongo ni Bunge lenyewe. Kutokana na ufafanuzi huo, Mkulo alisema kuwa kikubwa kinachotakiwa hata kama ni mtu wa chama chochote cha kisiasa ama kiongozi kuchuja mambo na kuangalia athari zake kwa kina na si kukurupuka kwa kutafuta umaarufu ambao hauna tija kwa taifa zaidi ya kusababisha matatizo.



My Take:

1. Mkulo anataka kutuaminisha kwamba kazi ya mapato ya serikali ni kulipa mishahara basi. Sasa sijui hata hivyo vikao vya bajeti wanakaa kwa ajili ya nini.

2. Kwa takwimu za mkulo ina maana mpaka sasa serikali ina ziada ya shillingi bilioni elfu moja mia mbili na nane au Shillingi Trilioni 1 na bilioni mbili

3. Inakuwaje sasa serikali yenye ziada ya mihela yote hiyo halafu inaenda kukopa tena?

4. Hivi huu si uwendawazimu? Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 . Mishahara tu ni 62%, hiyo serikali iakuwaje na hela?

5. Kwa mapato hayo na matumizi hayo kwa mishahara tu, si ni indicator ya wazi kabisa kwamba tuna liserikali likuubwa tena lisilo na manufaa yeyote.

6. Hiyo trend ya matumizi hainekani kabisa kwamba jamaa wanajali kubana matumizi wao ni kutumia tu!

7. Kama hizi data nni za kweli, basi Mkulo, JK and the government are failing us miserably.

8. Bunge linaingiajae hapa kumchukulia hatua Zitto kama amesema uwongo?

Mkulo anafikiri watanzania hatujui kinachoendelea serikali kwani kazi yake ni kulipa mishahara? Tunamuomba atupe mapato ya nchi kwa mwaka mzima wa fedha, kilichotumika na kilichopatikana ndio tutafahamu nani mkweli nani muongo. Kutupa mapato ya nchi na kiasi gani kimelipwa katika mshahara ni usanii au serikali kazi yake ni kulipa mishahara tu? Pesa za ulinzi, shughuli za maendeleo, posho za wakubwa, matumizi ya ikulu, safari za viongozi, hospitali, akiba ya chakula, na akiba ya baadae .
 
Tatizo la mawaziri wa Tanzania ni wanadhani wamepewa nafasi hizo ili tu WAKANUSHE madai ya kweli yanayoletwa dihidi ya serikali.

Zitto amesema ukweli mimi ni mfanyakazi wa serikali nina madai ya muda mrefu wiki iliyopita nimefuatilia nikaambiwa na mwajiri kuwa sasa hivi hakuna pesa kabisa LABDA HADI Mwezi wa 9 baada ya bajeti. Wale wote waliopata promotion kuanzia mwezi februari hawajalipwa stahili zao hata mmoja.

MKULLO ANAONYESHA JINSI GANI ALIVYO MJINGA KUKANUSHA TUUU.

Hivi kwenye hii semina elekezi walielekezwa kufanya nini vile? Ndiyo job description yao mzee kama hukujua basi sasa elewa hilo!
 
Mimi japo si mchumi naomba kuelimishwa kidogo.
Hivi bajeti hupangwa vipi? ama mishahara ya wafanyakazi hupangwa kulingana na fedha tulizo nazo ama tunazotegemea kukusanya. Sijui uchumi lakini naona huu uchumi wa nchi hii ni uchumi kichaa, yani wanakusanya mwezi huohuo ndo wanalipa wafanya kazi mwezi huo huo?
Na je ikitokea walipa kodi waka-jongo kwa siku 20 ina maana na mshahara utachelewa kwa siku 20? Mhhhh kuna tatizo kubwa mno. Hata kama kweli ndo wamekusanya kama anavyoeleza , lakini mie bado naona kuna tatizo la msingi kabisa.

Japo sina data ama uthibitsho wowote lakini naona uchumi wa Tanzania utafika kuzimu hata kama sio leo
 
Mimi japo si mchumi naomba kuelimishwa kidogo.
Hivi bajeti hupangwa vipi? ama mishahara ya wafanyakazi hupangwa kulingana na fedha tulizo nazo ama tunazotegemea kukusanya. Sijui uchumi lakini naona huu uchumi wa nchi hii ni uchumi kichaa, yani wanakusanya mwezi huohuo ndo wanalipa wafanya kazi mwezi huo huo?
Na je ikitokea walipa kodi waka-jongo kwa siku 20 ina maana na mshahara utachelewa kwa siku 20? Mhhhh kuna tatizo kubwa mno. Hata kama kweli ndo wamekusanya kama anavyoeleza , lakini mie bado naona kuna tatizo la msingi kabisa.

Japo sina data ama uthibitsho wowote lakini naona uchumi wa Tanzania utafika kuzimu hata kama sio leo

Mkuu mimi pia unajua nimeshtushwa sana na huu mwenendo! Hata tutumie maneno mazuri vp, lakini we have a problem, big problem.
 
Mkuu mimi pia unajua nimeshtushwa sana na huu mwenendo! Hata tutumie maneno mazuri vp, lakini we have a problem, big problem.

Mkuu,
Tena sana kuna tatizo kubwa mno, yawezekana jamaa kataja namba kisahihi. Lakini hizo namba ukizitia ktk stochastic process hazikubali kabisa.
Na hata hivyo, yani nchi inaendeshwa kama familia kule kijijini yani baada ya mlo unaenda kutafuta kubahatisha mlo mwingine mafuta ya kupikia ktk kibaba. Kuna tatizo la msingi sana nchi haiwezi kwenda kwa staili hiyo
 
Anywayz mkuu tunaweza pia kwenda na hiyo namba, assume kuna wafanyakazi 10,000 wanaopata hiyo av. ya mil. nne. Total hapo ni bilion 40.

Hao wanaobaki ukichukua hiyo bil. 200 ukagawa kwa 490,000 unapata 408,000 kila mtu way far from 135,000 wanayolipa kima cha chini na ambao watakuwa kama 80% ya wafanyakazi wote wa serikali. Kifupi ni kwamba hela nyingi kati ya hiyo itakuwa inaenda kwenye posho, na ni kakikundi labda 5% ndiyo wanafaidi. Tukirudi nyuma unakuta madai ya kina Mgaya yalikuwa sahihi kabisa!

Nyambala, kumbuka mwaka jana tu May 3, Mweshimiwa alisema ana "Mbayuwayu" 350,000. Leo May 10 ni mwaka mmoja tu serikali haiwezi tengeneza ajira kwa mbayuwayu wengine (200,000) zaidi ya 50%! Inaonesha pesa nyingi inaishia kwenye ufisadi.
 
Kwa maana hiyo Mheshiwa Mkullo anataka kutuambia kuwa Serikali ya Tanzania ni mchumia tumbo? Makusanyo ni kwa ajili yao tu serikalini? This is very dangerous kwa ustawi wa Tanzania yenye neema!!
 
Mimi kama mfanyakazi wa serikali naidai serikali hela zangu za mshahara. Nilipanda daraja kazini tokea July mwaka jana, hatua iliyoambatana na kupanda kwa mshahara kwa difference ya zaidi ya laki mbili. Hata hivyo hadi sasa bado imekuwa nyimbo kuhusu kulipwa mshahara stahiki, na kupewa malimbikizo yangu (AREAS). Nimejaribu kuuliza mara kadhaa kwa cashier lakini jibu limekuwa serikali bado haina hela za kulipa mshahara mpya. Najua tupo mamia ya watu wenye case kama yangu kwenye taasisi hii ninayofanyia kazi.
Sasa kama Mkullo anasema kuwa serikali haijaishiwa na inalipa mishahara kama kawaida, then watulipe hela zetu. Najua hata huku JF wapo watu wengi wanye case za malimbikizo ya mishahara, posho za likizo, posho za safari na masomo, malipo ya overtime n.k.

Mkullo asitudanganye...
 
Mkulo ni muongo tena wa kuogopwa kama KIMETA

Mimi nina miezi sita tangia nimerudi kutoka likizo na bado sijalipwa pesa zangu za likizo kisa serikali HAINA pesa.

Taasisi ninayoifanyia kazi ina miezi mitatu sasa haijapa OC (Other Charges) kisa serikali haina pesa.

Mwezi wa February (kama sikosei) Serikali ilikata OC kwa zaidi ya 25% ya Wizara, Idara na Taasisi za serikali, OC ambayo ilipitishwa na bunge sababu eti ni kubana matumizi kisa serikali haina pesa. Tatizo Mi-bunge ya CCM haiwezi kumuuliza Mkulo alipata wapi mandate ya kukata OCs zilizopitishwa na Bunge.

Kama kweli Mkulo una ubavu tunaomba ukutane na Mh. Zitto kwenye mdahalo aidha TBC1, ITV or Ch10 tujue bivu ni zipi, kwa ulivyo nanga huwezi kuthubutu.
 
mimi naungana na mwenzangu mmoja kuwa baada ya kuwashukia mawaziri kuwa kwanini wamekuwa kimya kuhubiri mazuri na kujibu hoja na za wapinzani matokeo yake wapinzani ndio wanaoteza hivyo kusidisha uamini wa serikali kwa wananchi kupungua mwanzo wake ndio huu mkulo anakurupuka huku anajaribu kuwaaminisha watanzania kuwa wanachoongea wapinzani haina ukweli wakati hapa mimi mwenyewe shahidi kuwa dada yangu kashindwa kumtumia mdogo wangu hela kisa hawajalipwa mishahara sasa mkullo anakutuaminisha upumbavu wake na serikali yao hongera zitto umesema ukweli
 
Tatizo ninaloliona mimi ni kwamba jana kikwete amewaagiza wawe wanajibu mapigo. sasa wao bila kujipanga wanakurupuka na matokeo yake ndio haya. Mh. Zito ni mbunge na ni ushahidi tosha kwamba hawajalipwa posho kwa sababu serikali ina ukata. angekuwa amelipwa posho asingesema hayo. Je Mh. zito akiamua kuanika mengine kuhusu ukata wa serikali sijui Mkulo atajibuje!!!!!

anasema kwa sababu za kupenda nchi Zitto anatakiwa kukaa kimya kwani tutakosa misaada mingi sana wakijua tumefilisika wakati wao wanatoa pesa. Yaani, eti ndio Waziri anajibu hivyo!!!:A S cry::A S cry::A S cry::A S cry:
 
Topic zingine Bana..hata hujui vipi tuzijadili.... Hadithi za muuza kahawa hizi.
Nimesema toka mwanzo wewe ni mgonjwa, hujui tujadili vipi????????? Watu hawajalipwa mishahara na wabunge hawajalipwa posho,umee elewa jadili sasa!!!!!!! Au wewe pia ni mmoja wao????????
 
Nikisoma thread kama hii huwa najiuliza, waandishi wa habari sio great thinkers kama wana JF? Mbona hoja zinazojadiliwa hapa hawakumuuliza na kisha kutuhabarisha majibu yake?

Mfano: mbona waandishi wa habari hawakumuuliza baada ya kulipa mishahara kilichobaki kwa nini anaita ziada as if serikali haina matumizi mengine?

Nashindwa kuelewa!!!!!?
 
Mkuu soma bajeti 2010/2011 utayajua hayo yote. Kwani serikali iliisha sema itakopa kwa ajili ya pesa za maendeleo (development expenditures) na hilo ndilo wanalo fanya

Unaweza ukasema halafu usitekeleze na hii ndio aina ya serikali ya kj, maneno kibaoooo no vitendo. Semina elekezi, safari, sijui ziara.....wacha nijinyamazie manake hasira tupu.
 
Back
Top Bottom