Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Mkulo: Serikali haijafilisika
na Mwandishi wetu, Dodoma
Source: Hapa
WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, amesema serikali haijafilisika na haijawahi kukopa fedha kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake.
Mkulo alisema hayo mjini Dodoma jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akijibu tuhuma za Naibu Katibu Mkuu wa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto, aliyesema kuwa serikali imefilisika kiasi cha kukopa kwenye mabenki ya ndani kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake na wabunge.
"Napenda kutumia fursa hii kukanusha vikali madai hayo kuwa ni uongo mtupu na upotishaji unaofanywa kwa maksudi kwa lengo la kujitafutia umaarufu wa kisiasa… napenda kuwaeleza wananchi kuwa taarifa hizo si sahihi. Serikali inalipa watumishi wake mishahara kwa kutumia mapato yake ya ndani pia ina uwezo wa kugharamia shughuli zake nyingine ikiwemo kuendesha Bunge," alisema Mkulo.
Alisema mishahara ya watumishi wa serikali katika kipindi cha kuanzia Desemba hadi Aprili mwaka huu, makusanyo na mapato ya ndani ni malipo ya mishahara ya watumishi wa serikali.
Akifafanua hilo Mkulo alieleza kwamba Desemba mwaka jana serikali ilikusanya sh bilioni 594 ambapo kiasi cha sh bilioni 243.80 kilitumika kulipa mishahara na ziada ya sh bilioni 350.20 ilipatikana wakati Januari mwaka huu makusanyo yalikuwa sh bilioni 433.50 na mishahara iliyolipwa ni sh bilioni 240 huku ziada ya sh bilioni 193 ikiendelea kuwepo.
Mkulo aliendelea kufafanua kuwa Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 huku Machi serikali ikikusanya sh bilioni 567 na ikalipa mishahara sh bilioni 249 na kubaki na ziada ya sh bil. 317 wakati Aprili walikusanya sh bilioni 432 na ikalipa mishahara sh bilioni 246.70 na kubaki na ziada ya sh bilioni 185.40.
"Uchambuzi huu unaonyesha dhahiri kuwa serikali inayo mapato ya kutosha ambayo yanakidhi kulipa mishahara ya watumishi wa serikali kwa ukamilifu na tunayo ziada ya kutosha kugharamia shughuli nyingine za serikali… kwa kawaida serikali inatumia fedha taslimu kulipa gharama zake.
"…Kwa hiyo mapato ya Desemba yanalipa mishahara na matumizi ya Januari. Mapato ya Januari yanalipa matumizi ya Februari na kadhalika, kwa utaratibu huu hakuna hata mwezi mmoja ambao wafanyakazi wa serikali wamekosa mshahara.
"Wanaotoa uongo huo wanatafuta umaarufu wa kisiasa, wamekosa uzalendo kwa taifa lao," alisisitiza Mkulo na kuongeza kwamba posho mbalimbali za wabunge zimelipwa kwa wakati licha ya ongezeko la wawakilishi hao na kutaja stahili zao kuwa ni kwa ajili ya shughuli za kamati za Bunge, posho majimboni, mishahara na mafuta ya kila mwezi.
Aliongeza kuwa mwezi uliopita mishahara ya wabunge ilitolewa Aprili 22 mwaka huu na fedha kwa ajili ya posho mbalimbali nazo zimeshatolewa kwenye ofisi za Bunge. Hivyo alisisitiza na kuelewesha umma kuwa serikali haijashindwa kulipa mishahara ya wabunge na posho zao tofauti na taarifa zilizotolewa na Zitto akidai wabunge hawajalipwa.
Akizungumzia mikopo ya serikali na malengo yake, Mkulo alisema pamoja na kutumia mapato ya ndani kugharamia shughuli zake, hukopa kutoka vyanzo mbalimbali ili kugharamia shughuli za maendeleo. Mikopo hiyo inahusisha ile yenye masharti nafuu na kibiashara.
"Kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011 serikali ilipanga kukopa kiasi cha dola za Marekani milioni 525 ambapo kati hizo dola za Marekani 250 zitagharamia miuondombinu wakati kiasi cha dola za Marekani milioni 175 zitatumika kununua mitambo ya kufua umeme wenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 kwa ajili ya Dar es Salaam na megawati 60 kwa ajili ya Mwanza," alisema.
Mkulo alisema ameamua kutoa ufafanuzi huo ili kuonyesha kwa kifupi kuwa serikali ina uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, mishahara na gharama zote za kuendesha Bunge kutokana na mapato yake ya ndani. Sio kweli na ni upotoshaji wa makusudi wenye malengo ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa.
Alipoulizwa hatua gani atachukuliwa Zitto kutokana na kutoa taarifa za uongo kwa Watanzania, alijibu kuwa yeye alichofanya ni kueleza kile ambacho ndicho sahihi kwa serikali na kwamba wanaoweza kumchukulia hatua Zitto kwa kusema uongo ni Bunge lenyewe. Kutokana na ufafanuzi huo, Mkulo alisema kuwa kikubwa kinachotakiwa hata kama ni mtu wa chama chochote cha kisiasa ama kiongozi kuchuja mambo na kuangalia athari zake kwa kina na si kukurupuka kwa kutafuta umaarufu ambao hauna tija kwa taifa zaidi ya kusababisha matatizo.
My Take:
1. Mkulo anataka kutuaminisha kwamba kazi ya mapato ya serikali ni kulipa mishahara basi. Sasa sijui hata hivyo vikao vya bajeti wanakaa kwa ajili ya nini.
2. Kwa takwimu za mkulo ina maana mpaka sasa serikali ina ziada ya shillingi bilioni elfu moja mia mbili na nane au Shillingi Trilioni 1 na bilioni mbili
3. Inakuwaje sasa serikali yenye ziada ya mihela yote hiyo halafu inaenda kukopa tena?
4. Hivi huu si uwendawazimu? Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 . Mishahara tu ni 62%, hiyo serikali iakuwaje na hela?
5. Kwa mapato hayo na matumizi hayo kwa mishahara tu, si ni indicator ya wazi kabisa kwamba tuna liserikali likuubwa tena lisilo na manufaa yeyote.
6. Hiyo trend ya matumizi hainekani kabisa kwamba jamaa wanajali kubana matumizi wao ni kutumia tu!
7. Kama hizi data nni za kweli, basi Mkulo, JK and the government are failing us miserably.
8. Bunge linaingiajae hapa kumchukulia hatua Zitto kama amesema uwongo?
na Mwandishi wetu, Dodoma
Source: Hapa
WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, amesema serikali haijafilisika na haijawahi kukopa fedha kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake.
Mkulo alisema hayo mjini Dodoma jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akijibu tuhuma za Naibu Katibu Mkuu wa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto, aliyesema kuwa serikali imefilisika kiasi cha kukopa kwenye mabenki ya ndani kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake na wabunge.
"Napenda kutumia fursa hii kukanusha vikali madai hayo kuwa ni uongo mtupu na upotishaji unaofanywa kwa maksudi kwa lengo la kujitafutia umaarufu wa kisiasa… napenda kuwaeleza wananchi kuwa taarifa hizo si sahihi. Serikali inalipa watumishi wake mishahara kwa kutumia mapato yake ya ndani pia ina uwezo wa kugharamia shughuli zake nyingine ikiwemo kuendesha Bunge," alisema Mkulo.
Alisema mishahara ya watumishi wa serikali katika kipindi cha kuanzia Desemba hadi Aprili mwaka huu, makusanyo na mapato ya ndani ni malipo ya mishahara ya watumishi wa serikali.
Akifafanua hilo Mkulo alieleza kwamba Desemba mwaka jana serikali ilikusanya sh bilioni 594 ambapo kiasi cha sh bilioni 243.80 kilitumika kulipa mishahara na ziada ya sh bilioni 350.20 ilipatikana wakati Januari mwaka huu makusanyo yalikuwa sh bilioni 433.50 na mishahara iliyolipwa ni sh bilioni 240 huku ziada ya sh bilioni 193 ikiendelea kuwepo.
Mkulo aliendelea kufafanua kuwa Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 huku Machi serikali ikikusanya sh bilioni 567 na ikalipa mishahara sh bilioni 249 na kubaki na ziada ya sh bil. 317 wakati Aprili walikusanya sh bilioni 432 na ikalipa mishahara sh bilioni 246.70 na kubaki na ziada ya sh bilioni 185.40.
"Uchambuzi huu unaonyesha dhahiri kuwa serikali inayo mapato ya kutosha ambayo yanakidhi kulipa mishahara ya watumishi wa serikali kwa ukamilifu na tunayo ziada ya kutosha kugharamia shughuli nyingine za serikali… kwa kawaida serikali inatumia fedha taslimu kulipa gharama zake.
"…Kwa hiyo mapato ya Desemba yanalipa mishahara na matumizi ya Januari. Mapato ya Januari yanalipa matumizi ya Februari na kadhalika, kwa utaratibu huu hakuna hata mwezi mmoja ambao wafanyakazi wa serikali wamekosa mshahara.
"Wanaotoa uongo huo wanatafuta umaarufu wa kisiasa, wamekosa uzalendo kwa taifa lao," alisisitiza Mkulo na kuongeza kwamba posho mbalimbali za wabunge zimelipwa kwa wakati licha ya ongezeko la wawakilishi hao na kutaja stahili zao kuwa ni kwa ajili ya shughuli za kamati za Bunge, posho majimboni, mishahara na mafuta ya kila mwezi.
Aliongeza kuwa mwezi uliopita mishahara ya wabunge ilitolewa Aprili 22 mwaka huu na fedha kwa ajili ya posho mbalimbali nazo zimeshatolewa kwenye ofisi za Bunge. Hivyo alisisitiza na kuelewesha umma kuwa serikali haijashindwa kulipa mishahara ya wabunge na posho zao tofauti na taarifa zilizotolewa na Zitto akidai wabunge hawajalipwa.
Akizungumzia mikopo ya serikali na malengo yake, Mkulo alisema pamoja na kutumia mapato ya ndani kugharamia shughuli zake, hukopa kutoka vyanzo mbalimbali ili kugharamia shughuli za maendeleo. Mikopo hiyo inahusisha ile yenye masharti nafuu na kibiashara.
"Kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011 serikali ilipanga kukopa kiasi cha dola za Marekani milioni 525 ambapo kati hizo dola za Marekani 250 zitagharamia miuondombinu wakati kiasi cha dola za Marekani milioni 175 zitatumika kununua mitambo ya kufua umeme wenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 kwa ajili ya Dar es Salaam na megawati 60 kwa ajili ya Mwanza," alisema.
Mkulo alisema ameamua kutoa ufafanuzi huo ili kuonyesha kwa kifupi kuwa serikali ina uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, mishahara na gharama zote za kuendesha Bunge kutokana na mapato yake ya ndani. Sio kweli na ni upotoshaji wa makusudi wenye malengo ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa.
Alipoulizwa hatua gani atachukuliwa Zitto kutokana na kutoa taarifa za uongo kwa Watanzania, alijibu kuwa yeye alichofanya ni kueleza kile ambacho ndicho sahihi kwa serikali na kwamba wanaoweza kumchukulia hatua Zitto kwa kusema uongo ni Bunge lenyewe. Kutokana na ufafanuzi huo, Mkulo alisema kuwa kikubwa kinachotakiwa hata kama ni mtu wa chama chochote cha kisiasa ama kiongozi kuchuja mambo na kuangalia athari zake kwa kina na si kukurupuka kwa kutafuta umaarufu ambao hauna tija kwa taifa zaidi ya kusababisha matatizo.
My Take:
1. Mkulo anataka kutuaminisha kwamba kazi ya mapato ya serikali ni kulipa mishahara basi. Sasa sijui hata hivyo vikao vya bajeti wanakaa kwa ajili ya nini.
2. Kwa takwimu za mkulo ina maana mpaka sasa serikali ina ziada ya shillingi bilioni elfu moja mia mbili na nane au Shillingi Trilioni 1 na bilioni mbili
3. Inakuwaje sasa serikali yenye ziada ya mihela yote hiyo halafu inaenda kukopa tena?
4. Hivi huu si uwendawazimu? Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 . Mishahara tu ni 62%, hiyo serikali iakuwaje na hela?
5. Kwa mapato hayo na matumizi hayo kwa mishahara tu, si ni indicator ya wazi kabisa kwamba tuna liserikali likuubwa tena lisilo na manufaa yeyote.
6. Hiyo trend ya matumizi hainekani kabisa kwamba jamaa wanajali kubana matumizi wao ni kutumia tu!
7. Kama hizi data nni za kweli, basi Mkulo, JK and the government are failing us miserably.
8. Bunge linaingiajae hapa kumchukulia hatua Zitto kama amesema uwongo?