Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
Wana JF, Ningewaleteeni taarifa yote ya Mkulo kukana kuhusika kwake, lakini nawaleteeni kipande tu maana taarifa yake ni ndefu sanaaa. Narudia tena usizingatie namba hizo nimepunguza baadhi ya maneno katika taarifa hii ni ndefu mnoooo.
1.0 Tungependa kutoa ufafanuzi kuhusu hoja hizo kama ifuatavyo:- Kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere hakikuuzwa na Wizara ya Fedha, wala na Waziri wa Fedha. Kiwanja hicho kiliuzwa na aliyekuwa Mwenyekiti na Kaimu Mkurugenzi wa CHC kinyume na maelekezo ya Wizara ya Fedha na Kamati ya Wataalam (DTT), kwamba kiwanja hicho kiuzwe kwa bei ya soko kwa kuzingatia Sheria na Taratibu.
2.0 Ukweli upo kwamba, baada ya maelekezo ya Wizara ya Fedha kwamba bei ya soko na taratibu na sheria zitumike, Kamati ya Wataalamu wa Serikali, ilikaa na kushauri kwamba taratibu na sheria ni kutangaza ili kupata bei ya soko.
3.0 Bodi ya CHC ilikaa na kujadili maelekezo ya Wizara ya Fedha na ushauri wa Kamati ya Wataalam. Baadhi ya Wajumbe wa Bodi walishindwa kuelewa maana ya taratibu na sheria na bei ya soko, hivyo Bodi iliagiza Waziri wa Fedha aombwe ufafanuzi. Mwenyekiti na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC walitumwa na Bodi wamwone Waziri wa Fedha ili warudishe majibu kwenye Bodi. Waziri wa Fedha alitoa maelezo kwao kwamba, tayari alishatoa maelekezo kwa maandishi hivyo waendelee kwa kuzingatia maelekezo yaliyotolewa.
4.0 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC hawakurudi kwenye Bodi baada ya kupata ufafanuzi kutoka kwa Waziri wa Fedha, bali waliamua kuuza kiwanja hicho kwa bei ya Mtathmini, badala ya kutangaza na kupata bei ya soko kama walivyoelekezwa na Wizara ya Fedha na Kamati ya Wataalam. Aidha, hawakurudi kwa Wizara ya Fedha kutoa taarifa ya utekelezaji wa maelekezo ya Wizara.
5.0 Tuhuma kuhusu kwamba, Wizara ya Fedha ilihusika katika uuzwaji wa kiwanja hicho kwa kutoa maagizo kwa uongozi wa Shirika kuuza kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere bila kuishirikisha Bodi ya Wakurugenzi, hazina ukweli.
6.0 Kwa kuzingatia maelekezo ya Waziri wa Fedha ni dhahiri kuwa, Mhe. Waziri wa Fedha, hakuhusika na uuzaji wa kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere na wala hakuingilia utendaji wa CHC. Maelekezo aliyotoa yaliitaka CHC ifanye maamuzi kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.Badala yake, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC waliamua kuuza kiwanja hicho bila kuzingatia ushauri wa Kamati ya Wataalam (DTT) na maelekezo ya Wizara ya Fedha.
7.0 Kwa misingi hiyo, tuhuma kwamba, Mhe. Waziri wa Fedha alihusika na uuzaji wa kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere sio za ukweli.
1.0 Tungependa kutoa ufafanuzi kuhusu hoja hizo kama ifuatavyo:- Kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere hakikuuzwa na Wizara ya Fedha, wala na Waziri wa Fedha. Kiwanja hicho kiliuzwa na aliyekuwa Mwenyekiti na Kaimu Mkurugenzi wa CHC kinyume na maelekezo ya Wizara ya Fedha na Kamati ya Wataalam (DTT), kwamba kiwanja hicho kiuzwe kwa bei ya soko kwa kuzingatia Sheria na Taratibu.
2.0 Ukweli upo kwamba, baada ya maelekezo ya Wizara ya Fedha kwamba bei ya soko na taratibu na sheria zitumike, Kamati ya Wataalamu wa Serikali, ilikaa na kushauri kwamba taratibu na sheria ni kutangaza ili kupata bei ya soko.
3.0 Bodi ya CHC ilikaa na kujadili maelekezo ya Wizara ya Fedha na ushauri wa Kamati ya Wataalam. Baadhi ya Wajumbe wa Bodi walishindwa kuelewa maana ya taratibu na sheria na bei ya soko, hivyo Bodi iliagiza Waziri wa Fedha aombwe ufafanuzi. Mwenyekiti na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC walitumwa na Bodi wamwone Waziri wa Fedha ili warudishe majibu kwenye Bodi. Waziri wa Fedha alitoa maelezo kwao kwamba, tayari alishatoa maelekezo kwa maandishi hivyo waendelee kwa kuzingatia maelekezo yaliyotolewa.
4.0 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC hawakurudi kwenye Bodi baada ya kupata ufafanuzi kutoka kwa Waziri wa Fedha, bali waliamua kuuza kiwanja hicho kwa bei ya Mtathmini, badala ya kutangaza na kupata bei ya soko kama walivyoelekezwa na Wizara ya Fedha na Kamati ya Wataalam. Aidha, hawakurudi kwa Wizara ya Fedha kutoa taarifa ya utekelezaji wa maelekezo ya Wizara.
5.0 Tuhuma kuhusu kwamba, Wizara ya Fedha ilihusika katika uuzwaji wa kiwanja hicho kwa kutoa maagizo kwa uongozi wa Shirika kuuza kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere bila kuishirikisha Bodi ya Wakurugenzi, hazina ukweli.
6.0 Kwa kuzingatia maelekezo ya Waziri wa Fedha ni dhahiri kuwa, Mhe. Waziri wa Fedha, hakuhusika na uuzaji wa kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere na wala hakuingilia utendaji wa CHC. Maelekezo aliyotoa yaliitaka CHC ifanye maamuzi kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.Badala yake, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC waliamua kuuza kiwanja hicho bila kuzingatia ushauri wa Kamati ya Wataalam (DTT) na maelekezo ya Wizara ya Fedha.
7.0 Kwa misingi hiyo, tuhuma kwamba, Mhe. Waziri wa Fedha alihusika na uuzaji wa kiwanja Na. 10 barabara ya Nyerere sio za ukweli.
KATIBU MKUU
WIZARA YA FEDHA
APRILI, 2012
WIZARA YA FEDHA
APRILI, 2012