Mkuchika: Upinzani umepoteza umaarufu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
* Asema uroho wa madaraka unawamaliza
* Vigogo waikimbia CHADEMA wajiunga CCM


Na David Paul, Biharamulo (Uhuru)

UMAARUFU wa vyama vya upinzani nchini umekuwa ukishuka kadri siku zinavyokwenda kutokana na malumbano ya kila mara ndani ya vyama hivyo, yanayosababishwa na viongozi wakuu kung’ang’ania madaraka.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), George Mkuchika, alisema hayo kwa nyakati tofauti, alipohutubia mikutano ya hadhara katika kata za Lusahunga na Biharamulo Mjini, kumnadi mgombea ubunge wa CCM katika jimbo la Biharamulo Magharibi, Oscar Mukasa.

Alisema kuporomoka kwa umaarufu wa wapinzani kunatokana na malumbano ya mara kwa mara ya baadhi ya viongozi yanayosababishwa na uroho wa madaraka.

Kutokana na hilo, alisema wapinzani wasipewe ridhaa ya kuongoza, kwani nchi itaharibika.

“Hawa wenzetu wa upinzani wamekuwa wakisimama majukwaani na kuwaeleza wananchi kuwa mmekichoka CCM, nasema si kweli, Watanzania bado mna imani kubwa na CCM, na ushahidi tunao, angalieni wenyewe takwimu za matokeo ya uchaguzi uliopita kuanzia mwaka 1995.

“Mwaka 1995 mgombea wa CCM Benjamin Mkapa, alipata asilimia 62 ya kura zote na mwaka 2000, alipata asilimia 72. Mwaka 2005 Rais Kikwete (Jakaya) alipata asilimia 80, ni wazi kuwa wananchi bado wana imani kubwa na CCM,” alisema.

Akizungumzia viti vya ubunge, alisema mwaka 1995 vyama vya upinzani vilipata 49, huku katika uchaguzi wa mwaka 2000 idadi ikipungua na kuwa viti 29.

Mkuchika alisema hali iliendelea kuwa mbaya zaidi katika uchaguzi wa mwaka 2005, ambapo vyama vya upinzani viliambulia viti 26 kati ya majimbo 232 yaliyopo.

Kutokana na takwimu hizo, Mkuchika aliwaomba wakazi wa Biharamulo Magharibi kuhakikisha hawapotezi kura zao kwa kuwachagua wapinzani, ambao kimsingi wameonekana kupoteza mwelekeo na imani kwa wananchi.

Uchaguzi katika jimbo hilo unafanyika Julai 5, mwaka huu, ambapo wapigakura wamehakikishiwa usalama wa kutosha ili kuwawezesha kujitokeza kupiga kura kwa wingi.

Wakati huo huo, CHADEMA kimeendelea kupata pigo katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Biharamulo Magharibi, baada ya CCM kuendelea kukisambaratisha.

Licha ya hivi karibuni wanachama wake takriban 60 kujiunga na Chama Cha Mapinduzi kutoka maeneo ya Soko Kuu la Biharamulo, majuzi Katibu Mwenezi wake wa wilaya alijiunga CCM.

Katibu Mwenezi huyo wa CHADEMA, David Mayala, alikihama chama hicho mwishoni mwa wiki iliyopita, baada ya kuhudhuria mkutano wa kampeni kumnadi mgombea wa CCM, Oscar Mukasa, uliofanyika kwenye kijiji cha Luziba.

Akizungumza kwenye mkutano huo baada ya kukabidhi kadi ya CHADEMA kwa viongozi wa CCM, Mayala alisema ameamua kujiunga na Chama Cha Mapinduzi baada ya kuvutiwa na sera zake.

Mayala alidai CHADEMA hakina dira na kuongeza: “Jamani msidanganywe hata kidogo, kule upinzani hakuna kitu kipya ni kupoteza muda tu.

“CHADEMA wana malengo binafsi si kama ilivyo CCM ambayo inalenga kuwasaidia wananchi,” alisema huku akishangiliwa na umati uliohudhuria mkutano huo.

Kwa mujibu wa Mayala, pia amekerwa na sera za CHADEMA zinazolenga vurugu, akisema chama hicho hakistahili kupewa kura.

Mwingine aliyejiunga na CCM kutoka CHADEMA ni Katibu wa tawi la Nemba, lililoko kata ya Nyabuso, ambayo ni ngome ya chama hicho, Lucas Nyamegoro.

Nyamegoro alijiunga na CCM juzi, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mbindi, kata ya Nyabusozi.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Nyamegoro aliwataka wananchi wasitishwe au kurubuniwa na wapinzani, hususan CHADEMA kwa kuwa chama hicho kinajali maslahi binafsi.

Nyamegoro alisema hakuna chama kinachoweza kuwaletea maendeleo wananchi na kutatua kero zinazowakabili zaidi ya CCM.
 
Sio kweli hata kidogo maana katika kipindi ambacho CCM wamebabaika hata kuanguka kwa Serikali ni mwaka 2005-2010, Mambo yote ya ufisadi, wizi na mali za umma ni kwa ajili ya upinzani. Hivyo kusema Umaarufu wa Upinzania umeshuka ni kweli, Soma Ripoti ya REDET na utasema kuwa wao ndio wameshuka umaarufu wao, na pia kuna Report ya kuwa Baraza la Mawaziri limeshuka Umaarufu wake na
 
Madai ni ya kada na kiongozi wa CCM kwenye kampeni na ripoti imetolewa na gazeti lisilo huru la CCM - Uhuru. Ambacho hawasemi ni wizi, rushwa na vitisho dhidi ya upinzani na wananchi kwa ujumla vinavyozidi kupata umaarufu na kupewa kipaumbele ndani ya CCM. Kudai kuwa upinzani unapoteza umaarufu ina maana kuwa wananchi wanabariki kuendelea kuibiwa, wanachangamkia rushwa na wanakubali na kufurahia kuonewa - mbona hii haiingii akilini ?
Kama hii ingekuwa kweli
Wabunge wao watukuka
wangepitisha bajeti ya serikali
Bila woga wala vitisho kutoka kwa Spika.
 
No, serikali ndiyo inayochochea rabsha ktk vyama vya upinzani kwa kung'ang'ania sheria kandamizi zidi ya vyama vya upinzani.
 
Mbona wao kama kweli Makada hawasema kuwa CCM wamepata umaarufu na Mambo ya ufisadi na wizi wa mali za umma na kujigamba miongoni mwa wapiga kura, ukiona watu kama hawa na tena huyu Mkuchika ndio aliyekuwa na kauli tata sana mara nyingi na kuwa contradicts sana na wakubwa zake, Wasije kujiogopea kuwa mwaka 2010 watu watachagua mafiga matatu
 
CCM wana endeleza mazoezi ya kuwanunua na ngoma ni baada ya uchaguzi.Wakumbuke Mtikila alifikia hatua kama yao lakini hata baada ya kipigo balanve hajapata wakamuulize .
 
Umaarufu wa CCM ndio umeshuka na Tazama hata Umaarufu wa Mzee wa Kaya nao umeshuka na kuzidiwa hata Zitto Kabwe, Wasijidanganye CCM kuwa Umaarufu umeshuka sio kweli hata Kidogo, Report ya Redet inasema haya
 
Huyu Mkuchika si anajulikana? Alipigwa pini na Jukwaa la wahariri asinukuliwe na magazeti baada ya kulifungia gazeti la Mwanahalisi kwa kusema uongo -- yaani kulisingizia liliandika uongo. Sijui aliwahonga baadhi ya wahariri wa jukwaa ambo walipiga kura kumfungulia pini baada ya kifungo cha gazeti kumalizika. Wengi walitaka pini iendelee -- asinukuliwe na magazeti huru kamwe - hadi amalize kipindi cha uwaziri wake.

Ni mtu ambaye hujisemea hovyo hovyo -- alitamka Bungeni eti CNN ni mali ya serikali ya Marekani!
 
Last edited by a moderator:
Could Mkuchika have said differently? And could Uhuru have reported diffently? Sometimes the source of info determines the worthness of that info. On this one, I have decided to judge the book on the basis of its cover, not even the title!
 
Does anyone here take seriously what Mkuchika says or thinks? Not me. But putting it in the context of an election that is being fought, I guess Mkuchika has no option but to put down the opposition.
 
Could Mkuchika have said differently? And could Uhuru have reported diffently? Sometimes the source of info determines the worthness of that info. On this one, I have decided to judge the book on the basis of its cover, not even the title!
I agree with you mkuu. In the past 15 years or so it looks like one of tasks of some state organs were to confuse if not to cause chaos in the opposition political parties. That is why I tend to think as we slowly moving, the real opposition parties have started to emerge. I think some of these guys who change their political colours represent those who were planted to confuse Tanzanians that opposition could never be the best option.
 
ukisoma gazeti la uhuru kwa wiki moja tu inatosha kukufanya uwe mwehu sasa sijui mhariri wake kama akili zake bado nzima.
 
ukisoma gazeti la uhuru kwa wiki moja tu inatosha kukufanya uwe mwehu sasa sijui mhariri wake kama akili zake bado nzima.

Hee magezi, kweli we una magezi sana! does magezi means akili in your local language?

Back to the issue,
Mimi binafsi nikisha soma kichwa cha habari kwamba kaongea Mkuchika, huwa sipotezi hata muda wangu kumalizia habari nzima, sasa ikichanganya na kwamba imeletwa na UHURU! ni afadhali nisome...
 
Could Mkuchika have said differently? And could Uhuru have reported diffently?

On this one, I have decided to judge the book on the basis of its cover, not even the title!

you have a point bwana!it is a part of campaign
 
Huo ni mtazamo wako tafuta vingine vya kudanganya suala la umaarufu kuongezeka,ni wazi na inajulikana chama ambacho kinakosha mioyo ya watz kwa sasa siyo sisiemuu.ngojeni njia yenu itageuka giza na mtakosa mwelekeo.uongo una mwisho.
 
Ningekuwa Mkuchika i would have said the same. Hata George Bush alivyokuja hapa TAnzanmia alipouluzwa kuwa nani atashindwa uchaguzi wa Marekani alisema wazi kabisa, chama chake kitashinda, lakini pia alijua wazi kabisa kuwa Obama atashinda. Kwa hiyo hapa sioni la kumlaumu Mkuchika.
 
Does anyone here take seriously what Mkuchika says or thinks? Not me. But putting it in the context of an election that is being fought, I guess Mkuchika has no option but to put down the opposition.

Mkuu heshima mbele. Mimi na wewe tunaweza tusimchukulie seriously lakini sisi siyo wapiga kura. You have to look at it at the point of view of his audience. Je hao aliokuwa anawaambia hivyo do they know what we know? Do they have access to the information that we are privileged to have? Mkuchika obviously knows his audience and he knew they wouldn't question his words. This is what we call political propaganda.
 
mkuchika had statistics on his side.....atleast hakutoa tu maneno from thin air.
hao wanaomsikiliza wata judge maneno yake kwa mujibu wa statistics alizotoa ambazo zinaonyesha vyama vya upinzani vinakosa umaarufu.

hadi pale kwenye uchaguzi ujao vyama vya upinzani vitakapopata viti vingi zaidi, ni wazi kuwa ccm inathaminiwa zaidi ya upinzani.
 
Back
Top Bottom