akilimtindi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 421
- 83
Wakuu Samahanini nilipotea kwa muda kwenye kutafuta katika hali yetu ya kawaida. Nimerudi na naomba mniruhusu kuendelea kuchangia, yangu leo machache.
Hivi ni kweli huyu ajulikanaye kama Mheshimiwa Captain Kamanda Mkuchika ndiye Waziri wetu wa Habari tunayemtegemea? Nimemshangaa kwa muda maana namsikia kwa muda akiongea mambo ambayo siyaelewi. Kwanza nilimsikia akisema anapiga marufuku wimbo wa Taifa kwenye simu, pili leo namsikia akitema pumba nyingine wakati anakabidhi bendera ya taifa kwa timu yetu kwenda Sudani, kasema Baba wa Taifa alivyofanikiwa kumtoa Idd Amin alienda hadi kwake Uganda kumchapia hukohuko. Je, huo ndio mfano halisi wa kuwapa timu yetu ya taifa? Je, timu ya taifa ya Sudani yaweza kufananishwa na Idd Amin?
Swali langu la msingi hili hapa, hivi haya yote ni matamshi ya Serikali au ya huyu Mheshimiwa saaaana Captain Kamanda Mkuchika?
Hivi ni kweli huyu ajulikanaye kama Mheshimiwa Captain Kamanda Mkuchika ndiye Waziri wetu wa Habari tunayemtegemea? Nimemshangaa kwa muda maana namsikia kwa muda akiongea mambo ambayo siyaelewi. Kwanza nilimsikia akisema anapiga marufuku wimbo wa Taifa kwenye simu, pili leo namsikia akitema pumba nyingine wakati anakabidhi bendera ya taifa kwa timu yetu kwenda Sudani, kasema Baba wa Taifa alivyofanikiwa kumtoa Idd Amin alienda hadi kwake Uganda kumchapia hukohuko. Je, huo ndio mfano halisi wa kuwapa timu yetu ya taifa? Je, timu ya taifa ya Sudani yaweza kufananishwa na Idd Amin?
Swali langu la msingi hili hapa, hivi haya yote ni matamshi ya Serikali au ya huyu Mheshimiwa saaaana Captain Kamanda Mkuchika?