Enny
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 962
- 130
Kuna Jamaa ana mpenzi wake, wanakaa tofauti lakini wapo karibu sana. Jamaa anafunguo za nyumba ya mpenzi wake kwa hiyo asipomkuta hufungua na kukaa akimsubiria halikadharika na demu hivyohivyo. Sasa kasheshe imejitokeza kumbe jamaa alichukua kadi ya gari ya demu bila kumwambia kaenda kuchukulia mkopo yapata mwaka sasa. Na jamaa hali mbaya sasa ameshindwa kumalizia deni, watoa mikopo wamekuja juu wanataka gari tu. Hapo demu ndio amejua kumbe kadi yake ilitumika kukopa huo mkopo nae kaja juu ile mbaya na hamtaki tena huyo jamaa.
katika hali hiyo wa JF mnashauri nini?
katika hali hiyo wa JF mnashauri nini?