Sabung'ori
JF-Expert Member
- Jul 19, 2011
- 2,166
- 1,247
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani
Iringa, Gerald Guninita
amemkamata na kumweka chini
ya ulinzi, Mwenyekiti wa Serikali
ya Kijiji cha Udekwa kilichopo
Tarafa ya Mahenge, Obadiah
Lubugo, kwa kutochangia Sh.
70,000 za Mbio za Mwenge.
Lubugo, ambaye ni Mwenyekiti
wa Serikali ya Kijiji kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), alionja kadhia hiyo
juzi baada ya kuelekeza fedha
hizo katika manunuzi ya chaki
kwenye Shule ya Msingi Udekwa.
Rekodi ya kijiji hicho inaonyesha
kuwa tangu Tanzania ilipopata
uhuru mwaka 1961, Mwenge
huo haujawahi kupita hapo hadi
hivi sasa, tukio ambalo linatoa
tafsiri tofauti na michango halisia
ya wananchi.
Akilalamikia hatua hiyo mbele ya
mkutano wake na waandishi wa
habari, Lubugo alisema
amehuzunishwa na hatua hiyo
ya Mkuu wa Wilaya kumkamata
na kumlazimisha kulipa fedha
hizo wakati Mwenge huo
ulishapita Juni 22, mwaka huu.
Amenikamata na kunilazimisha
kulipa huo mchango wakati
shuleni (Udekwa) kulikuwa
hamna hata chaki na tulipeleka
kwa Mkuu wa Shule Sh. 274,000
na akasaini kwa ajili ya manunuzi
ya chaki na mambo mengine.
Lakini cha ajabu alipofika kijijini
kwetu, DC akasema kama sina
fedha hizo nikae Polisi kuanzia
tarehe 29 mwezi Juni hadi Julai
2, mwaka huu ndipo nipelekwe
ofisini kwake," alilalamika.
Lubugo alisema Sh. 274,000
zilizoelekezwa na serikali ya kijiji
kwenda kwenye manunuzi ya
chaki na masuala mengine ya
kitaaluma, zilipitishwa na
wajumbe wa serikali yake
kutokana na shule hiyo kutopata
mgawo wa fedha serikalini kwa
matumizi hayo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa barua
iliyoandikwa na Halmashauri ya
Wilaya hiyo, yenye kumbukumbu
namba KDC/A4/1/30 ya Aprili 12,
mwaka huu, kwenda kwa
maofisa watendaji wa kata,
ikielekeza maandalizi na
michango ya Mbio za Mwenge
wa Uhuru, inaagiza kila kijiji
kuchangia Sh.70,000.
Sehemu ya barua hiyo inaeleza
hivi: "Mwisho wa kuwasilisha
michango hiyo ni tarehe 10 Mei,
2012 na kila Mtendaji wa Kijiji
anapaswa kupatiwa risiti.
Ningependa mhimize suala la
uchangiaji wa Mbio za Mwenge
kwa vijiji vilivyo kwenye kata
zenu ambapo kila kijiji
kinatakiwa kuchangia
Sh.70,000.
NIPASHE ilipomtafuta Mkuu wa
Wilaya hiyo kwa njia ya simu ya
mkononi pamoja na kumtumia
ujumbe mfupi wa maandishi
(SMS), kwa ajili ya kumtaka
kuthibitisha au kukanusha madai
hayo, lakini hakujibu.
Afisa Habari wa wilaya hiyo
aliyejulikana kwa jina moja la
Christopher, aliwajibu waandishi
wa habari kwamba hawezi
kupokea simu na ameagiza
afuatwe kijiji cha Lundamatwe.
SOURCE: NIPASHE
Iringa, Gerald Guninita
amemkamata na kumweka chini
ya ulinzi, Mwenyekiti wa Serikali
ya Kijiji cha Udekwa kilichopo
Tarafa ya Mahenge, Obadiah
Lubugo, kwa kutochangia Sh.
70,000 za Mbio za Mwenge.
Lubugo, ambaye ni Mwenyekiti
wa Serikali ya Kijiji kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), alionja kadhia hiyo
juzi baada ya kuelekeza fedha
hizo katika manunuzi ya chaki
kwenye Shule ya Msingi Udekwa.
Rekodi ya kijiji hicho inaonyesha
kuwa tangu Tanzania ilipopata
uhuru mwaka 1961, Mwenge
huo haujawahi kupita hapo hadi
hivi sasa, tukio ambalo linatoa
tafsiri tofauti na michango halisia
ya wananchi.
Akilalamikia hatua hiyo mbele ya
mkutano wake na waandishi wa
habari, Lubugo alisema
amehuzunishwa na hatua hiyo
ya Mkuu wa Wilaya kumkamata
na kumlazimisha kulipa fedha
hizo wakati Mwenge huo
ulishapita Juni 22, mwaka huu.
Amenikamata na kunilazimisha
kulipa huo mchango wakati
shuleni (Udekwa) kulikuwa
hamna hata chaki na tulipeleka
kwa Mkuu wa Shule Sh. 274,000
na akasaini kwa ajili ya manunuzi
ya chaki na mambo mengine.
Lakini cha ajabu alipofika kijijini
kwetu, DC akasema kama sina
fedha hizo nikae Polisi kuanzia
tarehe 29 mwezi Juni hadi Julai
2, mwaka huu ndipo nipelekwe
ofisini kwake," alilalamika.
Lubugo alisema Sh. 274,000
zilizoelekezwa na serikali ya kijiji
kwenda kwenye manunuzi ya
chaki na masuala mengine ya
kitaaluma, zilipitishwa na
wajumbe wa serikali yake
kutokana na shule hiyo kutopata
mgawo wa fedha serikalini kwa
matumizi hayo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa barua
iliyoandikwa na Halmashauri ya
Wilaya hiyo, yenye kumbukumbu
namba KDC/A4/1/30 ya Aprili 12,
mwaka huu, kwenda kwa
maofisa watendaji wa kata,
ikielekeza maandalizi na
michango ya Mbio za Mwenge
wa Uhuru, inaagiza kila kijiji
kuchangia Sh.70,000.
Sehemu ya barua hiyo inaeleza
hivi: "Mwisho wa kuwasilisha
michango hiyo ni tarehe 10 Mei,
2012 na kila Mtendaji wa Kijiji
anapaswa kupatiwa risiti.
Ningependa mhimize suala la
uchangiaji wa Mbio za Mwenge
kwa vijiji vilivyo kwenye kata
zenu ambapo kila kijiji
kinatakiwa kuchangia
Sh.70,000.
NIPASHE ilipomtafuta Mkuu wa
Wilaya hiyo kwa njia ya simu ya
mkononi pamoja na kumtumia
ujumbe mfupi wa maandishi
(SMS), kwa ajili ya kumtaka
kuthibitisha au kukanusha madai
hayo, lakini hakujibu.
Afisa Habari wa wilaya hiyo
aliyejulikana kwa jina moja la
Christopher, aliwajibu waandishi
wa habari kwamba hawezi
kupokea simu na ameagiza
afuatwe kijiji cha Lundamatwe.
SOURCE: NIPASHE