Mkeo akifungwa jela utamsubiri au??

Kuna kitu ninakiona na sikielewi kabisa.Mwanaume akifungwa jela, mke anapaswa naye kuwa kifungoni angalau cha nje.Jamii inamtegemea amsubiri mumewe arudi nyumbani hata kama anatumikia kifungo cha miaka 50! Sheria hata hivyo inamruhusu mke kudai talaka kama mume atafungwa kifungo cha muda mrefu.

Lakini mke akiwa na kesi tu..(hapo hajafungwa)...mume ataanza kujitafutia liwazo kwa kisingizio ati mke hayupo nyumbani anahangaika na kesi.Akifungwa ndiyo kabisaaa asahau kumkuta mumewe akimsubiri.

1.Hivi ni kwanini jamani?

2.Kwa wanaume tu...mkeo akifungwa utamsubiri amalize kifungo?

WoS, watu wanavinjari hata wake zao au waume zao hawajafungwa na wanaishi nyumba moja! Sasa kwa wanaume mke akifungwa kwa miaka 10 au zaidi si atakuta jamaa kishajichukulia kimwana kingine jumla jumla? Kwa wanawake anaweza asihamishie mtu ndani ya nyumba lakini akawa na nyumba ndogo yake ya kwenda 'kujiliwaza' kila anapojisikia kufanya hivyo.
 
2.Kwa wanaume tu...mkeo akifungwa utamsubiri amalize kifungo?[/QUOTE]

Wewe mumeo akifungwa utamsubiri mpaka atoke kifungoni?
 
Kuna kitu ninakiona na sikielewi kabisa.Mwanaume akifungwa jela, mke anapaswa naye kuwa kifungoni angalau cha nje.Jamii inamtegemea amsubiri mumewe arudi nyumbani hata kama anatumikia kifungo cha miaka 50! Sheria hata hivyo inamruhusu mke kudai talaka kama mume atafungwa kifungo cha muda mrefu.

Lakini mke akiwa na kesi tu..(hapo hajafungwa)...mume ataanza kujitafutia liwazo kwa kisingizio ati mke hayupo nyumbani anahangaika na kesi.Akifungwa ndiyo kabisaaa asahau kumkuta mumewe akimsubiri.

1.Hivi ni kwanini jamani?

2.Kwa wanaume tu...mkeo akifungwa utamsubiri amalize kifungo?

This is on a person to person basis. Si rahisi kumlaumu mtu kwa kuto kusubiri bila kuangalia hali halisi iwe mwanaume au mwanamke. You shouldn't be expected to wait. You should wait because that's what you want to do from the bottom of your heart. Siyo unamsubiria mtu huko bado una jiridhisha na wengine(this is to both men and women). I would wait for my woman but tuwe wakweli ina tegemea na mazingira yenyewe. One scenario ni kama kuna watoto wana husika. Je kipi ni bora kwa hao watoto?
 
Last edited:
kwangu mimi nitamsubiri,kwa muda wote atakaokaa jela,LAKINI I WILL BE PUMPING OUTSIDE ANYWAYS!i'm very honest na hili jamani.mimi dhambi za uongo sitaki
 
Say umemsubiri kwa kipindi chote cha kifungo chake, akitoka na kukuambia amekuwa vegetarian utafanya nini?
Kurudi kwenye mada hili swala linategemea na maamuzi ya mtu na mtu na mazingira ambayo ndoa yao imo (kabla na wakati wa kifungo), hapa ndipo nadhani swala la open marriage linakuja into play-IMHO.
 
Kuna kitu ninakiona na sikielewi kabisa.Mwanaume akifungwa jela, mke anapaswa naye kuwa kifungoni angalau cha nje.Jamii inamtegemea amsubiri mumewe arudi nyumbani hata kama anatumikia kifungo cha miaka 50! Sheria hata hivyo inamruhusu mke kudai talaka kama mume atafungwa kifungo cha muda mrefu.

Lakini mke akiwa na kesi tu..(hapo hajafungwa)...mume ataanza kujitafutia liwazo kwa kisingizio ati mke hayupo nyumbani anahangaika na kesi.Akifungwa ndiyo kabisaaa asahau kumkuta mumewe akimsubiri.

1.Hivi ni kwanini jamani?

2.Kwa wanaume tu...mkeo akifungwa utamsubiri amalize kifungo?

Swali lipo tricky. Inategemea na mambo mengi. Kwa mfano kama nina lengo la kuwa na watoto katika maisha yangu, halafu ile nimeoa tu kabla hata hatujapata mtoto, mke wangu anafungwa miaka say 25 or more. Kwa hakika siwezi kusubiri. Na hata kama mimi ndio nafungwa katika situation kama hiyo sitategemea/sitademand mke wangu anisubiri.

Kama ni kifungo kifupi na hakitaathiri mipango ya maisha kwa kiasi kikubwa then kusubiri inaweza kuwa a better alternative.

Hata hivyo binaadamu wote ni wadhaifu, wake kwa waume. Yes anaweza aubiri kwa maana ya kutooa au kuolewa lakini bado akawa na affairs nje katika huko kusubiri. Angalau nafahamu kisa kimoja cha mwanamke ambaye mumewe alipofungwa yeye alikuwa na affairs nje na bahati mbaya akazaa. Mumewe alipofunguliwa, wakaendelea na ndoa pamoja na kuwepo kwa mtoto huyo wa nje nadhani mwanaume alimwelewa mkewa na akamsamehe).
 
2.Kwa wanaume tu...mkeo akifungwa utamsubiri amalize kifungo?

Wewe mumeo akifungwa utamsubiri mpaka atoke kifungoni?[/QUOTE]

Inategemea.... kama alikuwa ananijali na kuniheshimu... basi nitamsubiri hadi atoke hata kama ni kifundo cha muda mrefu.Kama kifungo ni kirefu sana zaidi ya miaka 10, na alikuwa mtu mkorofi... kwa kweli itabidi ku process talaka niwe huru ili nikijikuta kwenye situation nisije leta watoto nje ya ndoa.
im just kidding! Kwa kweli sijui nitafanya nini..ndio maana naomba michango yenu.
 
Say umemsubiri kwa kipindi chote cha kifungo chake, akitoka na kukuambia amekuwa vegetarian utafanya nini?
Kurudi kwenye mada hili swala linategemea na maamuzi ya mtu na mtu na mazingira ambayo ndoa yao imo (kabla na wakati wa kifungo), hapa ndipo nadhani swala la open marriage linakuja into play-IMHO.

Hizi ndio ishuz ninazotaka tuziangalie.Utasubiri mtu, atarudi huko kawa kitu tofauti kabisa.Si ni balaa?
 
Wewe mumeo akifungwa utamsubiri mpaka atoke kifungoni?[

Inategemea.... kama alikuwa ananijali na kuniheshimu... basi nitamsubiri hadi atoke hata kama ni kifundo cha muda mrefu.Kama kifungo ni kirefu sana zaidi ya miaka 10, na alikuwa mtu mkorofi... kwa kweli itabidi ku process talaka niwe huru ili nikijikuta kwenye situation nisije leta watoto nje ya ndoa.
im just kidding! Kwa kweli sijui nitafanya nini..ndio maana naomba michango yenu.

Ha ha ha ha ha ha LOL! WoS miaka 10 mingi sana kusubiri njemba iliyofungwa unaweza kuendelea kunanihii ;) lakini bila ya kuongeza familia kama alivyoiacha mtumikia kifungo.
 
usinichekeshe Masa lol!
No, ni philosophical questions tu ambazo mtu humjia akilini hasa baada ya kuona matukio fulani.

Ahhh! jirani tuambiane jirani ha ha ha ha ni aje? Natania tu jirani najua mambo yote ni shwari kabisa ;)
 
Ha ha ha ha ha ha LOL! WoS miaka 10 mingi sana kusubiri njemba iliyofungwa unaweza kuendelea kunanihii ;) lakini bila ya kuongeza familia kama alivyoiacha mtumikia kifungo.

Kumbe hii ishu inajulikana? Kuna jamaa alifungwa kipindi cha uhujumu uchumi.Aliwekwa kizuizini na haikujilikana atatoka lini.Basi huyo bibie/mkewe akajikuta analiwazwa na mtu fulani.Siku moja mume akaachiliwa..akarudi nyumbani akamkuta mkewe ambaye wala wahakuwa wamezaa, yuko vilevile hana hata mtoto na wakaendelea kuishi raha mustarehe.Kama kawaida vidudu mtu hawakukawia.Story zikaletwa na utamu kukolezwa.Ilikuwa patashika!Ina maana huyo mdada alishindwa kusubiri na hapohapo hakujua kama atafute talaka ama la! Na kwa utamaduni wetu waafrika, mwanamke angeenda kudai talaka angeonekana wa ajabu!
 
Kumbe hii ishu inajulikana? Kuna jamaa alifungwa kipindi cha uhujumu uchumi.Aliwekwa kizuizini na haikujilikana atatoka lini.Basi huyo bibie/mkewe akajikuta analiwazwa na mtu fulani.Siku moja mume akaachiliwa..akarudi nyumbani akamkuta mkewe ambaye wala wahakuwa wamezaa, yuko vilevile hana hata mtoto na wakaendelea kuishi raha mustarehe.Kama kawaida vidudu mtu hawakukawia.Story zikaletwa na utamu kukolezwa.Ilikuwa patashika!Ina maana huyo mdada alishindwa kusubiri na hapohapo hakujua kama atafute talaka ama la! Na kwa utamaduni wetu waafrika, mwanamke angeenda kudai talaka angeonekana wa ajabu!

Unaona basi jirani! ukitumia akili za kuzaliwa kama huyo bibie basi unaweza kabisa kuwa na njemba ya kukuondoa ukiwa ;) huku ukiendelea kumsubiri wa ubani ili akirudi anakukuta kama alivyokuacha ha ha ha ha with exception ya dalili za kuongeza miaka kidogo na ukiwa aliokuachia kwa miaka 10 ya kuishi kwa upweke ;)
 
Jirani
Hafungwi mtu... ikitokea jirani hutaacha kujua hahahahah

WoS,

Swali lako ni zuri na miongoni mwa mambo ambayo watu wengi hujiuliza. Pia kuna swali jingine kwa mfani "nikifa leo mke/mume wangu ataishije? Majibu si rahisi kuyapata kwa sababu hujafa na hata ukifa hutarudi kuona kinachoendelea.

Pia kama ulivyosema jibu la swali lako huwezi kulipata sasa (in real time) mpaka hayo mambo yatokee.

Lakini umesahau kuwa watu wengi wanaofungwa ni wanaume kwa hiyo unaweza kupata mifano mingi. Hadi tutakapopata usawa wa jinsia (50%:50% representation) ndio tunaweza kufanya uchambuzi usiolalia upande (balanced/unbiased analysis).

Ila kwangu mimi nitabiliana na hali halisi. Kama mama atakuwa selo kwa miaka 1-10 naweza kumpa heshima yake ya kuendelea kuitwa my wife, wakati huo nikiendelea kucheza salama ili kupunguza maumivu. Ikizidi hapo lazima watoto nao wapate mama wa kuwalea. Kuna kabila moja huko Kanda ya Ziwa kama mume alikufa au kufungwa na kumwacha kigoli basi huyo mama alikuwa anakabidhiwa kwa kijana mwenzake kwenye familia ili mambo yasiharibike. Nadhani walikuwa na busara ingawa kwa sasa haiwezekani tena kwa sababu ya magonjwa na utandawizi!!
 
Back
Top Bottom