Mke wangu hapendi niwasaidie wazazi wangu

lukunij

Member
Jul 4, 2012
36
7
ninaishi katika ndoa sasa mwaka wa tatu nimejaliwa kuwa na mtoto mmoja kinachonishangaza mke wangu amebadilika sana ,kimapato hali yangu si mzuri ukilinganisha na awali ,kila siku kugombana tu ndani ya nyumba na hata heshima imepungua tunajibizana kila kukicha sasa kitu kichonitisha ni pale aliponuna eti kwa sababu nimemsaidia baba yangu pesa na baba aliwahikunisaidia kama laki 5 cku chache zilizopita,sasa na yeye anashida ya pesa nimempa sh laki 6 mkewangu amenuna na kusema ninamsaidia tu baba yangu na wazazi wake siwajali,je munanisaidia vip kiushauri kweli bado ananipenda au?
 
anakupenda sana tu..
tatizo ana roho mbaya...muombee
 
Mweleze hao ni wazazi,mnatakiwa kuwatunza.Ila sasa siyo wa upande mmoja tu.Iwe pande zote
 
ninaishi katika ndoa sasa mwaka wa tatu nimejaliwa kuwa na mtoto mmoja kinachonishangaza mke wangu amebadilika sana ,kimapato hali yangu si mzuri ukilinganisha na awali ,kila siku kugombana tu ndani ya nyumba na hata heshima imepungua tunajibizana kila kukicha sasa kitu kichonitisha ni pale aliponuna eti kwa sababu nimemsaidia baba yangu pesa na baba aliwahikunisaidia kama laki 5 cku chache zilizopita,sasa na yeye anashida ya pesa nimempa sh laki 6 mkewangu amenuna na kusema ninamsaidia tu baba yangu na wazazi wake siwajali,je munanisaidia vip kiushauri kweli bado ananipenda au?

Hapo kwenye bold, Inawezekana hamshirikishani vya kutosha kwenye mahusiano yenu. Maana kama baba yako aliwahi kukusaidia wakati wa shida na yeye akapata shida, logically mkeo asingeweza kununa kwa wewe kumsaidia baba yako unless uwe hukumshirikisha mkeo kuhusu huo msaada.

Ukiwa na familia ni bora kuenenda kwa hekima kwa balance misaada na mawasiliano baina ya hizo koo mbili. Ni vizuri ukae na mkeo na kupanga nini cha kufanya na kuwa na kauli ya pamoja na kufanya mambo kama familia kuliko kila mtu kujifanyia anachojisikia.

Pia usiwe na inferiority complex kuwa mkeo kabadilika kutokana na kipato, inawezekana ni mambo madogo tu ya kukaa chini na kuongea na kuyamaliza. Hebu jaribu kumuita jioni ya leo uongee naye kuhusiana na mambo ya kifamilia na jaribu kumshirikisha kwenye mipango kadhaa na matumizi ya fedha uone reaction yake. Angalizo: Ongea naye kwa hekima!
 
ninaishi katika ndoa sasa mwaka wa tatu nimejaliwa kuwa na mtoto mmoja kinachonishangaza mke wangu amebadilika sana ,kimapato hali yangu si mzuri ukilinganisha na awali ,kila siku kugombana tu ndani ya nyumba na hata heshima imepungua tunajibizana kila kukicha sasa kitu kichonitisha ni pale aliponuna eti kwa sababu nimemsaidia baba yangu pesa na baba aliwahikunisaidia kama laki 5 cku chache zilizopita,sasa na yeye anashida ya pesa nimempa sh laki 6 mkewangu amenuna na kusema ninamsaidia tu baba yangu na wazazi wake siwajali,je munanisaidia vip kiushauri kweli bado ananipenda au?

Angalia hiyo mistari rd. hilo ndo tatizo. wakati unamuoa ulimwonyesha unazo. sasa umefulia unaakuwa na inferiority complex. hata akikuambia ukweli unaona kabadilika.sio yeye tu kilakitu kimebadilika. be a man and face reality.
 
Ana roho mbaya huyo! Na usiache kuwasaidia wazazi wako!

Kama ana kupenda kweli kwa nini ana chukia ukiwasaidia wazazi wako?

Muombe mungu sana abadilike!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom