mamayeyo
Senior Member
- Apr 4, 2012
- 167
- 132
Ebu nishaurini,nina mke ambaye tumeona kama miezi sita hivi imepita..katika hari ya uchumba wetu tulikuwa na mapenzi ya kawaida,si ya moto wala baridi katika kipindi cha miaka minne..
Tulikubaliana tuoane ..lakini katika kipindi chote cha ndoa sijawahi kusikia mke wangu akinitamkia kuwa ananipenda japo tunafanyia mambo mbalimbali kama wanandoa,kila nikimuuliza kwa nini huwa usijawahi ukisema kuwa unanipenda hata siku moja toka tuoane basi huwa ananuna mpaka basi..
Jana nimemwambia siku nikipata mtu anayeniambia ananipenda na kunijari kuliko wewe..utakuja kujuta na huku ukiwa umekwisha chelewa..basi kanununa usiku kucha mpaka naondoka nyumbani..
Nishaulini nichukue hatua gani kwa huyu bibie..
Inaelekea hujiamini kabisa wewe pia hujatulia. Je wewe huwa unamweleza kuwa unampenda au unataka akuambie wewe tu? Hebu mwache mtoto wa watu kama ndivyo alivyo. Kakubali kuwaacha wazazi wake na kuambatana na wewe kwa tabu na raha. Hizo chokochoko zako ndo tabu zenyewe anazovumilia. Angekuwa hakupendi angekubali kuishi na wewe mwenye kero za kudai kutamkiwa kupendwa? Acha hizo.