Mke wangu anajihusisha na mambo ya ushirikina!

mwambie ambane atupatie historia yake ni lini ameanza kufanya mambo hayo, tangu akiwa mtoto au hivi karibuni.

je ameridhishwa mikoba au amejifunzia katika saloon za kike mnakowaruhus wake zenu kushiriki umbea na baiashara ya ngono bila ninyi kujua. saloon kuna mambo waulizeni wanawake watawaeleza
 
mwambie aache utoto,bongo asilimia kubwa ya wanawake na wanaume wanakwenda kwa kalumanzila,akimwacha ataacha wangapi,tell him to learn to live with it ila amatahadharishe asimwekee mazagazaga kwenye chakula.
 
hakuna ki2 sipendi kama kuishi na mshirikina ndan ya nyumba loh, pole sana.
hawa wameshaoana kumwambia ampige mkewe chini mh pagumu sana.
cha msingi huyo bwana atoe msimamo wake kuwa hapendi io tabia tena kama ni wa2 wa dini wangewahusisha na wahusika either misikitin na kanisan na huyo mama ajielee kinagaubaga anfuata nn uko kwa waganga.
kama anadoubts fulan fulan dats y anakwem=nda uko ungemuhakikishia bs awe na aman.
pia muwe mnasali daily b4 u slip, ilo pepo litamtoka 2.
 
Mke wangu,........halafu mke wa rafiki yangu............SASA NI MKE WENU HAPO NDO MNAPOWEKWA SAWA NA JUJU
 
Mke wangu...............rafiki yangu nusura agongwe na magari.....mke wake....SASA HUYO NI MKE WENU NDO MAANA MNAFANYIWA JUJU ILI MUWE WAPOLE
 
Wala usiache Mwanamke Mchawi aishi..................................kwahiyo mhurumie kwa kumuachia uhai wake ila mpige chini (achana naye).............uchawi ni roho hawezi kuacha kwa kusemwa au maonyo, watu wengi wanapenda kuacha uchawi, lakini shughuli namna ya kutoa hizo roho. Kama unampenda na hutaki kumuacha mpeleke kanisani afanyiwe maombi ya kuondoa roho chafu, mikataba, na uchawi na pia aonyeshe vitu vyote alivyowahi kupewa na mganga na sehemu alizowahi kuviweka ili navyo viombewe na kuchomwa moto.........
huu ushauri nao kiboko..kweli kuna umuhimu wa kwenda church ku-refesh yaliyopita.
 
hhahaha wala asiwe na hofu kwani uchawi hausaidii ataloga kama hajui mapenzi ni nini haitamsaidia kwani katika uchawi huo hajathibitisha kama ni wa kumdhuru au wa kulinda ndoa kwa wale waliwao kwa kuamini ulkinzi wa ndoga ni uchawi
 
Kuna watu wanaamini sana ndumba
Jamaa anawezwa pigwa limbwata alete mchungaji akemee pepo hilo.
 
Duniani kuna mambo! Mie ni Dadaake mke wangu, binti wa miaka thelathini na kidogo lakini habari zake si nzuri! Jana kanisimulia mambo ambayo sikupaswa hata kuyasikia na sikuamini kuwa ni mshirikina kiasi hicho! Kwa bahati mbaya sitaweza kueleza story yenyewe kwa sasa ila niliishia kuamini tu kuwa MAOMBI yana nguvu hata kama unasali kwa mazoea tu! maana ali-confess mbele yangu kuwa wamenishindwa!! so hata hili nalo laweza kuwa kweli, ntaanzisha thread nikiwa na computer nielezee kwa mtindo wa "rafiki yangu"
TUNASUBIRI!i
 
Wahenga wanasema ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni....!!!

Rafiki yangu wa karibu sana jana kidogo agongwe na magari baada ya kumfuatilia mke wake kwa umakini zaidi na kugundua kuwa mkewe anahusudu sana na anashiriki katika mambo ya kishirikina. Kwa sababu mke wake huyo anafahamu kuwa mumewe hapendi haya mambo ya kishirikina, basi ilibidi ayafanye kwa tahadhari sana ili kuhakikisha kuwa mume wake hafahamu kinachoendelea.

Mumewe alikuwa anahisi kuwa mkewe anashiriki ktk mambo hayo. Mambo yalikuja kuharibika pale mumewe alipomtegea vitu vya kunasa sauti katika maeneo ya nyumbani na maeneo ambayo mkewe anafanyia kazi zake na kushitushwa na mawasiliano ya kulipana pesa baina yake na mganga wake huyo.
Baada ya mumewe kugundua hivyo na kupata ushahidi wa sauti, mkewe alijitetea kuwa anajilinda mwenyewe na anashughulikia afya yake na kuwa eti hana mpango wa kumdhuru yeye.

Anasema mkewe baada ya kuona ishu imevuja kaomba msamaha na kuahidi kuwa hatafanya tena upuuzi huo. Mume anasema haamini maneno hayo, anadai labda mkewe anasema hivyo ili kujipanga zaidi na kuhakikisha kuwa nyendo zake hazivuji tena.
Sasa jana rafiki yangu huyo kaja povu likiwa linamtoka akisema kesha mzaba mkewe vibao kadhaa na anafikiria kuachana naye. Kaniomba ushauri afanye nini maana keshachanganyikiwa baada ya kugundua kuwa mkewe amekuwa akifanya mambo hayo behind the door!
Kaja kuniomba ushauri na mimi nikaona sio vibaya nikaliweka hapa jamvini ili watu waweze kunisaidia kumshauri rafiki yangu katika kipindi hiki kigumu!

Mwambie na yeye aende kwa mganga...
 
mwambie ambane atupatie historia yake ni lini ameanza kufanya mambo hayo, tangu akiwa mtoto au hivi karibuni.

je ameridhishwa mikoba au amejifunzia katika saloon za kike mnakowaruhus wake zenu kushiriki umbea na baiashara ya ngono bila ninyi kujua. saloon kuna mambo waulizeni wanawake watawaeleza
Mh! Lazima utakua nawe ni Fundi (mtaalam) wa hayo mamboz.
 
unalosema ni kweli kabisa. siwezi kuacha kutumia third part kama ishu inamhusu third part, ingekuwa inanihusu nisingehangaika kuweka third part...hii ni kwa sababu humu jf hatutumii majina halisi kwa hiyo hata kama nikisema ni ishu yangu huwezi kunfahamu/kunitambua.

Lakini heading ya thread yenyewe inaonesha ni mkeo. Kuwa mpole tu rafiki maana hukujipanga vizuri.
 
nafikiri ni makubaliano toka mwanzo hayakuwa clear! Mi na wangu tumekubaliana yeyote akijihusisha na ushirikina it will be the end of us! haya mambo ni mkataba tu ukiwa clear na both sides mkaelewa hakutakuwana lawama! mshirikina mbaya sana asikwambie mtu anaweza kukulisha wafu au hata vitu visivyoliwa hata kinyesi ili mradi afanikiwe anachokitaka! kwangu mie ningepiga chini tu no mjadala
 
Superstitious goat.

With wives like these, who needs marriage?

Kiranga, huyo mke anahitaji sana elimu, na huwezi jua; uwezekano mkubwa amekulia kwenye familia ya kishirikina.
Tukirudi nyuma, wafanyabiashara wakubwa wangapi washirikina, mafisi wangapi wa serikali ni washirikina, wanasiasa wangapi ni washirikina?

Can you say, 'with leaders like ours; who
needs leadership?'
 
ni kweli hata mimi naona anahitaji elimu huyo shemeji yangu. inawezekana hata marafiki zake na baadhi ya majirani ndio waliomuingiza ktk hiyo tabia. alisahau ule msemo wa JK unaosema Akili za kuambiwa changanya na za kwako maarufu kama mbayuwayu!
 
ni kweli hata mimi naona anahitaji elimu huyo shemeji yangu. inawezekana hata marafiki zake na baadhi ya majirani ndio waliomuingiza ktk hiyo tabia. alisahau ule msemo wa JK unaosema Akili za kuambiwa changanya na za kwako maarufu kama mbayuwayu!
Kiranga, huyo mke anahitaji sana elimu, na huwezi jua; uwezekano mkubwa amekulia kwenye familia ya kishirikina.
Tukirudi nyuma, wafanyabiashara wakubwa wangapi washirikina, mafisi wangapi wa serikali ni washirikina, wanasiasa wangapi ni washirikina?

Can you say, 'with leaders like ours; who
needs leadership?'
 
chunguza kwanza alafu ukishatambua ukweli tafuta muda uongee naye na ujue ni kwa nini anafanya mambo kama hayo,kama tatizo liko kwako basi mzidishie kilichopungua ili asikutendee ushirikina kama suluhisho ya shida yake kwako
 
Kwa nini mnapenda kutumia neno rafiki yangu, badala ya ninyi wenyewe? hao rafiki zenu ni kwa nini msiwashauri wawe member wa JF? nahisi udanganyifu mtupu kuwatumia third part kwa karibu kila thread.


Hata mimi siyapendagi haya mambo ya rafiki yangu, rafiki yangu!!... ona hapo chini

"Nashukuru sana maana umeongea kitu cha msingi mno!....inavyoonekana mkewe huenda kwenye hayo mambo kwa ajili ya afya yake...actually it is a wastage of money and uaminifu kwa mumewe..."

Read between the lines.
 
Back
Top Bottom