Mke wa pili ...!A curse or blessing?

Pole sana dada. Na mara nyingi wanaopata laana za kuvunjika ndoa ni wanaume kwa sababu wao kama kichwa ndio chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika. In most cases women move on na maisha yanakuwa pouwa kuliko hapo awali. Mungu anawaadhibu hawa kaka zetu kwa tamaa zao za dogo dogo na kukubali kusambaratisha familia zao.

Kwa wanawake wengi waliotoka kwenye ndoa naona mambo yao si mabaya.



Yaani kaka ram unayosema ya dada yako yamewafika wengi mmoja wapo ni mimi hapa ninayeandika hapa. Yaani kuachana na mume /mke wa kwanza mara nyingi ni laana maana Mungu mwenyewe alisema kwenye BIBILIA nachukiia kuachana kwenu. Mimi niliolewa kwa ndoa ya Kanisani tumekaa kwa amani miaka 3 ule wa nne maneno yalianza tokea kwa ndugu wa mwanaume "hazai , hazai" nasikia alikuwa malaya. Mimi nikasikitika sana kwamba maisha yangu nilitulia na kufundishwa na wazazi kwamba nikiguswa guswa na wanaume nitpata ujauzito. Kwahiyo nikasoma nikamaliza bila kuguswa mpaka nikaolewa. Laajabu miaka 4 imepita hakuna mtoto, na mwenzangu kwa vile makabila ni tofauti akaanza kuletewa maneno ya uongo akayasikiliza mpaka mwaka wa 5 tukatengana hakuna chakula hakuna matumizi ni mimi kila kitu mpaka nikaanza kupigwa bila sababu basdaye nikajiondoa baada ya kipigo kikubwa cha mwisho. Kwa ufupi mwenzangu alikuwa na msichana mkerewe walikuwa naye siku tele zilizopita. Basi wakakaa sana wanafanikiwa tu mimi maisha yangu yalikuwa kawaida tu. Mpaka siku moja nikaamua kufungua case mahakani baada ya kugundua kwamba waliisha funga ndoa Bomani. Case ikanguruma akaulizwa umefungaje ndoa na huku una ndoa nyingine?. Akafanya mipango case ikahamishiwa ADR Kisutu yaani mimi through wakili wangu alihongwa hela akasaini case iende kuvunjwa.....
Case ikavunjwa bila hata kusikilizwa neno lolote nikalia mahakamani wenzangu walikuja wamekamatana kama kumbi kumbi mahakamani wananicheka. Basi nikaambiwa halali yako mama ni laki 5, mwenzako atapata wapi hela za kukupa?. Nikasema mimi sichukuwi hizo hela nikatoka mahakamani nikaacha hata kufuatilia tena talaka na wakili wangu alisaini kila kitu kwa niaba yangu.
Baada ya miaka 3, aliyekuwa mume wangu na mkewe wote waliachishwa kazi wakahama hapa mjini wakenda nje ya Dar karibu ma Moro huko wanalima na kuleta mazao kwa biashara hapa mjini. Mnamo mwaka 2004, aliyekuwa mume wangu alituma rafikye akiniomba nimsamehe maana kila anachofanya hakifanikiwi.......
Ndoa ni moja ila kuna zingine unashidwa inabidi uvunje ila ukivunja ndoa hakikisha huna makosa la sivyo utakiona cha mtemakuni.....
 
Kuwa na vimada ni quit different na kuoa. Tena wenye vimada wengi ni wanaume ambao wanajua limits. Hao vimada hawana nafasi ya kuingilia mipangilio ya familia hasa masuala ya kiuchumu. Hata kama unakuta anajengea nyumba au kununulia gari kimada, wengi unakuta ni kuwa anazo pesa za kutosha hiyo ni change. Kuoa maanake umepata mshauri mpya katika maisha yako; kama ni mwanamke wa anasa; na mara nyingi huwa hivyo jua umepotea. Maana I can imagine type of a woman ambaye ana dare kumtoa mwenzie kwenye ndoa kwa kujiona yeye ni bora zaidi. In most cases ni wale wadada wa aina fulani.


Narudia tena sio kwamba na Support but tuangalie logic;

Swali....
  • Wangapi pia wameoa wana Mke mmoja na bado maisha ni mabaya or just Sustainable??
  • Wangapi wameoa wana Mke mmoja but ana vimada kumi kidogo?? What's the difference??
 
Baba Enock leo umewaza nini. Unajua nimechangia bila kuangalia nani kaleta huu uzi ulopiga shule. Is that you real? I remember your comments on supporting things that made me think of you as a last person to respect marriage.

Big up!
 
Mimi nina kaka yangu alioa mke ambaye mama yake (My aunt) na nduguze waliona kuwa jamaa kaingia mkenge. Wameishi for almost 20 years (kama niko sahihi) ndio bro kaanza kuona wife hafai. Na bro mwenyewe ni mfanyabiahsara maarufu na pesa zipo za kutosha. Kaamua kuachana na mkewe. Marafiki zake wanasema it was a right decision. But nikimuangalia alivyobadilika nasema mara elfu angebaki na huyo mkewe mcharuko. Maana amekuwa kama chizi. Ameshakaa na mwanamke mwingine for less than two year wametengana. Yaani ni nuksi hata kama situation forced him to make such a decision. Kwa sasa naweza kumuita bachelor maana naona amekata tamaa ya kuoa tena. Sasa nambie bachelor wa uzeeni. Na bado hajafulia lakini anapata tabu kupata right candidate.

Watoto wake sasa wanamchukia hamna maelezo. It is always like that when marriages ends it's the father to blame. Watoto walikuwa vipenzi wa baba yao lakini sasa hivi wananambia NK ni bora niombe ela kwa mtu mwingine si kwa baba imagine chuki gani hiyo kati ya mtoto na babake.
 
Back
Top Bottom