mimi sijali kuhus mke wa mbowe (lilian mtei). Hata akiamua kuhama na nchi ili pia asionekane sioni tatizo.
tatizo ninaloliona ni la kwa nini mbowe hajitokezi kujibu mengi yanayoisulubu chadema??
inakuwaje watumishi na wanachama maarufu/muhimu (kafulila & danda juju) wanahama chama lakini mwenyekiti hajitokezi kutoa angalau tamko au kujibu maswali ya waandishi wa habari?
mbowe kama anaogopa waandishi leo hii kwa mambo madogo madogo kiasi hiki, je anategemea kumuongoza nani?
hawa wandugu kafulila na danda wanatumiwa na kundi fulani kuichafua chadema pengine washapewa vijisenti maana wanasiasa wetu wana njaa balaa hawajali misingi ya siasa maana hata ndg zitto ilinishangaza kuhusu kuunga mkono kutumia uozo wa mitambo ya dowans wakati dr.mwakiembe alishaonya kutoitumia au wanataka umaarafu wa kisiasa kama zitto, hata wakiondoka chadema itabaki na nguvu, hata zitto akiondoka chadema itabaki na nguvu.
Mwenyekiti mbowe na mzee ndesamburo wameifadhili chadema kwa kipindi chote kwaio lazima wawe na usemi mkubwa au tuite ushawishi mkubwa kwenye chama.
Hata japan na germany zinaongoza kutoa michango y ela nyingi katika un kama vile uk , usa na france wanavyofanya na ndio maana zinalilia nafasi ya kudumu kwenye baraza la usalama la un.
Hata kwenye kampuni wenye hisa kubwa wana usemi mkubwa kuliko wenye hisa ndogo.
Kwaio mwenye nguvu mpishe afanye mambo yake