lara 1
JF-Expert Member
- Jun 10, 2012
- 15,700
- 29,111
Watu mnaogopa uzee. Lol.
Utakuja tu hata mfanyeje.
Ndio maana ni vyema kujipenda si kungojea kupendwa...mtajikuta depressed mkiona makunyanzi kisa...jamaa ataniona nimechakaa.
Mi suala la kuzeeka wala halinisumbuhi...kinachonisumbua akili ni ntakuwa mzee wa aina gani...nataka niwe mama/bibi mwenye heshima na si kusifiwa uzuri tu. I want my sons to be proud of my achievements as a person sidhani kama kwao ita matter kama mama ana maziwa artificial yalosimama.
Mimi kuna wamama nawatamani kweli na wameshastahafu na mvi zao kichwani...kwangu nawaona wako sexy si kwa mvuto kwa sababu kuna walichotuachia sisi tulo nyuma yao.
Hahahaaa! Wazo zuri sana, ila wengine shule tumeenda mpaka elimu ya juu bt no kuelimika!!! LOL! Tumezoea shortcut tu, ujasiriamali ushatushinda tumebaki TUNAJASIRIAMWILI tu!!! Kazi ipo. Fainali uzeeni!