Mke na Mama

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
180
Wadau mama anaumwa na anataka kukaa na mimi,mke wangu anasema hana furaha kukaa na mama nyumba moja,nimechanganyikiwa nishaurini,nimuondoe mamam au nikae nae na mke wangu hatakuwa na furaha???

Nisaidieni wajameni.
 
Bora umueleze mkeo atumie hekma ivi ingekua mama yake mzazi asinge mpokea hapo nyumbani? ukiwa kama mwanamme nilazima Mkeo amheshimu na kumdhamini mzazi wako kama wake.
 
Mkuu kuna vitu hapo hujaeleza, haiwezi from nowhere mtu akatae kukaa na mama yako..by the way huyo mke nae bado primitive sana au shule ndogo(I mean life school sio ya darasani), is simple logic kuishi na mtu, moja kuepuka kitu ambacho hapendi wewe ukifanye pili kuepuka vitu vinavyowakwaruzisha, tatu epuka kuwa nae karibu na kujibizana nae hiyo itasaidia sana...wewe pia mme msaidie mke katika hayo matatu na ataishi na mama mkwe wake fresh kabisa.
 
mkuu hebu ongea vizuri na mkeo kwani sidhani kama ni rahisi agome bila sababu...jitahidi kumfanya akuambie na umuamini...inawezekana nawewe unamsikiliza sana mama yako kuliko mkeo.
 
Wadau mama anaumwa na anataka kukaa na mimi,mke wangu anasema hana furaha kukaa na mama nyumba moja,nimechanganyikiwa nishaurini,nimuondoe mamam au nikae nae na mke wangu hatakuwa na furaha???

Nisaidieni wajameni.

Hapo kwenye red tufafanulie vizuri, mama yako anaumwa na anataka kukaa na wewe au anataka kuja kuugulia kwako? na huyo mkeo sijaelewa hasikii furaha kumuuguza mama yako au? kuna kitu hujaweka wazi ebu fafanua vizuri ili usaidiwe
 
Jaribu kumuuliza mkeo sababu ya msingi ya kutokutaka kuishi na mama yako,pia muulize mama yako sababu ya kutaka kuja kuishi kwako,inatakiwa ujue kuwa kila mmoja ana thamani yake,thamani ya mama haiwezi kuwa ya mkeo wala thamani ya mkeo haiwezi kuwa ya mama yako,lakini pia mama yako anatakiwa atambue kuwa umeoa na unahitaji kuishi na mkeo unless kwa muda au anakuja hapo kwaajili ya matibabu au hana pa kuishi,lakini inaonekana pa kuishi kupo ndo maana anataka kutoka huko aliko ili aje kwako,lakini pia hata kama hana pa kukaa mtafutie pa kukaa,kwani kukaa na wazazi inatakiwa hekima sana,pia kama umeoa ni wakati wa kukaa na mkeo na watoto sio wazazi,kama unataka amani take my advise,mweleweshe mama yako,kama matibabu yako mbali na aliko kaa nae akimaliza matibabu aende nyumbani!
 
Labda mnaishi nyumba ya kupanga, hasahasa zile za chumba kimoja, so kwa harakaharaka mkeo anaweza kudhani kuwa mama akija wewe utatakiwa kuhama nyumba coz yeye atakuwa analala nae, kifupi atakuwa anakosa raha ya ndoa. Fafanua vrz ili tukushauri. Maelezo yako bado yako hewani!
 
Mama yako anaumwa halafu unauliza watu wakushauri namna ya kumplz mkeo eti akubali ukae na mama yako ili apate matunzo na matibabu sahihi,...mimi naona haya mabo ya kutaka kuiga kila mambo ni ujinga_mama yako ana nafasi kubwa kuliko pengine hata ya mkeo ukweli ndio huo ingawa unaudhi,...

Acha kupoteza muda ku-uliza watu wakati mama yako anaumwa fanya fasta muite aje umpeleke hospital na umwambie huyo mkeo ambaye anaonekana ni jeuri asiye na huruma hata kwa mama yako ambaye anaumwa aachane na msimamo huo,...mama akipona ndio usuluhishe hizo tofauti kama zipo............
 
Wadau mama anaumwa na anataka kukaa na mimi,mke wangu anasema hana furaha kukaa na mama nyumba moja,nimechanganyikiwa nishaurini,nimuondoe mamam au nikae nae na mke wangu hatakuwa na furaha???

Nisaidieni wajameni.

pole sana.

umesema mama anaumwa...anataka akae nawe umuuguze.
Je, utamuuguza kwa muda gani?...
Je, huna dada/kaka wengine anapoweza kufikia?

Sisemi mkeo ana haki ya kukataa....lakini ni wewe pekee unayejua kwanini mmefikia hapo.
Je, naye atapouguliwa na mzazi/ndugu yake...atakuelewa ukikataa kuugulia hapo kwako?

Naomba utafakari hayo kwanza,....huu ni mtihani mzito. Usipoangalia utajikuta
'umempoteza' mama au 'umempoteza' mke, ingawa nakushauri fanya lile utalopata radhi za mzee wako.
Mama ni mmoja... hutapata kama yeye. Mke ni mama wa wanao...
 
Mama yako anaumwa halafu unauliza watu wakushauri namna ya kumplz mkeo eti akubali ukae na mama yako ili apate matunzo na matibabu sahihi,...mimi naona haya mabo ya kutaka kuiga kila mambo ni ujinga_mama yako ana nafasi kubwa kuliko pengine hata ya mkeo ukweli ndio huo ingawa unaudhi,...

Acha kupoteza muda ku-uliza watu wakati mama yako anaumwa fanya fasta muite aje umpeleke hospital na umwambie huyo mkeo ambaye anaonekana ni jeuri asiye na huruma hata kwa mama yako ambaye anaumwa aachane na msimamo huo,...mama akipona ndio usuluhishe hizo tofauti kama zipo............

Igwe usikurupuke namna hiyo kaka. Ukijibiwa hiyo nyumba ni ya mke, utasemaje?
Busara zinahitajika zaidi kwenye hili kuliko povu. Kila nyumba inahitaji busara zake.
Kuombana ushauri ndio desturi za waungwana.
 
Yote kwa yote kama mke wangu hwezi kumvumilia mama yangu mzazi hata wakati wa ugonjwa hanifai na ipo siku nikiugua pia atafanya hayo hayo.
 
mwambie mkeo aache ubinafsi na uchoyo angekua mama yake je? Na kwenye hilo hauhitaji ruhusa
 

Igwe usikurupuke namna hiyo kaka. Ukijibiwa hiyo nyumba ni ya mke, utasemaje?
Busara zinahitajika zaidi kwenye hili kuliko povu. Kila nyumba inahitaji busara zake.
Kuombana ushauri ndio desturi za waungwana.

Ni sawa mkuu,
Ila kwa mtazamo wangu kuna baadhi ya mambo ambayo nafikiri hayahitaji busara kuya-solve(inabidi kutumia nguvu)...mama anaumwa halafu mke wangu eti hataki nije nikae nae ili nimuuguze,...ooooooooooh no kaka,.....anayway watu tumetofautiana na kila mtu ana dunia yake kwenye hili kiongozi wangu.....mama kwa bahati mbaya akifa eti tunaongozana na mke wangu kwenda msibani..

Kwenye iman yangu ya dini kuna verse'baba ni kichwa cha nyumba'....na kama kichwa cha nyumba ni lazima ufanye maamuzi magumu ambayo pengine yatakera upande wa pili lakn yenye heri na baraka kwa familia
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Duh, aisee kweli kuwa uyaone. Kwahiyo watu wakikushauri msikilize mkeo achana na mama yako mzazi utatekeleza ?

Inaonyesha behind the scene una mambo mengi sana, sitegemei katika hali ya kawaida kwa mtu wa kawaida na katika mazingira ya kawaida mama yako mzazi anaumwa eti unakuja kuuliza watu wakushauri kuwa ufanye nini ?

Nikuulize swali moja, una mtoto kwa huyo mkeo ?

Otherwise ukisikia una mke kimeo balaa ndiyo huyo uliyenaye.
 
Duh, aisee kweli kuwa uyaone. Kwahiyo watu wakikushauri msikilize mkeo achana na mama yako mzazi utatekeleza ?

Inaonyesha behind the scene una mambo mengi sana, sitegemei katika hali ya kawaida kwa mtu wa kawaida na katika mazingira ya kawaida mama yako mzazi anaumwa eti unakuja kuuliza watu wakushauri kuwa ufanye nini ?

Nikuulize swali moja, una mtoto kwa huyo mkeo ?

Otherwise ukisikia una mke kimeo balaa ndiyo huyo uliyenaye.

Kweli kaka_lazima huyu jamaa ajisaili upya namna ya mahusiano na mke wake....la sivyo kuna siku atamwambia muue huyo mama yako kwani ananikera.
 
Ni sawa mkuu,
Ila kwa mtazamo wangu kuna baadhi ya mambo ambayo nafikiri hayahitaji busara kuya-solve(inabidi kutumia nguvu)...mama anaumwa halafu mke wangu eti hataki nije nikae nae ili nimuuguze,...ooooooooooh no kaka,.....anayway watu tumetofautiana na kila mtu ana dunia yake kwenye hili kiongozi wangu.....mama kwa bahati mbaya akifa eti tunaongozana na mke wangu kwenda msibani..

Kwenye iman yangu ya dini kuna verse'baba ni kichwa cha nyumba'....na kama kichwa cha nyumba ni lazima ufanye maamuzi magumu ambayo pengine yatakera upande wa pili lakn yenye heri na baraka kwa familia

LOL,...nimekuelewa wapi unasimamia,...ila tatizo hapa si unaona lilivyo 'uchi wa mnyama?'
Huyu bwana amepungukiwa busara za kumshawishi mkewe waje kumuuguza mama hapo kwao.

Sasa ukimwambia atumie maguvu tu, nani atampikia huyo bi mkubwa, nani atamkogesha,
nani atakuwa akimvisha?...maana hatujajua huyo bi mkubwa anajiweza au la...

Binafsi wala sitopenda mama yangu aje kwangu kisha adhalilike na manyanyaso na masimango nikiwa sipo nyumbani.

 
imeandikwa kwenye Biblia umpende na kumheshimu mzazi wako siku zako ziwe nyingi katika nchiupewayo na bwana Mungu wako
 
Mama ni muhim kuliko mke kwani mke unaweza kupata mwengine lkn mama hupati.namke mwema mwema ni yule anayekupendea wazazi wk kama anavyowapenda wa kwake
 

LOL,...nimekuelewa wapi unasimamia,...ila tatizo hapa si unaona lilivyo 'uchi wa mnyama?'
Huyu bwana amepungukiwa busara za kumshawishi mkewe waje kumuuguza mama hapo kwao.

Sasa ukimwambia atumie maguvu tu, nani atampikia huyo bi mkubwa, nani atamkogesha,
nani atakuwa akimvisha?...maana hatujajua huyo bi mkubwa anajiweza au la...

Binafsi wala sitopenda mama yangu aje kwangu kisha adhalilike na manyanyaso na masimango nikiwa sipo nyumbani.


Ni sawa kiongozi wangu,...
Ila hapa issue ni kwamba mama anaumwa na suala la matibabu ni lazima ili apone,...masuala ya kusema nani atam_care hayawezi kushindikana unaweza kumuagiza sister,dogo,au hata ukatafuta msichana yeyote wa kunfanyia hivyo halafu ukamlipa..by the way hatujaambiwa kazidiwa...

Na kwa taarifa yako mwanamke wa aina hiyo hata kama utamplz halafu akalidhia mama yako akaja katu hawezi kumjali inabidi tu utafute altenative ya kum-care mama yako.......nazidi kusisitiza tu kwamba akili na nguvu ya ziada inahitajika haraka ili mama apate unafuu..otherwise sidhan kama ni busara tena kuendelea kumuomba huyo mkeo eti mama yako aje kutibiwa_lazimisha kiongozi kama vip atajisikia vibaya let her go
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom