Mke Msomi + Mume Msomi = Ndoa nzuri yenye mafanikio?

Tulikuwa tunapiga soga wakati wa kuukaribisha mwaka mpya; moja ya hoja iliyotolewa ilikuwa ni suala la mmoja wetu ambaye alisema kuwa "lazima mke wangu awe msomi bwana, mimi mambo ya kuoa wa darasa la saba simo". Huo ukawa mwanzo wa mjadala mzito wa umuhimu wa usomi (wa elimu ya juu hasa yenye shahada) katika ndoa. Wengine walikuwa wanadai kama wote hamjasoma hamuwezi kuendesha mijadala ya kisomi; na kuwa ndoa haiwezi kudumu au kuwa ya furaha kwani mume anaweza kuwa na dharau fulani hivi kwa mke wake.

Wengine wakasema mwanamke akiwa msomi sana kuliko mwanamme, mwanamme atajiona duni sana na italeta shida kwenye ndoa. Na mmoja akadai wote wakiwa wasomi sana uhusiano wao unaweza kuwa mzuri sana au unaweza kuwa na matatizo kwani itakuwa vigumu sana kumaliza mijadala itakuwa inabakia kuahirishwa na wote wawili wanakuwa very independent minded.

Hadi kengele ya saa sita za usiku inagonga tulikuwa hatujapata jibu muafaka maana tuliona mahali fulani mtu anatangaza anatafuta mchumba na kigezo cha kwanza kabisa kilikuwa "awe na elimu ya chuo kikuu". Mtu mmoja akasema "we unafikiri kwanini baadhi ya wanawake wenye madaraka sana na wasomi wanajikuta hawana waume wa kudumu"?

Hivyo swali linabakia.

MKJJ;

Katika chaguo lolote uwezo wa kifedha hasa kwa mwanaume una nafasi kubwa pia katika kuiweka ndoa sawa. Ikiwa si hivyo basi ndo unakuta "wanawake wenye madaraka sana na wasomi wanajikuta hawana waume wa kudumu". Ingawa hii pia si kwa wote hasa wale wenye mapenzi ya kweli.
 
Ole wenu mwanmke aliyesoma hata akawa na Masters, & mumeo Dr, most of time hakuna NDOA hapo, go & search, wanawake wengiiiiiii
wakiwa na high level ya Education say from ka degree, most of them kwenye ndoa are trouble makers, why...!!!? wanachanganya U Beijing (
women rights, gender equality hadi home) & NATURE
that means waliosoma haki degree & above most wanataka KUWA KICHWA NDANI YA NYUMBA, in short mwanmke anataka kuwa dume home, since when..? hamna ndoa hapo, go & do reseach ndogo

:redfaces::redfaces:
 
lakini % kubwa inabakia kuwa mapenzi hayachagui labda kama mpo after kitu fulani

Ndoa ni kitu kinachojengwa na mapenzi ya dhati kutoka moyoni. Kama ndoa itasimama kwakuangalia idadi ya vitabu au degree ukutani, hiyo si ndoa ya kweli bila kujali nani ni zaidi ya mwingine.
Lakini pia tujiulize, tunaposema msomi je ni kiwango gani cha elimu kianchoshabihiana na neno hilo.
 
Kwanza lazima tukubali kwamba mfumo dume hauwezi kufutika katika uso wa dunia, at least kwa upande wetu huu wa dunia..

kwa mantiki hiyo, wanawake wasomi hawawezi kuishi na wanaume kwa amani, maisha yatakuwa ya taabu sana. Wanawake wasomi are trouble makers, kama alivyoeleza Mr. President hapo juu, Gender Rights, Sleeping Rights, Drinking Rights, Walking Rights, we acha tu...

Kuta 4 za nyumba zinaficha mambo mengi....
 
Kama couple ni 'a match' usomi wao unasadia kuimarisha uhusiano wao....
Kama wawili hawafanani kimtizamo, basi mwanaume msomi/mwanamke asiye msomi au wote sio wasomi inakufanya uhusiano uwepo na udumu...
 
Kwanza lazima tukubali kwamba mfumo dume hauwezi kufutika katika uso wa dunia, at least kwa upande wetu huu wa dunia..

kwa mantiki hiyo, wanawake wasomi hawawezi kuishi na wanaume kwa amani, maisha yatakuwa ya taabu sana. Wanawake wasomi are trouble makers, kama alivyoeleza Mr. President hapo juu, Gender Rights, Sleeping Rights, Drinking Rights, Walking Rights, we acha tu...

Kuta 4 za nyumba zinaficha mambo mengi....

Samahani askofu wewe ni mwanaume/mwanamke msomi?
 
Kwa Ndoa za siku hizi lazima mmoja akubali kuwa chini mwingine juu hapo Ndoa itadumu.

Mkigangamaa wote hapo hakuna kitu kila siku kwenye usuluhishi
 
Kwa Ndoa za siku hizi lazima mmoja akubali kuwa chini mwingine juu hapo Ndoa itadumu.

Mkigangamaa wote hapo hakuna kitu kila siku kwenye usuluhishi

Mpwa mbona unakorofisha? Hapo kwenye bold hebu kapa-edit pasomeke mwanamke. Tafazali tafazali.
 
Kwa Ndoa za siku hizi lazima mmoja akubali kuwa chini mwingine juu hapo Ndoa itadumu.

Mkigangamaa wote hapo hakuna kitu kila siku kwenye usuluhishi

Ndoa ni ngumu sana kuweza kutoka na generalization pana. Ukweli ni namna logistics zenu pamoja na foundation mliyoweka. Wengi wanaoa just because wamefikia umri wa kuoa au kuolewa for many a partner is just a partner.
Kurudi kwenye mada na hasa mabadiliko yanayoendelea duniani traditional marriage (mume zaidi ya mke) inaonekana kupotea kabisa. Ila unapokuwa na pairing ya wasomi and everything being CONSTANT mambo yanaenda vizuri.
Gone are the days ya wanaume kuwa initiators wa mambo mengi katika ndoa.
Katika ndoa hata kama mke akawa msomi kuliko mume, kama ideology ya mume ni kwamba yeye ni zaidi na ni lazima ajue kuliko mke lazima itabaki kuwa tatizo na itakuwa tatizo kubwa sana. Society yetu haijaenda sawa na mabadiliko ya dunia kwa ujumla ila things are changing.
Tukubali kila aina ya pairing ina matatizo ila namna ya kuweza kuyashinda ni muhimu sna katika uhai wa ndoa hiyo. Mengine yanavumilika mengine hayavumiliki. Wakati mwingine mwanamke si msomi ila hapendi kunyanyasika, yaani ana sauti na anaondoka. Pointi ya usomi hapo haifanyi kazi.
 
Kwanza lazima tukubali kwamba mfumo dume hauwezi kufutika katika uso wa dunia, at least kwa upande wetu huu wa dunia..

kwa mantiki hiyo, wanawake wasomi hawawezi kuishi na wanaume kwa amani, maisha yatakuwa ya taabu sana. Wanawake wasomi are trouble makers, kama alivyoeleza Mr. President hapo juu, Gender Rights, Sleeping Rights, Drinking Rights, Walking Rights, we acha tu...

Kuta 4 za nyumba zinaficha mambo mengi....

Umenena vema Askofu,,,mara nyingi mwanamke akiwa juu kuliko mwanaume mambo mengi yanajitokeza,kiburi,dharau,jeuri,,n.k no respect
 
Mpwa mbona unakorofisha? Hapo kwenye bold hebu kapa-edit pasomeke mwanamke. Tafazali tafazali.

Hahahaha yeah mwanamke mmoja akubali kujishusha na asijikweze haya mapenzi ya Izidingo ze nid haya yanaharibu kabisa ndoa nyingi
 
Umenena vema Askofu,,,mara nyingi mwanamke akiwa juu kuliko mwanaume mambo mengi yanajitokeza,kiburi,dharau,jeuri,,n.k no respect

Safi sana hili tumeliona sana hata fweza nazo zinachangia kwa kiasi kikubwa mwanamke akiwa na kipato kikubwa dah hashikiki nyumbani
 
Umenena vema Askofu,,,mara nyingi mwanamke akiwa juu kuliko mwanaume mambo mengi yanajitokeza,kiburi,dharau,jeuri,,n.k no respect

Hahahaha! Nimesoma kwa mawani yangu. Mwanamke akiwa juu hiyo style hata Mungu hapendi bana. Mungu napenda mwanamke kuwa chini mwanaume nakuwa juu yake. Sasa nyie vijana wa siku hizi mnataka mpaka mmwanamke achunge mbuzi mpaka mnatumia mbuzi kagoma style, sijui ndo nini hicho.

Babu anarudi kulala.
 
Mifano ipo hata Marekani wanawake waliosoma ni likely to become feminist ama Lesbian. Asilimia kubwa (sio wote ) wako insane na mfumo dume kwao kila kitu ni mfumo dume. Hata mkiwa katika majadiliano ya kawaida tu ya majukumu ya kifamilia utaona tu mjadala unaanza kuhamia huko. Kwa nini Condolezza Rice hana bwana? Wanawake wasomi ni tatizo (sio wote) asilimia kubwa ni opportunists.
 
Hahahaha! Nimesoma kwa mawani yangu. Mwanamke akiwa juu hiyo style hata Mungu hapendi bana. Mungu napenda mwanamke kuwa chini mwanaume nakuwa juu yake. Sasa nyie vijana wa siku hizi mnataka mpaka mmwanamke achunge mbuzi mpaka mnatumia mbuzi kagoma style, sijui ndo nini hicho.

Babu anarudi kulala.


hahahaha!habari ndo hiyo,,narejea maandiko,,mwanaume anapaswa kuwa kichwa

na mimi narudi kitandani,,lol
 
Back
Top Bottom