Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Tulikuwa tunapiga soga wakati wa kuukaribisha mwaka mpya; moja ya hoja iliyotolewa ilikuwa ni suala la mmoja wetu ambaye alisema kuwa "lazima mke wangu awe msomi bwana, mimi mambo ya kuoa wa darasa la saba simo". Huo ukawa mwanzo wa mjadala mzito wa umuhimu wa usomi (wa elimu ya juu hasa yenye shahada) katika ndoa. Wengine walikuwa wanadai kama wote hamjasoma hamuwezi kuendesha mijadala ya kisomi; na kuwa ndoa haiwezi kudumu au kuwa ya furaha kwani mume anaweza kuwa na dharau fulani hivi kwa mke wake.
Wengine wakasema mwanamke akiwa msomi sana kuliko mwanamme, mwanamme atajiona duni sana na italeta shida kwenye ndoa. Na mmoja akadai wote wakiwa wasomi sana uhusiano wao unaweza kuwa mzuri sana au unaweza kuwa na matatizo kwani itakuwa vigumu sana kumaliza mijadala itakuwa inabakia kuahirishwa na wote wawili wanakuwa very independent minded.
Hadi kengele ya saa sita za usiku inagonga tulikuwa hatujapata jibu muafaka maana tuliona mahali fulani mtu anatangaza anatafuta mchumba na kigezo cha kwanza kabisa kilikuwa "awe na elimu ya chuo kikuu". Mtu mmoja akasema "we unafikiri kwanini baadhi ya wanawake wenye madaraka sana na wasomi wanajikuta hawana waume wa kudumu"?
Hivyo swali linabakia.
Wengine wakasema mwanamke akiwa msomi sana kuliko mwanamme, mwanamme atajiona duni sana na italeta shida kwenye ndoa. Na mmoja akadai wote wakiwa wasomi sana uhusiano wao unaweza kuwa mzuri sana au unaweza kuwa na matatizo kwani itakuwa vigumu sana kumaliza mijadala itakuwa inabakia kuahirishwa na wote wawili wanakuwa very independent minded.
Hadi kengele ya saa sita za usiku inagonga tulikuwa hatujapata jibu muafaka maana tuliona mahali fulani mtu anatangaza anatafuta mchumba na kigezo cha kwanza kabisa kilikuwa "awe na elimu ya chuo kikuu". Mtu mmoja akasema "we unafikiri kwanini baadhi ya wanawake wenye madaraka sana na wasomi wanajikuta hawana waume wa kudumu"?
Hivyo swali linabakia.