kwa mie ambaye tumeishi na ndugu toka utotoni, najua challange zao, ndugu wa mume na wa mke hawapaswi kuishi nao. Tuma msaada huko aliko. Ikishindikana ikabidi kuishi nae ajue sheria, kanuni na taratibu za nyujba yenu....na ajue akizivunja atarudi kwao.
Nikirudi kwenye mada yako, baadhi ya ndugu wa mume kuishi nao ni kazi sana, unakuta kwa sababu tu nyumba ni ya kaka yake wanafikiri wamemuoa na huyo mke, wanasahau nyumba ni baba na mama na mama ndo msimamizi wa mambo pale nyumbani.
Sasa kuishi na mtu asiyefuata taratibu zenu, atakapokosea mke lazima aseme hapo ndipo chuki huibuka, mwingine hata kazi hashiriki atayakalisha atake kutengewe hadi maji ya kunawa nani anataka shida hizi?
Baadhi yao umbea, na majungu kutwa kuchonga maneno au kuoeleka maneno ya uongo kwa wakwe kuwa mke hivi mke vile nani anataka shida hizi?
Bahati mbaya ndugu wa mume anapokosea hawataki kuambuwa, hii nayo huleta vurugu, haiwezekani mke apelekwe kwenye nyumba yake.....
Na wanaume mna tatizo la kutotatua matatizo ya ndugu zenu, mnajifanya kama hamuyaoni, mkiyaona mnamwambia mke avumilie mkeo ana moyo wa chuma?
Nikija kwa ndugu wa mke, mke ni rahisi kudhibiti nduguzake, na ndugu ni wasikivu kwa mume maan hawatzki kuharibu, ndo maana huwa rahisi kuishi nao.
Nasisituza kama hakuna umuhimu wa kuishi na ndugu wa upande wowote heri muishi wenyewe, pelekeni msaada huko waliko... Maana kaka zetu ndugu zenu wengine wanataka kushindana na mke ndani, mke akipata wax watataka na ndg yao awanunulie wax la sivyo midomo juu.....