Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Nipe kalamu nishike, hoja zangu niandike,
Nipe nami nisikikike, walimwengu wapilike,
Mnipe niliandike, na hili lifahamike,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kapigwa mtu kikumbo, mke kaachia nyumba
Kalia bwana Mahimbo, kwa jaji kenda kuomba
Akatungia na wimbo, kamshinda hata Komba,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kaja dada Josephina, kamuaga kwa kuzira
Mumewe akamnuna, na kusema kwa hasira,
Huyo mama akanena, pamekuwa na ukora,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kibanda nakuachia, baba nanii naondoka,
Huku mama analia, na mizigo ameshika,
Kwangu nakukimbilia, kwako hapa nimechoka,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!
Kaenda alikokwenda, maisha kuyaanzia,
Akataka pa kupenda, na moyo kutulizia,
Kampata wake nyonda, zilipendwa kaachia,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!
Mtu kumwacha mwenziwe, huyo anayo sababu,
Kulazimisha isiwe, ni mwanzo kupata tabu,
Kamwe mgonjwa usiwe, nenda upate tabibu,
Mke kukimbia nyumba si wizi ni kuzidiwa!
Kaondoka ana kisa, si letu hilo ni lao,
Kumhukumu mkosa, ati kaacha mbachao,
Vikizidi vinatesa, mtu hurudia kwao,
Mke kukimbia nyumba, si ziwi ni kuzidiwa!!
Ukimtenda mwenzio, wengine wanangojea,
Mnyanyase na vilio, wapo wanaoombea,
Wawe ndio kimbilio, ndio wenza wagombea,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!
Ukiwa naye mwandani, mpende akakupende,
Simfanye kisirani, mtoto wa watu akonde,
Utenda mahakamani, ati jaji akulinde,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!
Utadai bilioni, ati mke umeporwa,
Kakuaga hadharani, hakusubiri kuparwa,
Watakucheka watani, umezidiwa hujaporwa,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa.
Natama ninatuwama, wa kijiji nimesema,
Shujaa amesimama, kapendwa na huyo mama,
Haki yako kulalama, lakini kwanza tazama,
Mke kukimbia nyumba si wizi ni kuzidiwa!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Nipe nami nisikikike, walimwengu wapilike,
Mnipe niliandike, na hili lifahamike,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kapigwa mtu kikumbo, mke kaachia nyumba
Kalia bwana Mahimbo, kwa jaji kenda kuomba
Akatungia na wimbo, kamshinda hata Komba,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kaja dada Josephina, kamuaga kwa kuzira
Mumewe akamnuna, na kusema kwa hasira,
Huyo mama akanena, pamekuwa na ukora,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!!
Kibanda nakuachia, baba nanii naondoka,
Huku mama analia, na mizigo ameshika,
Kwangu nakukimbilia, kwako hapa nimechoka,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!
Kaenda alikokwenda, maisha kuyaanzia,
Akataka pa kupenda, na moyo kutulizia,
Kampata wake nyonda, zilipendwa kaachia,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!!
Mtu kumwacha mwenziwe, huyo anayo sababu,
Kulazimisha isiwe, ni mwanzo kupata tabu,
Kamwe mgonjwa usiwe, nenda upate tabibu,
Mke kukimbia nyumba si wizi ni kuzidiwa!
Kaondoka ana kisa, si letu hilo ni lao,
Kumhukumu mkosa, ati kaacha mbachao,
Vikizidi vinatesa, mtu hurudia kwao,
Mke kukimbia nyumba, si ziwi ni kuzidiwa!!
Ukimtenda mwenzio, wengine wanangojea,
Mnyanyase na vilio, wapo wanaoombea,
Wawe ndio kimbilio, ndio wenza wagombea,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!
Ukiwa naye mwandani, mpende akakupende,
Simfanye kisirani, mtoto wa watu akonde,
Utenda mahakamani, ati jaji akulinde,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa!
Utadai bilioni, ati mke umeporwa,
Kakuaga hadharani, hakusubiri kuparwa,
Watakucheka watani, umezidiwa hujaporwa,
Mke kukimbia nyumba, si wizi ni kuzidiwa.
Natama ninatuwama, wa kijiji nimesema,
Shujaa amesimama, kapendwa na huyo mama,
Haki yako kulalama, lakini kwanza tazama,
Mke kukimbia nyumba si wizi ni kuzidiwa!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)