Mke kubadili jina la ukoo baada ya kuolewa!

Lizzy nilipo oa nilimuomba mwenzangu abadili jina akagoma, nimuacha wala sikumlazimisha. Bahati nzuri nikapata kazi nje ya nchi akatakiwa aombe ruhusa ya kazini kwao ili aje anitembelee. Aliambiwa hujaolewa na kama umeolewa kwa nini unatumia jina hili? kama unataka ruhusa basi fanya utaratibu wa kubadili jina. Ilibidi aombe kubadilisha jina. Akapewa ruhusa. Alipofika huku ilibidi nimuombee health insurance akaambiwa utafuata jina la mumeo hata kama kwenye passport yako unatumia la baba yako maana ndiye anakatwa kwenye mshahara wake. Pia kazini kwangu nilipowasilisha document zake za kumuongeza kama dependant wangu walikataa kusajili jina lake. Ikabidi tutumie la kwangu ndiyo mambo yaende sawa kwa ujumla ulikuwa sumbufu moja kwa moja. Yeye mwenyewe alikili kuwa alilazimisha kitu bila kujua madhala yake. Kwa Ushauri tuu LIZZY jaribu kuwa mpole.

Mhhhh sijawahi kuona au kusikia usumbufu wa aina hiyo kwasababu tu mtu anatumia jina lake badala ya la mume!!Kwani hamna vyeti vya kuonyesha kwamba kweli mmeona???Sijui mtu akiolewa zaidi ya mara moja atabadili jina mara ngapi!!!
 
Mkuu unless yupo kwenye nchi za kiarabu which am not sure na sheria zao.., lakini majority ya nchi you cant force mtu kutumia jina fulani.. thats why nimetoa mfano wa Dr. kwenye post #34 kwamba huyu dada atakuwa amejenga jina lake kwa muda mrefu kwahiyo kubadilisha litakuwa na effect kwa kazi yake...

Think about this Leo ukimuoa Whitney Houston utataka abadilishe Jina aitwe Whitney Wakumwitu... huoni kwamba hii itamuaffect kwenye biashara yake?

Mkuu sipingani na ww hata kidogo. Ila nimeeleza tuu yaliyonikuta. Kwa upande wangu sikuona big deal na ndiyo maana sikulazimisha. Na wala sikuchukua efforts zozote kujua kwa nini kazini walilazimisha atumie jina langu. Kingine pia kumbuka hata cheti cha ndoa huwa kinataja jina lake na ukoo wake... na mwanaume pia jina lake na ukoo wake. Hivyo hayo mengine labda tuwaulize wanasheria kuna impact gani ya kubadilisha ama kutobadilisha sheria.
 
Mhhhh sijawahi kuona au kusikia usumbufu wa aina hiyo kwasababu tu mtu anatumia jina lake badala ya la mume!!Kwani hamna vyeti vya kuonyesha kwamba kweli mmeona???Sijui mtu akiolewa zaidi ya mara moja atabadili jina mara ngapi!!!

Hata mimi hilo swali silijui mkuu. unapo muandikisha mkeo kuwa dependent wako lazima uwakilishe na vyeti na wao wanatoa Index number kwa kila mwana familia. Ambayo inakuja na jina la kila muhusika, suprisingly pamoja na kuweka jina la my wife na ubini wake wao walileta index number ikiwa na jina lake la mwanzo na ubini wangu.
 
Mkuu sipingani na ww hata kidogo. Ila nimeeleza tuu yaliyonikuta. Kwa upande wangu sikuona big deal na ndiyo maana sikulazimisha. Na wala sikuchukua efforts zozote kujua kwa nini kazini walilazimisha atumie jina langu. Kingine pia kumbuka hata cheti cha ndoa huwa kinataja jina lake na ukoo wake... na mwanaume pia jina lake na ukoo wake. Hivyo hayo mengine labda tuwaulize wanasheria kuna impact gani ya kubadilisha ama kutobadilisha sheria.

It sounds well to speak from your experience. Kwa utamaduni tulionao sasa ni kwamba mwanamke akiolewa anahamia upande wa mwanaume na anapata huduma zote kutoka huko hata akifa, hivyo ndio maana kuna sehemu zinasisitiza utumie jina la mwanaume. Sasa kama kuna watu wanaona ni aina fulani ya udhalilishaji kwa mwanamke basi wabadilishe watakavyoona inafaa, ila kwa mimi sioni ubaya wowote
 
Kwangu mimi naona haina umuhimu na kuna baadhi ya kazi inabidi utumie jina lako kamili bila ya mume, na vile vile kuna baadhi ya kazi lazima ubebe jina la mume.
Binafsi sitabeba jina la mtu niliejuana nae ukubwani kisa cha kukana wazazi wangu ebo!

Ukikua utaafikiria upya, subiri muda ufike! kumbe bado!!!hahah
 
1.Hakuna umuhimu wa kubadili jina,hatuunganishwi kwenye ndoa na majina,mwanamke aamue mwenyewe atakalo.
2.Hakuna madhara usipobadili jina kwa kiasi kikubwa ukiacha lile la identity.
 
Du! Mi nafkiri mke kubadili jina ni suala kuonyesha wamekuwa kitu kimoja.Kuna watu wanadai kama ndivyo kwann wanaume wasitumie majina ya upande wa wake,nafkiri ni suala la utaratibu tu hata hivyo baadhi ya nchi wamekwenda mbali zaidi, niliwahi kuwa Japan kwa muda mfupi wao sheria yao ya ndoa inawalazimisha once wanapooana mke lazima abadili atumie surname ya mumewe. Nafikiri usumbufu kama baadhi ya wadau waliousema hapo juu ukizidi sio ajabu sheria ya ndoa Bongo ikabadilishwa ku-accomodate hilo. Mkubali msikubali kubadili jina muhimu
 
Mi sijabadili wala nini nimebakiza hospital na kwenye passport ila pia passport inasumbua naposafiri kikazi maelezo marefu sana inasumbua mmno
 
Kwa kweli sioni umuhimu wa kubadili jina, kama kweli tunapendana jina haliwezi kutoa mchango wowote, kila mtu abakie tu na majina yake.
 
Ni mila na tamaduni kwani mwanamke anapo olewa huhukuliwa amesha kuwa moja ya ukoo wa mwanaume ndiyo maana baadhi ya makabila yalikuwa hayawasomeshi wanawake kwa kuogopa kuwa wafaidisha waoaji na kuna makabila mwanamke akisha olewa hata kuzikwa hatozikwa nyumbani kwa kwao ila atazikwa nyumbani kwa mmewe...

sasa hayo mamila na matamaduni ya longi unayaongelea ya nini tena, umeshasema zamani, sasa hivi haiko hivyo tena
 
Du! Mi nafkiri mke kubadili jina ni suala kuonyesha wamekuwa kitu kimoja.Kuna watu wanadai kama ndivyo kwann wanaume wasitumie majina ya upande wa wake,nafkiri ni suala la utaratibu tu hata hivyo baadhi ya nchi wamekwenda mbali zaidi, niliwahi kuwa Japan kwa muda mfupi wao sheria yao ya ndoa inawalazimisha once wanapooana mke lazima abadili atumie surname ya mumewe. Nafikiri usumbufu kama baadhi ya wadau waliousema hapo juu ukizidi sio ajabu sheria ya ndoa Bongo ikabadilishwa ku-accomodate hilo. Mkubali msikubali kubadili jina muhimu

Muhimu kwa nani? hiyo yote naona nikutojiamini kwa mwanaume, hivi tulipendana wakati nina majina yangu, umenioa, bado tu hujiamini unataka nibadili na jina, basi ndoa za watu ambao wake wamebadili majina zingekuwa hazivunjiki, mbona tunashuhudia nyingi tu zinakwenda hovyo. Mi naona la la msingi kama mdada mwenyewe anapenda na abadili lakini isiwe lazima maana umuhimu si uoni hapo!
 
Kama unamopenda kweli akakuomba kwa nini usikubali? Mpe sababu zinazoeleweka si ugomvi.
Je uko tayari suala la jina liwafarakanishe mpaka kuvunjika kwa ndoa?

Hivi kweli kwa mwanamume ambaye ananipenda kwa dhati jina si Tatizo. kwani jina lina nafasi gani katika uhusiano?
 
Ila ikitokea mtu kabadilisha jina haf wakatengana na mumewe inakera kweli hasa kwa kina mama wanaofanya kazi. Nimeshawahi kuwashuhudia kina mama watatu mmoja akiwa ndugu wa karibu.

Kwa kweli baada ya kutengana na waume zao waliendelea kuyapata machungu ya kutengana kwa kuendelea kuyatumia yale majina. Kuna mwingine alikuwa hataki hata kulisikia lile jina na hali kwenye document zake kazini ndo linatumika. Kwa hiyo mama anabaki kwenye matatizo ya kisaikolojia tu.
 
Back
Top Bottom