MKE Ana Tamaa!

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,408
Juzi nilipokuwa na mke wangu baada ya chakula cha usiku, aliniambia
nimwandikie nyumba yangu kwa jina lake, na hii nyumba ninayo kabla hatujafunga
ndoa, nikamuuliza kwani kuna tatizo gani ikiwa kwa jina langu. Akaniambia kuwa yeye
amezoea kwao, yaani baba yake kila anaponunua nyumba au gari anaandika kwa jina la
mamake.Nikamwamwambia nipe muda nifikiri, na leo kanikumbushia tena. Sasa nimeona
hii issue niilete hapa jamvini ili mnipe ushauri wenu wa busara...
 
Ushauri wangu ni: 1.Usiandike, hiyo ni mali aliyokukuta nayo; inaonekana ana tamaa na mali na siku ukichacha anakuacha na nyumba anachukua.
2. Kama utaamua kuandika; mwambie muandikishiane mukataba; kwamba jina lake litatumika tu wakati wa uhai wa ndoa; kama itavujika pia na
uhalali wa jina lake utakua umekoma. Kama mauti yatakufika pia mukataba huo useme warithi wa nyumba hiyo ni watoto wako.
 
Juzi nilipokuwa na mke wangu baada ya chakula cha usiku, aliniambia
nimwandikie nyumba yangu kwa jina lake, na hii nyumba ninayo kabla hatujafunga
ndoa, nikamuuliza kwani kuna tatizo gani ikiwa kwa jina langu. Akaniambia kuwa yeye
amezoea kwao, yaani baba yake kila anaponunua nyumba au gari anaandika kwa jina la
mamake.Nikamwamwambia nipe muda nifikiri, na leo kanikumbushia tena. Sasa nimeona
hii issue niilete hapa jamvini ili mnipe ushauri wenu wa busara...

Don't be stupid my friend. Wakati una pewa mapenzi moto moto huta ona athari zake lakini baadae utaona hasara yake. Sioni mantiki ya kumuandikia hiyo nyumbani kwa jina lake especially kama kakukuta navyo. Hiyo story ya baba ake ina weza kuwa uongo na hata kama ni ukweli wewe haikuhusu. Je na wewe ukimuambia kwenu umezoea mali zote zinaandikwa kwa jina la baba?

Ushauri wa bure....don't discuss matters like this right after sex or foreplay b'cause your head won't be thinking straight.
 
Dah! hapa kuna tatizo lazima atakuwa anafikiria kukuacha in long run ndio maana anademand aandikwe yeye fine enough tayari nyie ni
mke na mume vitu vyote vyenu sasa anataka kuleta experience ya kwao wakati baba yake alikuwa mdogo kama piriton kwa mama yake
hii aikubaliki kabisa lazima huyo atakuwa wife about a time
 
Naona kama huenda hakushiba vizuri chakula cha usiku.Kwani alikula nn siku hiyo tofauti na siku nyingine.She is very smart, just after food!.Mwambie aache tamaa, mkioana wawili ana kuwa mmjo.
 
Juwa makini sana boflo na huyo mwanamke. usithubutu kumwandika yeye na asikuletee mambo ya baba yake ndani ya nyumba yako.
 
Dah! Una mtihani mkubwa sana ila unatakiwa kuwa makini kwani SHE IS AFTER MONEY SO BE CAREFULLY.
 
Mpige marufuku kuendelea na kauli za kijinga hizo, otherwise she 's going to continue buzzing you all the way!.Maambo ya kwao analetaje kwenu babaake?..kwani hakuaga kwao kwamba anakuja kwako kuanzisha familia mpya yenye sheria zake?....Ukicheka nae umeuwawa babaake!
 
ndugu yangu ktk maisha yako yote usijaribu ata cku moja kufanya kitu kama icho
awa watu sio wakuchukulia kiivyo'mwambie izo ni sheria za kwa babaake apo ni
kwako na una taratibu zako ambazo yeye anatakiwa azifuate.
 
mpaka anakwambia hayo ujue something is very wrong my broda!
ushauri wangu mwambie serikali ya baba na mama yake ni tofauti na yako na yeye!
ukifikiria vizuri lazima upate woga sbb nina uhakika kabisa anachosubiri ni apate tu hiyo nyumba kisha akutimue,maana mwanamke mwenye mapenzi ya dhati anajua cha mumewe ni cheke,sasa huyu haridhiki hadi jina la nyumba liwe lake,why?tafakari vizuri.
-- jiweke sana karibu na mungu maana binadamu unayeshea naye hadi kitanda hashindwi hata kukufanya ukubali kwa nguvu za giza!
 
Kama unazo pesa kamnunulie nyumba ingine... Is she a housewife? do u have any kids? I think she has right to worry about her future? what if you die tomorrow? where will she go? if she dont work or have any other income and she has spent all her life taking care of u, u should take care of her too...

au mdaganye kama wanavyo danganya wenzako.... Everything I own is yours my love, do u know how much i Love u? :blah: nyie wanaume ndo mnajua kudanganya
 
hapa inweza kuwa jamaa hujasoma wasi wasi wa mkeo vizuri
pengine kuna mtu keshamwambia kuwa 'kaka yetu kakuoa huna kitu tutakurudisha kwenu na begi moja tu' nae ameingia na wasi wasi

mpende mkeo useme nae taratibu kwa sababu labda anajali kuhusu future yake hasa kama yeye ni mama wa nyumbani au kama pesa anayoipata yote anatumia kushughulikia familia na hana extra ya kufikiria wewe utakapoondoka duniani.

if u have the money, japo kama si nyumba, muweke investment katika kitu ambacho kitakaa...japo kiwanja, ambacho waweza kukiandikisha kuwa ukiondoka duniani kabla yake itakuwa mali yake
 
Mkuu.naona hapo kunamgogoro unafukuta ndani kwa ndani.Huyo mamaa kisha pata Walimu wanaompampu, angaria Mkuu.UTA LALA INJE KM MBWA KOKO.Jambo la mhimu mwambie afute kauli yake.pia nakuhakikishia hamtaweza kukaa kwa AMANI NA MKEO KUANZIA SASA.duh Basi Omba MUNGU KILA MARA ILI AKUEPUSHE NA BALAA ZAIDI.
 
Kama unazo pesa kamnunulie nyumba ingine... Is she a housewife? do u have any kids? I think she has right to worry about her future? what if you die tomorrow? where will she go? if she dont work or have any other income and she has spent all her life taking care of u, u should take care of her too...

au mdaganye kama wanavyo danganya wenzako.... Everything I own is yours my love, do u know how much i Love u? :blah: nyie wanaume ndo mnajua kudanganya
Hapo ndipo mie Baadhi ya mambo yananishinda,Yaani wewe ni mke wangu,nyumba ninayo na tunaishi wote humo ndani ,.halafu yanaanza mambo eti nimnunulie wife nyumba yake?Does it make sense?kuna haja gani iwapo tunaishi pamoja,.mwanamke afikirie future yake ,ndio nimnunulie nyumba?future gani tena kama sio tamaa?Kama hana mpango wa kukukimbia je atakuwa na upi mwingine?Kama mama mambo yake yamekaa vizuri anataka kununua/kujenga nyumba nyingine,.basi iwekwe bayana nia yakufanya hivyo ni nini?Kama ni ya biashara basi najua pia watoto watanufaika,.nami nitatoa hata kidogo nilichonacho kuchangia,kama ni kurekebisha makazi ya wazazi wa mmoja wetu basi ielezwe hivyo na nitachanga.,na hizo hati ziwaendee wazazi wenyewe.
Kama mke alikuwa ana nyumba yake kabla ya ndoa na mie ninaishi humo,basi nikipata uwezo nitajenga nyingine huku akijua ninalofanya ,na hiyo ni ya watoto wala sio yangu.Maisha gani ya ndoa yaliogubikwa na wasiwasi wa kuachana.
Wote tunaishi pamoja ndani ya ndoa alafu unaanza mambo ya nikuandikie urithi ,wa nyumba wakati bado nipo hai,we vipi una mpango wa kunipaisha..watu wengine sijui wanawaza nini,nikikuandikia halafu ukitangulia wewe mbele ya haki?Hiyo nyumba mnayoishi sasa mbona tayari ni urithi automatic sasa kuna haja ya kuuomba tena kwa maandishi mhh…
Natishika na mawazo mengine lol.
Vitu kama gari ,kumnunulia sikatai kabisaa.,ni uwezo tuu.
 
Hahahaha,

Kweli kwa mipigo hii unaweza kutushangaa tukikataa kuoa?
 
sidhani hilo neno huyo mwanamke kalitoa tu abruptly...nadhani amesha sense kuwa ndoa yenu iko ukingoni/imekufa...labda wewe tu ndio unakuwa mzito kuliona hilo!...mpk mtu kukutamkia wazi..itakuwa mliishi akiamini wewe ni selfish hakuna chochote chenu pamoja!vyote ni vyako...dada wa watu yuko desperate..anaona ataambulia patupu...kama bado unampenda...jitahidi uifufue ndoa yenu na ujitahidi kumbadilisha kifikra kuwa vyote mnavyofanya/mlivyonavyo ni vyenu pamoja, na watoto wenu....
 
Huyo ni mkeo! atakacho mpe so long as ni mkeo mridhishe mridhishane. maisha mafupi haya kuleni raha pamoja...huoni raha mtu akisema nyumba yangu hii? let her have one so that her love should not grow cold......!
nimempenda huyo mke .....badala ya kwenda kwa kalumanzila kaamua kukupa black and white of her heart.....mwambie nakupenda mke wangu !
 
Kaka huna mke, ningemuelewa iwapo angesema anataka na jina lake liwemo ktk hati ya nyumba.
 
Yaani ghafla ghafla tu hivyo? Mhh,sasa kama kakukuta nayo mbona anataka wewe uandike kwa jina lake mkuu?

Hebu ongea nae tu vizuri bila kumuonyesha kwamba umemgundua kuwa na tamaa.Mwambie huoni sababu kwa nini jina libadilike,nyumba ni yako na mnaitumia kwa manufaa yenu wewe na yeye pamoja na watoto wenu.Sasa hii haki ya kubadili jina anaitoa wapi?na wewe mwambie umezoea baba yako huwa anaandika mali zake kwa jina lake,full stop

Sijui huwa anakuwa katika mazingira gani wakatia akitoa mapendekezo kama hayo
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom