Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,111
Mwanamke mmoja nchini Malaysia ameamua kuomba talaka kumkimbia mume wake ambaye anapenda sana kufanya mapenzi akimlazimisha kufanya mapenzi zaidi ya mara 10 kila siku. Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 18 ambaye aliolewa hivi karibuni ameamua kumkimbia mumewe na kudai talaka baada ya kuchoka kufanya mapenzi na mumewe zaidi ya mara 10 kila siku.
Mwanamke huyo anadai mumewe atakuwa anatumia uchawi au madawa katika kufanya mapenzi kwani si hali ya kawaida mwanaume kufanya mapenzi mara nyingi kiasi hicho bila kuchoka.
Mwanamke huyo amepeleka madai yake ya talaka kwenye mahakama ya sharia za kiislamu nchini humo.
"Mwanamke huyo alianza kushangazwa na mumewe kwenye usiku wa kwanza wa honeymoon yao wakati mumewe alipolazimisha na kufanya naye mapenzi mara 17" alisema mwenyekiti msaidizi wa taasisi ya wanasheria wa sheria za kidini, Musa Awang.
Mwanamke huyo alidai kuwa mumewe atakuwa na shetani aliyejificha katika mwili wake.
Akizungumzia kauli hiyo, kiongozi wa kidini Datuk Ebu Hasan alisema kuwa "Ni mwanaume anayeshirikiana na shetani kufanya mapenzi pekee ndiye anaweza kufanya mapenzi mara nyingi kiasi hiki".
Mahakama ya sharia bado haijatoa uamuzi wake katika kesi hiyo ya aina yake.
Chanzo: nifahamishe.com
Mwanamke huyo anadai mumewe atakuwa anatumia uchawi au madawa katika kufanya mapenzi kwani si hali ya kawaida mwanaume kufanya mapenzi mara nyingi kiasi hicho bila kuchoka.
Mwanamke huyo amepeleka madai yake ya talaka kwenye mahakama ya sharia za kiislamu nchini humo.
"Mwanamke huyo alianza kushangazwa na mumewe kwenye usiku wa kwanza wa honeymoon yao wakati mumewe alipolazimisha na kufanya naye mapenzi mara 17" alisema mwenyekiti msaidizi wa taasisi ya wanasheria wa sheria za kidini, Musa Awang.
Mwanamke huyo alidai kuwa mumewe atakuwa na shetani aliyejificha katika mwili wake.
Akizungumzia kauli hiyo, kiongozi wa kidini Datuk Ebu Hasan alisema kuwa "Ni mwanaume anayeshirikiana na shetani kufanya mapenzi pekee ndiye anaweza kufanya mapenzi mara nyingi kiasi hiki".
Mahakama ya sharia bado haijatoa uamuzi wake katika kesi hiyo ya aina yake.
Chanzo: nifahamishe.com